Kigoma Yazizima kumlaki Dr Slaa

Kigoma Yazizima kumlaki Dr Slaa

Molemo

JF-Expert Member
Joined
Sep 24, 2010
Posts
14,620
Reaction score
13,361
Watu wameshawasili uwanjani hapa Community Centre mjini Kigoma kwa ajili ya ujio wa Gwiji wa Siasa Tanzania na Katibu Mkuu wa CHADEMA Dr Wilbroad Slaa.

Wengine tayari wameshaanza kuchukua nafasi zao. Ngoma inachezwa hapa kama maandalizi ya kumpokea Katibu Mkuu Dkt. Slaa.

Manji wa ngoma hii anaitwa Mapigo Saba, ambaye anajinasibu kuwa ana miaka 61, anazidi kuwahanikiza watu waendelee kujongea hapa.

Anasema vijana makini, wazee makini na akina mama makini wako CHADEMA. Watu wanamsubiri kwa hamu mgeni wao!

Updates 1.....

Kila kitu kiko sawasawa hapa, mathalani kuna jenereta la dharura kama umeme utakatika.

Red brigade wako imara karibu kila kona ya uwanja huu kuhakikisha ulinzi uko sawasawa. Kuna stori inatafutwa na kuandaliwa nje ya uwanja hapa.

Wanahabari tumeshanyaka mpango mzima unaoandaliwa maana inavyoonekana huku ndani mipango yao hawataweza kufanikisha kwa sababu ya uimara wa ulinzi wa Red Brigade na usalama wa Chadema.

Kuna waandishi wa magazeti ya...wameshaandaliwa na tayari wamepelekwa hapo nje ambapo kuna kitu kinaandaliwa.

Update 2....

Watu wametulia kbs hapa Uwanjani, wakiendelea kumsubiri kwa hamu mgeni wao. Watu wanazidi kumiminika uwanjani.

MC anaendelea kuwasisitiza wananchi wengi walioko pembeni mwa uwanja waungane na wenzao wengi pia walioko mbele ya jukwaa.

MC anaomba wimbo wa ''SLAA ANAWEZA''. Anasema huo wimbo unakubalika sana Kigoma anasema kuna siku kwenye harusi moja, Bwana Harusi aliwashangaza waalikwa alipoomba wimbo huo kwa ajili ya kutokea ukumbini.

Anasema maudhui yake ni murua na leo mtu mwenyewe yuko hapa. Waliyempigia kura za kutosha mwaka 2010 kwa sababu wanamuamini na wanaamini katika chama chao, CHADEMA.

Updates 3....

Dkt. Slaa ameingia uwanjani tayari wananchi waliokuwa pembeni na nje ya uwanja, wanakimbilia karibu na jukwaa kumuona na kumsikiliza Katibu Mkuu huku uwanja ukilipuka kwa shangwe kuu.

Kikundi cha Mapigo Saba kinaitwa kwa ajili ya kuimba wimbo maalum kwa ajili ya mgeni rasmi.

Mkiti Mwalimu Adam anachukua mic kufungua mkutano. Katibu Mkuu ameshaketi jukwaani tayari. Anazungumza mawili matatu na Mkiti wa Kanda ya Magharibi, Mohamed Mambo. Tayari mkutano umefunguliwa watu wanashangilia hapa.

Mapigo saba anasema wana nyimbo 2 kwa ajili ya Dkt. Slaa. Anasema Chadema Kigoma kuna amani.

Mratibu wa ziara, Mwita Waitara Mwikabe anachukua nafasi yake kuendesha itifaki ya mkutano. Sasa wanatambulishwa madiwani wa CHADEMA hapa.

Diwani wa Uvinza anawafurahisha watu kwa kusema CHADEMA ni mpango Mungu, tunasonga mbele, hakuna kurudi nyuma. Watu wanashangilia hapa.

