kikombe kingine chapatikan mtwara

Smarty

JF-Expert Member
Feb 25, 2011
776
426
jamani hizi njaa zinatupeleka pabaya na hawa viongozi wetu inaonekana ni hopless mandazi. Bibi mwingine yupo mtwara katk kijiji alichozaliwa mkapa naye anagawa kikombe kwa jero jero. Mpaka jioni mtasikia mkuu wa mkoa kanywa, wa wiilya kanywa na wengine wengi tuu. Hv tz tumerogwa! Kuna kipindi hii nchi ilitaka kuongozwa kwa kuskiliza utabiri wa sheke yahaya bahati nzuri hilo likazimwa. Sasa naona ni mwendo wa kikombe. Kwenye mahospitali manesi wanakula shushi wanataka waombe likizo kwa sababu kazi hamna. Poor tanzania.
 
mimi naona hao wote wanaojitokeza kutoa kikombe wapigwe marufuku sasa, na aachiwe babu pekee,
 
Inawezekana Tanzania tukawa na dawa zetu za asili kama inavyotokea sasa na watu wakapona kama inavyotokea sasa,tatizo linakuja pale kila mtu anakuja kwa namna ile ile ambayo wengine wameanza nayo,kwa mimi sikatai kwa hao kutoa tiba ila mazingira yenyewe ya tiba wanazotoa ndio zinanitia shaka.Lakini watu hawa walikuwa wapi siku zote kutoa hivyo vikombe?Au ndio Mungu kaifunulia Tanzania baada ya kuona tupo hoi kwa kila kitu na kuamua kuturehemu na tiba hizi za vikombe?
Mara nyingi huwa naamini kuwa IMANI humponya mtu,inawezekana kabisa mtu akapona kwa kuamini tu kuwa atapona na si kwa sababu ya dawa.
Huu ni wakati wa wizara ya afya kufanya utafiti na wao kuja na dawa yao ili wagonjwa wengi wanaotoroka mahospitalini wabaki na kupata tiba kuliko kwenda kufia njiani wakitafuta dawa.
 
mimi naona hao wote wanaojitokeza kutoa kikombe wapigwe marufuku sasa, na aachiwe babu pekee,

Kwa vigezo vipi? Au unafikiri huyo mungu atamwotesha babu tu? Hiyo roho inayoleta hizo ndoto ndio kwanza inatenda kazi. Huoni yule wa Tabora anavyofanya vitu hadharani halafu mnadai wengine wanafanya mzaha? Kikombe cha mjukuu nacho je? Huoni dogo mpaka kapewa gari na zawadi lukuki kwa kuponya watu? Babu unaye mtetea ana nini cha zaidi? Kweli imeanza kuonekana nanyi mwatafuta namna ya kuikwepa kuficha aibu. Kwamba babu pekee ndiye mwenye hati miliki ya kutibu magonjwa sugu? Face the truth people!

1 Corinthians 2 : 2
For I determined not to know any thing among you, save Jesus Christ, and him crucified
 
Kuibuka kwa Vikombe vipya kila uchao wa kulaumiwa ni SERIKALI. Kwa nini nasema hivyo??? Ni kwa sababu kama Serikali wangelikuwa makini toka siku ya awali Babu alipotangaza kuwa anaweza kutibu magonjwa sugu, serikali ilitakiwa kumpa masharti yafuatayo ili iweze kumruhusu atoe tiba. Masharti yenyewe ni kwanza kutojitangaza kuwa anatibu magonjwa sugu. Pili serikali ingechukua samples ya wagonjwa wote wanaojulikana mfano HIV wagonjwa 5, TB 5, BP 5, Kisukari 5 na kuwapeleka kwa babu kupatiwa kikombe, na kuwarudisha wodini au makwao na kuwafuatilia angalau kwa mwezi mmoja ili kuona maendeleo yao. Kama itaonekana hali zao zinachange to better, basi wangemruhusu babu na vinginevyo wangemfungia. Lakini hilo halikufanyika, matokeo kila uchao wanaibuka wengine. Mfano yule kijana wa Mbeya yeye anasema kabisa kuwa anasaidiwa na wasaidizi wake kichwani (a.ka mashetani) sasa kumwamini mtu kama huyu kwa kweli inatia wasiwasi saana na upeo wa viongozi wetu. Yule mama wa Tabora naye ukimwangalia anavyoombea watu kabla ya kuwapa dawa anachezesha mimacho kama mwenye kifafa, Nashangaa kwa mkuu wa mkoa kama Abeid Mwinyimsa kweli kupewa kikombe na yule mama na akanywa!!! Inatia hofu na sijui Taifa limefikia wapi???
 
