Kikosi Cha mizinga cha (wawami)

Black poison The Factor

JF-Expert Member
May 31, 2020
856
1,262
Wawami ndio akina nani?
Wawami ni kifupi cha wanawake wapiga mizinga. na kuna aina nyingi sana za kikosi hiki cha kupiga mizinga utofauti ni mbinu tu.

Ntaelezea kadhaa nanyie mtamalizia mengine.

1 kikosi hiki ni kile ambacho wanajifanya hawaombi hela ndefu, utasikia baby sikaji kukuomba hela nyingi maana ww bado unajitatfa, mara kalikwenda kakarudi, hawa madau yao ni kati ya 5k Hadi 15k ila ni kila siku.

2 Hawa wanageuza mbinu tu kutoka kikosi cha kwanza, hawaombi mara kwa mara ila siku ya mzinga lazima akili ivibrate mzee alafu ukiona ameanza kupiga simu za ovyo ujue mpango unasukwa, siku ya kukulipua ni kuanzia 200k hadi 500k na hapo ww sio kifaru wala sponsor, ukiwa kifaru au sponsor hapo ni maswala ya kuombwa nyumba na gari.

3 Hawa wanajifanya hawapendi hela ila ni kutuchezea akili tu, hawa ni waomba zawadi utasikia honey sikati hela zako mi niletee zawadi tu, hawa ndo wabaya sasa utatoa zawadi hadi urukwe na akili, jiandae kununua gauni kila wiki viatu t-shirt zote kali na kila atakachopenda hata simu utainunua kwa kigezo Cha zawadi, hivi hizi sio hela au? na usiponunua unakumbishwa my nataka zawadi! We mwehu nini wewe, hapa mchezo ni uleule tu.

4 Hawa ni kama mahakama kwenye kifungu cha vyote kwa pamoja, zawadi utatoa na hela utatoa hawa ndo wauaji kabisa, mizinga mizito iko hapa, toa hela na baadae ulete zawadi yaani mpaka useme.

Kazi kwetu wanaume wanasemaga kupanga ni kuchagua. Kwasasa unatumikia namba ngapi hapo, mi nipo single nimeamua nipumzike kidogo.
 
Back
Top Bottom