mpinga shetani
JF-Expert Member
- Nov 22, 2010
- 3,234
- 959
Ujumbe huu unasambazwa na MWALIMU mmoja aliyepata Shock baada kumsikiliza Kikwete
NITAFICHA WAPI USO WANGU KWA ALIYOSEMA RAIS?
Rais profesa Jakaya Mrisho Kikwete ameishukuru serikali ya Ujerumani kwa kututawala na kutuletea maendeleo wakati wa ukoloni. Akizungumza mbele ya waandishi wa habari ikulu leo alimuambia rais wa Ujerumani kwamba wakati wanatutawala walitufanyia mambo mengi sana mazuri ikiwemo kutujengea jengo la ikulu.
Rais ameniumbua.Sijui nitaficha wapi uso wangu. Tangu mwaka 2008 nimekuwa nikiwafundisha wanafunzi wangu historia huku nikiwaaminisha kwamba wakoloni hawakuwa na nia njema.Niliwaambia wakoloni walikuwa wakitunyonya, wa kitukandamiza na kutudhalilisha. Niliwaambia hata elimu waliyoitoa na miundombinu waliyojenga ilikuwa ya kuendeleza unyonyaji.
Niliwaambia wanafunzi wangu kuwa watu waliowapinga wakoloni na kuwapiga vita kama kina Mkwawa ndio mashujaa wetu.Niliwasema vibaya wakoloni huku nikitumia vitabu vya kina Walter Rodney kama HOW EUROPE UNDERDEVELOPED AFRICA na kunukuu sehemu ya The Dar es salaam School of thought kuaminisha wanafunzi wangu kwamba wakoloni hawakutufaa.
Leo rais kaniumbua.Kama wanafunzi wangu wamemsikiliza rais nitakoma.Lazima watamuamini kwa sababu rais wetu ni profesa. Forwarded as received..
NITAFICHA WAPI USO WANGU KWA ALIYOSEMA RAIS?
Rais profesa Jakaya Mrisho Kikwete ameishukuru serikali ya Ujerumani kwa kututawala na kutuletea maendeleo wakati wa ukoloni. Akizungumza mbele ya waandishi wa habari ikulu leo alimuambia rais wa Ujerumani kwamba wakati wanatutawala walitufanyia mambo mengi sana mazuri ikiwemo kutujengea jengo la ikulu.
Rais ameniumbua.Sijui nitaficha wapi uso wangu. Tangu mwaka 2008 nimekuwa nikiwafundisha wanafunzi wangu historia huku nikiwaaminisha kwamba wakoloni hawakuwa na nia njema.Niliwaambia wakoloni walikuwa wakitunyonya, wa kitukandamiza na kutudhalilisha. Niliwaambia hata elimu waliyoitoa na miundombinu waliyojenga ilikuwa ya kuendeleza unyonyaji.
Niliwaambia wanafunzi wangu kuwa watu waliowapinga wakoloni na kuwapiga vita kama kina Mkwawa ndio mashujaa wetu.Niliwasema vibaya wakoloni huku nikitumia vitabu vya kina Walter Rodney kama HOW EUROPE UNDERDEVELOPED AFRICA na kunukuu sehemu ya The Dar es salaam School of thought kuaminisha wanafunzi wangu kwamba wakoloni hawakutufaa.
Leo rais kaniumbua.Kama wanafunzi wangu wamemsikiliza rais nitakoma.Lazima watamuamini kwa sababu rais wetu ni profesa. Forwarded as received..