Sasa anapanda Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kigoma Ujiji anatoa taarifa namna CHADEMA kupitia Halmashauri yake inasimamia shughuli ya maendeleo.

Viongozi wa chama wanaendelea kujitambulisha. Leo kuna kikao cha Baraza la Mashauriano la mkoa, hivyo kuna viongozi wengi, baada ya Katibu wa Mkoa, Msafiri Wamalwa sasa kapanda Katibu wa Kanda ya Magharibi, Christopher Nyawanji.

Anatambulisha wasaidizi wake kwenye ofc ya kanda. Sasa Waitara anatoa taarifa fupi ya ziara tangu ianze Dec 4.

Updates 4.....

Sasa baada ya Mkiti wa Kanda, amepanda Katibu Mkuu Dr Slaa ambaye anashangiliwa mpaka inakuwa shida kusikilizana. Ameanza kwa kutoa dakika moja ya kukaa kimya, kwa sababu ya misiba iliyotokea kwa viongozi wawili wa CHADEMA Mkoa.

Updates 5....

Katibu Mkuu, Dkt. Slaa, ambaye amemaliza mkutano punde, amewaacha wananchi na hamu ya kuendelea kumsikiliza wakati akishusha nondo za mahesabu ya ruzuku na mapato mengine ya chama.

Sasa anaelekea kwenye kikao cha ndani, Baraza la Mashauriano la Mkoa.

Umati umetanda kila kona pembeni ya barabara wakimshangilia Dr Slaa na kusema CHADEMA ndiyo mkombozi wa Kigoma na Tanzania.Dr Slaa naye anashusha vioo vya gari na kupunga mikono kwa furaha kama heshima kwa wana Kigoma kwa mapokezi makubwa sana waliyompatia!!

Umati uliofurika kumsikiliza Dr Slaa mjini Kigoma leo:

attachment.php



Source:Afisa Habari Mkuu CHADEMA Tumaini Makene
 
Watu wameshawasili uwanjani hapa Community Centre mjini Kigoma kwa ajili ya ujio wa Gwiji wa Siasa Tanzania na Katibu Mkuu wa CHADEMA Dr Wilbroad Slaa.

Wengine tayari wameshaanza kuchukua nafasi zao. Ngoma inachezwa hapa kama maandalizi ya kumpokea Katibu Mkuu Dkt. Slaa.

Manji wa ngoma hii anaitwa Mapigo Saba, ambaye anajinasibu kuwa ana miaka 61, anazidi kuwahanikiza watu waendelee kujongea hapa.

Anasema vijana makini, wazee makini na akina mama makini wako CHADEMA. Watu wanamsubiri kwa hamu mgeni wao!

Source:Afisa Habari Mkuu CHADEMA Tumaini Makene

Kuna mjina kafika hapa mapema na kuanza kubwabwaja .Makene niko hapa uwanjani tafadhali sema uko upande gani hata tusalimiane .Au nilete nama yako kwa pm nikupigie nijongee
 
Watu wameshawasili uwanjani hapa Community Centre mjini Kigoma kwa ajili ya ujio wa Gwiji wa Siasa Tanzania na Katibu Mkuu wa CHADEMA Dr Wilbroad Slaa.

Wengine tayari wameshaanza kuchukua nafasi zao. Ngoma inachezwa hapa kama maandalizi ya kumpokea Katibu Mkuu Dkt. Slaa.

Manji wa ngoma hii anaitwa Mapigo Saba, ambaye anajinasibu kuwa ana miaka 61, anazidi kuwahanikiza watu waendelee kujongea hapa.

Anasema vijana makini, wazee makini na akina mama makini wako CHADEMA. Watu wanamsubiri kwa hamu mgeni wao!

Source:Afisa Habari Mkuu CHADEMA Tumaini Makene

Mimi tayari nimechukua nafasi yangu muda sana# Dr
 
Last edited by a moderator:
Tunasubiri habari zaidi mkuu...naamini makamanda km kawa watawasha moto Harpo kigoma
 
Nipo mkutanoni Mwanga Centre Kigoma nitatoa Updates, endapo Taswira akipotosha nitaweka mambo sawa
 
kadanganye wajinga, wasiofuatilia mambo, mkutano hauna watu, ndio mana hata ule wa asubuhi haukufanyika, hata huu ni watoto tu ndio wengi wamefata muziki
 
Watu wameshawasili uwanjani hapa Community Centre mjini Kigoma kwa ajili ya ujio wa Gwiji wa Siasa Tanzania na Katibu Mkuu wa CHADEMA Dr Wilbroad Slaa.

Wengine tayari wameshaanza kuchukua nafasi zao. Ngoma inachezwa hapa kama maandalizi ya kumpokea Katibu Mkuu Dkt. Slaa.

Manji wa ngoma hii anaitwa Mapigo Saba, ambaye anajinasibu kuwa ana miaka 61, anazidi kuwahanikiza watu waendelee kujongea hapa.

Anasema vijana makini, wazee makini na akina mama makini wako CHADEMA. Watu wanamsubiri kwa hamu mgeni wao!

Updates 1.....

Kila kitu kiko sawasawa hapa, mathalani kuna jenereta la dharura kama umeme utakatika.

Red brigade wako imara karibu kila kona ya uwanja huu kuhakikisha ulinzi uko sawasawa. Kuna stori inatafutwa na kuandaliwa nje ya uwanja hapa.

Wanahabari tumeshanyaka mpango mzima unaoandaliwa maana inavyoonekana huku ndani mipango yao hawataweza kufanikisha kwa sababu ya uimara wa ulinzi wa Red Brigade na usalama wa Chadema.

Kuna waandishi wa magazeti ya...wameshaandaliwa na tayari wamepelekwa hapo nje ambapo kuna kitu kinaandaliwa.

Source:Afisa Habari Mkuu CHADEMA Tumaini Makene

Slaa anazidi kuaibika, huo ndio ukweli. Mleta mada anapotosha umma
 
lete maneno ndugu

ukombozi utayari muda si mrefu tutashuhudia makundi kwa makundi wakijumuika kwenye tumaini jipya la maisha safi yaliyotawaliwa na aman,upendo,ushirikiano wa rasilimali zetu na chuki dhidi ya rushwa. Go go go dr.
 
Tunashukuru kwa update Molemo, pamoja sana mkuu
 
Last edited by a moderator:
Kuna mjina kafika hapa mapema na kuanza kubwabwaja .Makene niko hapa uwanjani tafadhali sema uko upande gani hata tusalimiane .Au nilete nama yako kwa pm nikupigie nijongee

Mtumie PM Molemo akupe, tafadhari usimmwagie tindikali (joking)
 
heri kifo cha cuf na nccr kuliko cha hili genge la waporaji
 
Kila k2 kiko sawasawa hapa, mathalani kuna jenereta la dharura kama umeme utakatika. Red brigade wako imara karibu kila kona ya uwanja huu kuhakikisha ulinzi uko sawasawa. Kuna stori inatafutwa na kuandaliwa nje ya uwanja hapa. Wanahabari tumeshanyaka mpango mzima unaoandaliwa maana inavyoonekana huku ndani mipango yao hawataweza kufanikisha kwa sacbu ya uimara wa ulinzi wa Red Brigade na usalama wa Chadema. Kuna waandishi wa magazeti ya...wameshaandaliwa na tayari wamepelekwa hapo nje ambapo kuna kitu kinaandaliwa.
 
kadanganye wajinga, wasiofuatilia mambo, mkutano hauna watu, ndio mana hata ule wa asubuhi haukufanyika, hata huu ni watoto tu ndio wengi wamefata muziki


Weka picha, tuone hao watoto sio unabwabwaja tu hapa na kuturushia mipovu yako
 
Back
Top Bottom