Nasema mimi natoka kivyangu kuanzia kesho nawatangazia wa tanzania na ulimwengu kwa Ujumla nimeotesha majuzi
na Malaika mwema niwapatie mateja wote wa Unga,Mirungi,Pombe na Bhangi Glass moja na sio kikombe Napatikana Morogoro
sitoi tiba ya maradhi Sugu
Karibuni
 
Utamsikia mwingine eti kaoteshwa kusaidia wale ambao hawajapta ajira na wale ambao hawajapata wachumba. uangonga kikombe leo baada ya siku saba uanaitwa kazini, au unapata mwenza
ha ha ha hah ! Tanzania bwana kama enzi za bulicheka
 
Kuibuka kwa Vikombe vipya kila uchao wa kulaumiwa ni SERIKALI. Kwa nini nasema hivyo??? Ni kwa sababu kama Serikali wangelikuwa makini toka siku ya awali Babu alipotangaza kuwa anaweza kutibu magonjwa sugu, serikali ilitakiwa kumpa masharti yafuatayo ili iweze kumruhusu atoe tiba. Masharti yenyewe ni kwanza kutojitangaza kuwa anatibu magonjwa sugu. Pili serikali ingechukua samples ya wagonjwa wote wanaojulikana mfano HIV wagonjwa 5, TB 5, BP 5, Kisukari 5 na kuwapeleka kwa babu kupatiwa kikombe, na kuwarudisha wodini au makwao na kuwafuatilia angalau kwa mwezi mmoja ili kuona maendeleo yao. Kama itaonekana hali zao zinachange to better, basi wangemruhusu babu na vinginevyo wangemfungia. Lakini hilo halikufanyika, matokeo kila uchao wanaibuka wengine. Mfano yule kijana wa Mbeya yeye anasema kabisa kuwa anasaidiwa na wasaidizi wake kichwani (a.ka mashetani) sasa kumwamini mtu kama huyu kwa kweli inatia wasiwasi saana na upeo wa viongozi wetu. Yule mama wa Tabora naye ukimwangalia anavyoombea watu kabla ya kuwapa dawa anachezesha mimacho kama mwenye kifafa, Nashangaa kwa mkuu wa mkoa kama Abeid Mwinyimsa kweli kupewa kikombe na yule mama na akanywa!!! Inatia hofu na sijui Taifa limefikia wapi???

Kwa hiyo babu pekee ndiye mwenye hati miliki ya ndoto. Washangilieni na hawa kama mlivyomshangilia babu. Yule wa Tabora wamhukumu kwa macho yake? Kweli mmekosa pa kujificha. Just come Clean people!
 
Mwonapo mambo hayo changamkeni maana ukombozi wenu u karibu.'
Kwa waaminio, ni wakati wa kujiandaa kuonana na Muumba wetu maaana usiku umeendelea saana na mchana umekaribia.
 
mimi naona hao wote wanaojitokeza kutoa kikombe wapigwe marufuku sasa, na aachiwe babu pekee,


Aachiwe babu kwa sababu yeye ana nini? wote wezi tu tatizo letu watanzania tuna ufinyu wa akili, hakuna shortcut za namna hiyo kama kikombe eti upone kisukari,ukimwi,cancer!! that is absurd....

tuachane na huu ujinga tujadili uchakachuaji unaotaka kufanyika kwenye katiba... hawa jamaa wanadivert attention ya umma kwa hivi vikombe, naskia morogoro napo wamepata kikombe chao... lolz we are doomed
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom