Kikosi maalum cha mauaji wakati wa utawala wa Yahya Jammeh wakamatwa na kushtakiwa kwa mauaji

Return Of Undertaker

JF-Expert Member
Jun 12, 2012
4,572
26,868
yemen+pic.jpg



Kwa ufupi
Mpaka sasa maofisa 20 wa Kitengo cha Usalama wa Taifa (NIA) ama wako mahakamani au wanakabiliwa na mashtaka kuhusiana na kifo cha mwanaharakati ambaye alikamatwa wakati wa maandamano.

Banjul, Gambia. Katika utawala wa Rais Yahya Jammeh ilikuwa kawaida kusikia mwanaharakati au mwanahabari au kiongozi fulani wa siasa kauawa na watu wasiojulikana na haukufanyika msako wala uchunguzi.

Mambo yamebadilika, wale watu ambao walikuwa wanadaiwa ‘wasiojulikana’ sasa wanasakwa na wanajulikana. Jumatatu polisi walimkamata ofisa mwandamizi wa intelijensia akihusishwa na mauaji ya mwanaharakati Solo Sandeng Aprili 2016.

Kifo cha mwanaharakati huyo akiwa mahabusu kilichochea vuguvugu la kisiasa ambalo hatimaye lilifanikisha kuuangusha utawala wa miaka 22 wa Jammeh.

Kuteswa na hatimaye kuuawa kwa mwanaharakati huyo aliyekuwa akiongoza chama cha United Democratic Party (UDP) kuliibua maandamano yasiyo ya kawaida ambayo yalihamasisha kambi dhaifu ya upinzani na iliyogawika kuungana dhidi ya utawala wa kidikteta.

Mpaka sasa maofisa 20 wa Kitengo cha Usalama wa Taifa (NIA) ama wako mahakamani au wanakabiliwa na mashtaka kuhusiana na kifo cha mwanaharakati huyo ambaye alikamatwa wakati wa maandamano.

Msemaji wa polisi David Kujabie alisema Jumatatu kwamba Mkuu wa Usalama wa Taifa, James Mendy alikamatwa na polisi na akawekwa kizuizini kwa mahojiano “kuhusiana na kuuawa kwa Solo Sandeng”.

Maofisa wengine tisa wa NIA, akiwemo kiongozi wa zamani, Yankuba Badjie wamefunguliwa mashtaka yanayohusu ushiriki wao katika kifo cha Sandeng. Mchakato unakwenda taratibu: mashahidi 13 wameitwa.

Maofisa wengine wa zamani wa NIA, Ngora Njie na Shiekh Tijan Camara walikubali wiki iliyopita kwamba watakuwa mashahidi upande wa mashtaka.
 
Nikikumbuka Arab spring, ya Zimbabwe na South Afrika na kwingi kwingineko napata matumaini makubwa kwamba Afrika inapiga hatua katika utawala wa sheria na demokrasia!!
 
Wasiojulikana kwa Wananchi tawala ikipita wanajulikana na kupata haki yao kirahisi huwa sio vitu vya kudumu..damu za watu haziendi bure hata siku moja..
 
  • Thanks
Reactions: MTK
Magufuli na makonda mna lakujifunza hapa dunia sio kama mnavyoichukulia View attachment 727920View attachment 727921View attachment 727922
Kwa huyu akitaka ahame hapa bongo kwani hata kwa sumu 2ta muua
yemen+pic.jpg



Kwa ufupi
Mpaka sasa maofisa 20 wa Kitengo cha Usalama wa Taifa (NIA) ama wako mahakamani au wanakabiliwa na mashtaka kuhusiana na kifo cha mwanaharakati ambaye alikamatwa wakati wa maandamano.

Banjul, Gambia. Katika utawala wa Rais Yahya Jammeh ilikuwa kawaida kusikia mwanaharakati au mwanahabari au kiongozi fulani wa siasa kauawa na watu wasiojulikana na haukufanyika msako wala uchunguzi.

Mambo yamebadilika, wale watu ambao walikuwa wanadaiwa ‘wasiojulikana’ sasa wanasakwa na wanajulikana. Jumatatu polisi walimkamata ofisa mwandamizi wa intelijensia akihusishwa na mauaji ya mwanaharakati Solo Sandeng Aprili 2016.

Kifo cha mwanaharakati huyo akiwa mahabusu kilichochea vuguvugu la kisiasa ambalo hatimaye lilifanikisha kuuangusha utawala wa miaka 22 wa Jammeh.

Kuteswa na hatimaye kuuawa kwa mwanaharakati huyo aliyekuwa akiongoza chama cha United Democratic Party (UDP) kuliibua maandamano yasiyo ya kawaida ambayo yalihamasisha kambi dhaifu ya upinzani na iliyogawika kuungana dhidi ya utawala wa kidikteta.

Mpaka sasa maofisa 20 wa Kitengo cha Usalama wa Taifa (NIA) ama wako mahakamani au wanakabiliwa na mashtaka kuhusiana na kifo cha mwanaharakati huyo ambaye alikamatwa wakati wa maandamano.

Msemaji wa polisi David Kujabie alisema Jumatatu kwamba Mkuu wa Usalama wa Taifa, James Mendy alikamatwa na polisi na akawekwa kizuizini kwa mahojiano “kuhusiana na kuuawa kwa Solo Sandeng”.

Maofisa wengine tisa wa NIA, akiwemo kiongozi wa zamani, Yankuba Badjie wamefunguliwa mashtaka yanayohusu ushiriki wao katika kifo cha Sandeng. Mchakato unakwenda taratibu: mashahidi 13 wameitwa.

Maofisa wengine wa zamani wa NIA, Ngora Njie na Shiekh Tijan Camara walikubali wiki iliyopita kwamba watakuwa mashahidi upande wa mashtaka.
 
Tukiweza kuondoa wazungu kwanza katika nchi zetu itakuwa bora zaidi kuliko kuendelea kuwakumbatia wale wanaofadhiliwa na wazungu au wale wanaoharibu aman ya mataifa yetu

wale mnaowaita wana demokrasia wa ulaya ndio hao wanao watafuta wasaliti wao na kuwakea sumu ili waafe

Africa sijui tumerogwa na nani tunaitafuta demkrasia wakat hata familia zetu hatuziongozi kidemokrasia je tutaweza iyongoza nchi iliyochafuka kwa demokrasia let us keep moving
 
Mungu ni zaidi ya watawala. Watawaliwa wakichoka watawala wanabaki kushangaa nakuto amini masikio,macho,fikra zao.
 
Back
Top Bottom