KING ASSENGA
JF-Expert Member
- Oct 8, 2016
- 929
- 1,494
Kwanza mshukuru Mungu kwa kuwa mzima bila kasoro yoyote kama ulivyo, sasa twende kwenye mada.
Kuna kijana mmoja tulikutana kwenye group moja la Dini, baada ya mimi kushusha nondo flani na makala zilizoshiba kuhusu imani na changamoto tulizonazo.
Kijana akaja inbox na ikawa mazoea kunitafuta na kuomba ushauri tu wa kiimani, ila baadae alinifungukia "Kaka maisha yangu siyaelewi nahisi nilizaliwa huku Duniani bahati mbaya. Kaka mimi sio mwanaume kama ninavyojiweka wala sio mwanamke". Nilishtuka sana kisha nikamuuliza kwanini unasema hivyo?
"Kaka mimi nina uume kama mwanaume na uke kama mwanamke na hii siri anayo baba na mama tu. Napata shida sana kujua mimi ni nani, na Dunia itanitambuaje. Natamani sana nife mapema nichoka upweke nilionao. Nimechoka sana kaka na
."
Nilimpa pole na kuanza kumuuliza maswali kadhaa kuhusu mwili wake, anapata hedhi kama mwanamke, uume haupo imara sana, anajihisi zaidi mwanamke ila tayari wazazi walimtambulishaga kama mwanaume.
Anatamani zaidi wanaume kimapenzi kuliko wanawake, hivyo anashindwa kujielewa ni upande upi sahihi?
Akaniuliza tena, "Je, nikienda kwa mwanaume sitaitwa shoga na kudharauliwa na kuwa mlaaniwa mbele za Mungu na hata wanadamu. Je sitatengwa? Na je, nikaamua kuwa na mwanamke kwanza ni mwanamke gani atanikubali? Je, sitaitwa msagaji na kuwa mlaaniwa mbele za Mungu na mbele za wanadamu?"
"Kaka nachukia sana maisha yangu, nachukia sana kuzaliwa kwangu Duniani, nimevumilia sana. Nina miaka 25 sasa siijui hatima, naona wivu sana wengine walivyo huru kuoa na kuoana angali mimi hiyo siyo haki yangu wala sifai kuwa miongoni, nishauri nifanyeje?"
Nisaidieni nimshauri nini, alinitumia picha ya jinsia zake pia, nilizifuta baada ya kushindwa kuamini na kuwa mbishi?!
Kuna kijana mmoja tulikutana kwenye group moja la Dini, baada ya mimi kushusha nondo flani na makala zilizoshiba kuhusu imani na changamoto tulizonazo.
Kijana akaja inbox na ikawa mazoea kunitafuta na kuomba ushauri tu wa kiimani, ila baadae alinifungukia "Kaka maisha yangu siyaelewi nahisi nilizaliwa huku Duniani bahati mbaya. Kaka mimi sio mwanaume kama ninavyojiweka wala sio mwanamke". Nilishtuka sana kisha nikamuuliza kwanini unasema hivyo?
"Kaka mimi nina uume kama mwanaume na uke kama mwanamke na hii siri anayo baba na mama tu. Napata shida sana kujua mimi ni nani, na Dunia itanitambuaje. Natamani sana nife mapema nichoka upweke nilionao. Nimechoka sana kaka na
."Nilimpa pole na kuanza kumuuliza maswali kadhaa kuhusu mwili wake, anapata hedhi kama mwanamke, uume haupo imara sana, anajihisi zaidi mwanamke ila tayari wazazi walimtambulishaga kama mwanaume.
Anatamani zaidi wanaume kimapenzi kuliko wanawake, hivyo anashindwa kujielewa ni upande upi sahihi?
Akaniuliza tena, "Je, nikienda kwa mwanaume sitaitwa shoga na kudharauliwa na kuwa mlaaniwa mbele za Mungu na hata wanadamu. Je sitatengwa? Na je, nikaamua kuwa na mwanamke kwanza ni mwanamke gani atanikubali? Je, sitaitwa msagaji na kuwa mlaaniwa mbele za Mungu na mbele za wanadamu?"
"Kaka nachukia sana maisha yangu, nachukia sana kuzaliwa kwangu Duniani, nimevumilia sana. Nina miaka 25 sasa siijui hatima, naona wivu sana wengine walivyo huru kuoa na kuoana angali mimi hiyo siyo haki yangu wala sifai kuwa miongoni, nishauri nifanyeje?"
Nisaidieni nimshauri nini, alinitumia picha ya jinsia zake pia, nilizifuta baada ya kushindwa kuamini na kuwa mbishi?!