Kikwete aendelee muhula mwingine

Msimamo wako haueleweki. Kumbuka muda mfupi uliopita kuna mahali umetoka kuandika hivi:

Mara zote unatakiwa upime ,sio unafuata upepo ,kwa kuwa tu watu wanapiga mayowe pale bungeni ukaona ndio hao wa kufuatwa ,kumbe athari za mwezi mchanga zinawapa shida.

Sekunde moja ni kubwa ikiwa wewe ndio mwenye kura ,hivyo mimi kama raia wa kawaida ninacho ringia ni kura yangu ,nitaipeleka pale ambapopana matumaini ,hadi hapa nikwambiapo au niandikapo basi bado matumaini yapo CCM kuliko kwengine kokote kule ,mwendo wa CCM wa mwezi au mwaka jana sio huu tulio nao.

WaTanzania wengi wataturn katika siku sijazo siku ambazo MTanzania ataanza kufungua macho kutokana na juhudi za Makusudi za Mheshimiwa JK. Tusidanganyane huko kwenye makaki amna kitu.
 
Koma kama ulivyokoma kunyonya ziwa la mama yo JK hafai haijapata kutokea Raisi aliyeshindwa kuongoza nchi kama huyu embu usitufanye tuje tupasuke mioyo

Hivi wewe unamimba naona hasira njenje ! Kama KJ ameshindwa angelikwisha kujiuzulu zamani ,huyu JK si nahoza anaebabaika na mawimbi,ni katika wale manahoza waliovuka maji ya shingo. Na ndio hivyo anayavuka ,sasa mtu kama huyu ndie kiranja anaeweza kuiongoza Tanzania bila ya kukwaruzana.
 
Du! Wakati rada zinaonesha kuwa raisi atakayetangulia kusalmiana na Mzee (Mwalimu) Nyerere pale 'Butiama'
kati ya wastaafu wote ni Kikwete?

Naamini kabisa huyu jamaa anamuelekeo wa kuifikisha Tanzania pale inapotaka kwenda,utendaji wake na serikali uliopo hivi sasa inaonekana ulichelewa ,lakini kasi ya maendeleo ambayo inaonekana kila pembe ya Tz ni wazi kuwa Tanzania imepata kiongozi mwenye upendo na wananchi wake.

WaTanzania hawana budi kumpa tena muhula wa uongozi kwa miaka kumi mingine.Huku tukisubiri Katiba mpya au Tanganyika mpya.
 
Naamini kabisa huyu jamaa anamuelekeo wa kuifikisha Tanzania pale inapotaka kwenda,utendaji wake na serikali uliopo hivi sasa inaonekana ulichelewa ,lakini kasi ya maendeleo ambayo inaonekana kila pembe ya Tz ni wazi kuwa Tanzania imepata kiongozi mwenye upendo na wananchi wake.

WaTanzania hawana budi kumpa tena muhula wa uongozi kwa miaka kumi mingine.Huku tukisubiri Katiba mpya au Tanganyika mpya.

Urais wa Tanzania siyo Tendo la ndoa useme mtu atafika mara nyingi anavyotaka!..
Damn!
 
Mie nadhani tungerudisha ruksa miaka 5 kisha mr. clean aje ajenge misingi tena kwa miaka 5..... Halafu Jk aisimamie kama ilivyo sasa...........au tuunganishe vyama vyote vya kisiasa. ........ha ha ha..
 
Naamini kabisa huyu jamaa anamuelekeo wa kuifikisha Tanzania pale inapotaka kwenda,utendaji wake na serikali uliopo hivi sasa inaonekana ulichelewa ,lakini kasi ya maendeleo ambayo inaonekana kila pembe ya Tz ni wazi kuwa Tanzania imepata kiongozi mwenye upendo na wananchi wake.

WaTanzania hawana budi kumpa tena muhula wa uongozi kwa miaka kumi mingine.Huku tukisubiri Katiba mpya au Tanganyika mpya.

Labda akagombee urais Zanzibar 2015 awe rais wa Tanzania Visiwani.... LOL!
 
Vichaa vingine havina dawa. Mwiba unaishi wapi iwapo unaona makengeza kwa mpendwa wako ambaye licha ya kuchokwa na wananchi amejichoka hata yeye mwenyewe. Huenda nawe ni wale wanaofakamia mabaki na kunenepeana kiasi cha kupofuka na kudhani wote wanaishi kwa vinono kama wewe. Siku moja utaujua ukweli hata kama utakuwa umechelewa. Ila usiwe wa kwanza kulalama.
 
Naamini kabisa huyu jamaa anamuelekeo wa kuifikisha Tanzania pale inapotaka kwenda,utendaji wake na serikali uliopo hivi sasa inaonekana ulichelewa ,lakini kasi ya maendeleo ambayo inaonekana kila pembe ya Tz ni wazi kuwa Tanzania imepata kiongozi mwenye upendo na wananchi wake.

WaTanzania hawana budi kumpa tena muhula wa uongozi kwa miaka kumi mingine.Huku tukisubiri Katiba mpya au Tanganyika mpya.
hahaaa mweee ...asante Mwiba kwa kunichekesha leo ...mungu akupe maisha marefu uelendelee kutuchekesha hivi hivi

Ndio maana ukikosekana hapa ninakumiss sana Mwiba, post zako zina akili sana

Inawezekana Mwiba ameamua kuleta ujumbe kwa njia hii ya kuudhi/ kuchekesha watu kulingana na vipi unaichambua mada yake.

