mimiamadiwenani
JF-Expert Member
- Mar 9, 2022
- 5,411
- 7,016
"Mwanangu ahsante sana na nimefarijika kwa kunikumbuka na kunitafuta, mimi ndiyo baba yako na ujue tu kuwa una baba mmoja tu, huna baba wawili.
Mama yako ndiye alitaka haya yote, alinizuia mimi kuwa karibu na wewe toka ukiwa na miaka 6, alikuweka mbali nami na kwenda na wewe nisikokujua.
Nashukuru kwamba umekuwa mkubwa sasa na unasoma chuo kikuu, mimi nakukaribisha kwa mikono miwili mwanangu, ombi lako la pesa za ada nimelisikia.
Sasa chukua hii M2 kalipe ada hiyo 1.2M then 800K baki nayo. Pia umeniambia huna simu, okay chukua hii iPhone 14 yangu ina mwezi mmoja tu, ngoja niirekebishe nikukabidhi.
Mwezi ujao jiandae nikupeleke shopping moja kwa rafiki yangu ukanunue jeans na nguo nyingine, bibi yako anakuulizia mno mwanangu na ana hamu mno ya kukuona.
Baba yako mdogo naye ana hamu mno ya kukuona, wewe si yatima mwanangu, una ndugu zako wawili wa kike, na mmoja mdogo wa kiume, nao wanakuulizia sana na wana hamu ya kukuona.
Ngoja nikupe namba ya bibi yako na ya baba yako mdogo wa Dubai... ooh nilisahau chukua pia na namba ya babu yako anakuulizia mno, amekuwekea ng'ombe wako kijijini.
Ngoja nitamuambia umenitafuta mwanangu, kisha utampigia.
Oooh nilisahau, kuna laptop pia ina miezi miwili tu, ni ya Apple nimeona huna pc mwanangu, ngoja nifute acc's zangu nikupe.
Namlaumu sana mama yako, yaani amekujaza sumu kuwa mimi nilikutelekeza ukiwa na miaka 6? Ila ndiyo wanawake walivyo."
Je, huyu kijana ataacha kumchukia mama yake na kumuona mbaya?
Mama yako ndiye alitaka haya yote, alinizuia mimi kuwa karibu na wewe toka ukiwa na miaka 6, alikuweka mbali nami na kwenda na wewe nisikokujua.
Nashukuru kwamba umekuwa mkubwa sasa na unasoma chuo kikuu, mimi nakukaribisha kwa mikono miwili mwanangu, ombi lako la pesa za ada nimelisikia.
Sasa chukua hii M2 kalipe ada hiyo 1.2M then 800K baki nayo. Pia umeniambia huna simu, okay chukua hii iPhone 14 yangu ina mwezi mmoja tu, ngoja niirekebishe nikukabidhi.
Mwezi ujao jiandae nikupeleke shopping moja kwa rafiki yangu ukanunue jeans na nguo nyingine, bibi yako anakuulizia mno mwanangu na ana hamu mno ya kukuona.
Baba yako mdogo naye ana hamu mno ya kukuona, wewe si yatima mwanangu, una ndugu zako wawili wa kike, na mmoja mdogo wa kiume, nao wanakuulizia sana na wana hamu ya kukuona.
Ngoja nikupe namba ya bibi yako na ya baba yako mdogo wa Dubai... ooh nilisahau chukua pia na namba ya babu yako anakuulizia mno, amekuwekea ng'ombe wako kijijini.
Ngoja nitamuambia umenitafuta mwanangu, kisha utampigia.
Oooh nilisahau, kuna laptop pia ina miezi miwili tu, ni ya Apple nimeona huna pc mwanangu, ngoja nifute acc's zangu nikupe.
Namlaumu sana mama yako, yaani amekujaza sumu kuwa mimi nilikutelekeza ukiwa na miaka 6? Ila ndiyo wanawake walivyo."
Je, huyu kijana ataacha kumchukia mama yake na kumuona mbaya?