Nililoliona mimi, sijui kama amekusudia hivyo au la, ni ujumbe uliomo katika hayo maandishi mekundu.
Kuna uwezekano mkubwa sana kuwa Katiba Mpya isiwe tayari itakapofika 2015.

Baada ya kazi ya usanii wa ukusanyaji maoni unaofanywa na Tume ya Warioba na ukamilishaji wa uchambuzi wa maoni hayo hadi kufikia kuandika katiba mpya ya Muungano imesemwa itafika 2014.

Kama Rasimu hiyo ya Katiba Mpya ya Muungano itapelekwa kupigiwa kura na pande mbili za muungano. Ni wazi matakwa ya UAMSHO kama hayakutimizwa katiba hiyo haitakubaliwa/ haitapitishwa na wananchi wa huko na hivyo kupelekea 2015 inaingia na uchaguzi mkuu ukiitishwa chini ya katiba ya zamani/hii iliyopo. Likitokea hilo sote tunajua nini yatakuwa matokeo ya Uchaguzi huo.

Je Rasimu ya Katiba mpya itakapokataliwa nini kitafanyika kuhusu uchaguzi mkuu? Na kama upande mmoja utakuwa haukupitisha katiba hiyo je Tanzania bara(Tanganyika) itapasa kuandika Katiba yake? (na kinyume chake,ingawaje Zanzibar wanayo katiba yao tayari)

Mada ya Mwiba inaudhi/ inachekesha lakini pia inaibua fikra ambazo wengine hatujazifikiria.

Tujaribu kuzitizama hizo chachu/ Changamoto alizoibua mwisho wa makala yake fupi. Yakitokea hayo, tutafanya nini?
Tutacheka sanaaa? Tutapigana na kuuana? Au tutakuwa wavumilivu na kukamilisha taratibu za kupata Katiba ya Muungano? Kwa kawaida kupata Katiba ya muungano huwa si rahisi (tunaweza kuchukua uzoefu wa kura za kupitisha Katiba ya EU) ...pengine ni wakati sasa kufikiria kuandika sambamba na Katiba ya muungano, Katiba ya Tanganyika..just in case.
Au?
..WaTanzania hawana budi kumpa tena muhula wa uongozi kwa miaka kumi mingine.Huku tukisubiri Katiba mpya au Tanganyika mpya.
 
Naamini kabisa huyu jamaa anamuelekeo wa kuifikisha Tanzania pale inapotaka kwenda,utendaji wake na serikali uliopo hivi sasa inaonekana ulichelewa ,lakini kasi ya maendeleo ambayo inaonekana kila pembe ya Tz ni wazi kuwa Tanzania imepata kiongozi mwenye upendo na wananchi wake.

WaTanzania hawana budi kumpa tena muhula wa uongozi kwa miaka kumi mingine.Huku tukisubiri Katiba mpya au Tanganyika mpya.

Are u mad?
 
Mpe nafasi aiongoze familia yenu,atawaletea maendeleo sana,especialy kama kwenu kuna warembo itakua mpango mzima....
 
Rais KIkwete anastahili pongezi sana especially kwa kutuletea hawa mawaziri wawili ambao ni watendaji sio wanasiasa. Hawa si wengine bali waziri wa Fedha Mgimwa na waziri wa Nishati. Naomba aendelee kuwapunguza wanasiasa na kutuletea watendani ili tuone kasi hii ikiendelea.
 
Makelele yenu mengi kama mnashangilia mpira tena ule wa kupitia redioni uliokuwa ukitangazwa kwenye idhaa ya biashara ya redio Tanzania anao anao goooal,wengi mmezaliwa juzi juzi hamuifahamu hio redio ,amini usiamini hapa JF kuna watu hawaijui senti tano ,ile ya nduaro.

Sielewi kile mnachokipinga kwa JK ,kama ni matatizo mbona yapo mengi tu kwa wengine ,hivi huko kwenye vyama vyenu hakuna matatizo ? Yaani Nyinyi mnaona mkiipata hiiNchi maisha mtayafanya yawe laini kama siagi ,mtapandisha mishahara siku tu mkiingia Ikulu ,hivi mnaota au mshakufa ?

Maendeleo ya JK kwa sasa yapo wazi kabisa ,hivi CCM ianzie tokea Tanu na ASP huko,wameiendesha Nchi hii kutoka kwenye shida na dhiki hadi leo wanaanza kuchimba mafuta na gesi ,itakuwa kosa kubwa sana kwa CCM kuziacha juhudi zake kwa wengine , Ukiangali JK ameweza na amewezesha karibuni itakuwa kila mtu ,WaTz wa leo ni matajiri kila mmoja anamiliki kajisimu cha mobile japo kimeo ,kinaitaji hela au sio ,unakakuta kapofull credit akiitajivocha.

Wengi tu sasa wanamiliki bodaboda na vyombo vya moto vya miguu miwili au mitatu vibajaji, kesho na kesho kutwa kila nyumba itakuwa na gari ndogo nje ,haya yote yamefumka katika kipindi kifupi cha JK.

Ikiwa wewe huoni kama hayo ni maendeleo basi utakuwa maiti inayotembea.

Kwani lazima aendelee kutuongoza? katiba inasemaje na kwanini tuipindue katiba sababu ya JK tu?
 
Back
Top Bottom