Kifo cha mwandishi wa Channel Ten: Kauli za Polisi na mwitikio wa Wanahabari

Kama ndiyo ma RPC Wenyewe ni hivi,tunasafari ndefu ya kwenda,hivi kama mtu amekiuka sheria ndiyo adhabu yake kuuawa na bomu?.Hivi kama RPC anakaribia kustaafu ndiyo aamuru kuua watu? Kazi ya wanahabari ni kuandika habari,sasa yule mwandishi aliuawa kwa lipi? je ,RPC alikijua alichotaka kuandika yule mwandishi?,ni sheria gani ambayo mwandishi alikiuka? kwani polisi hawa wezi kuzuia vurugu mpaka wa ue?picha zinaonesha polisi akimfyatulia bomu yule mwandishi,je adhabu yule mwandishi ndiye aliye vunja sheria au kile kikundi chote kilichokuwa pale? kama ni yeye peke yake,je umati ule wote wa polisi ulishindwa kumkamata mtu mmoja nakumpeleka kituoni? kama ni wengi waliokuwa pale,kwanini adhabu hii ya kifo impate maskini huyu mwandishi na wengine kuachwa kama adhabu hiyo ni stahiki kwa wavunja amri? RPC na jeshi la polisi lijitathmini upya,watu wakichoka wataanza kushughulika na mtu binafsi badala ya polisi kama taasisi,maana polisi wenyewe tunao huku huku mtaani katika nyumba za kupanga,sjui itakuwaje,nawapongeza wale police waadilifu na wale wenye kutii amri ya kuua kama vile kazi ya polisi ni maisha ya peponi ole wao. Labda ni upeo wangu wa kuelewa mambo ni mdogo,lakini naona hapa kunatatizo
Police wengi wanavuta bangi, unategemea nini kuhusu usalama wa raia? Jeshi la police limejaa wavuta bangi! Ni polisi wachache sana wanaofanya kazi kwa kufuata maadili ya kazi yao, wengi utawaona walivyo na hasira na raia hata kama mtu hana kosa/hatia yeyote. Pamoja na hayo, kulikuwa na fujo gani hadi kuamua kutumia nguvu kiasi hicho? Tufike mahali tuanze kuhoji matumizi ya siraha kama mabomu ni nani anagharamia? Tufahamu nani ni nani, amefikaje hapo alipo?
 
Usiropoke ovyo. Kwa wakati huu Watanzania wanatakiwa kuwa watulivu na Kumshirikisha M/Mungu kwa haya toe yanayotokea. Tuwe wapole na tukubali Dola inavyoelekeza. Kama ungekuwa wewe nadhani ungepitiliza zaidi ya hapo

Are you serious? M/Mungu ashirikishwe kwenye cold blooded murder? Are you mocking the dead?
 
Source Mwananchi "“Mwandishi alikuwa akikimbia kutoka upande wa wananchi kuelekea walipokuwa polisi. Kuna kitu kilirushwa kikitokea upande wa wananchi na kumfikia ambacho kilimjeruhi pia askari akiwamo Mkuu wa Kituo cha Polisi (OCS).”
1) Bomu likirushwa bullet proof vest haisaidii kujikinga, hivyo waliomshika wote wangejeruhiwa vibaya
2) Bomu likirushwa, madhara yake huwa kuanzia sm 60 above the ground, Mwandishi alikuwa chini wakimpiga
3) Ukiangalia picha(Mwananchi) utaona police ameelekeza bunduki ktk tumbo la mwandishi. Baada ya kufyatua bomu la machozi close proximity na mwandishi, the impact of the gun ndio uliochana tumbo la mwandishi. The residue ndizo zilizo mjeruhi OCS. Huo ni ukweli wa kitaalaam. Uliza wataalaam wa mabomu JWTZ watasema
 
Alikuwa wa kwanza kutoa tamko la uongo ,kwamba marehemu aliwakimbilia polisi ili
Kujiokoa na kabla hajasema kitu akalipuliwa na kitu kizito kilchorushwa.

Huu ni usanii wa ajabu sana,wamkamate wamhoji aeleze alikopata habari hizo.
Naiwe fundisho kwa wenzake kwamba hakuna aliyejuu ya sheria.
 
Ndiyo taarifa iliyoandaliwa ili itolewe baada ya kumaliza kazi iliyopangiliwa mapema,pale wanacheza one touch mkuu,huyo keshaimba verse yake anakaa pembeni kumpisha mwingine,mpaka postmortem itoke,viongozi wote wa genge la polisi watakuwa wameshatoa ripoti zao tofauti tofauti,hili ni Tz police FORCE.
 
kama kuna kitu kilirushwa na wananchi wakati akikimbilia upande wa polisi basi janzo cha jaraha kitakuwa tumboni sio mgongoni. Haimake sence kwamba awe anakimbilia upande wa polisi wakate yeye anajulikana mkoani na kazi yake na wananchi hawakuwa na hasira nae, atakimbilia vipi upande wa polisi wakati wao ndio wanaorusha mabomu kuwatawanya? Kwa hili na mengine mengi polisi hawana hoja, wameanza na ULipomboka na cinema yao ile kamanda wa dar aliekuja nayo, na mauaji yanaendelea. Kikosi cha FFU kimewachwa kipate kichwa kikijiona hakina haki ya kushitakiwa wala hakina majibu. Hivi ni training gani wanayopewa inayowapa kasumba waliokuwa nayo kwa wananchi? Wamekuwa kama wanyama pori kwa mashambulizi mbele ya wananchi, wazanzibari walisema mengi juu ya polisi lakini sasa naona effect yao nchi nzima. Mwenye kufurahia mauaji yeyote ya mwananchi ujuwe amefilisika ile sifa ya utu aliepewa nayo, halina uchama hili, ni unyanyasaji wa demokrasia ya nchi na uvunjaji wa haki za binaadamu.
 
Kwa faida ya watu ambao hawapo majumbani ebu tiririka tupe muktasari kwa jinsi inavyoona.

Polisi wa Tanzania 85% ya wale waliomaliza F4 waliondoka na division 0 au Division 4 ya points 30 na kuendelea na wengi walitumia vyeti vyetu watanzania tulio wengi ili kuupata huo upolisi ,ndiyo maana wengi hata hawatumii common sense ,wanatumia nguvu nyingi kuliko maarifa ,hata pale panapohitaji advocacy wao minguvu mingi,Haya mauaji yalipangwa maksudi ili kuwatisha CHADEMA. Hii ni aibu kwa serikali dhalimu ya CCM,si uliona yule poalisi msomi mwenye nyota 3 alijitahidi kumwokoa Hayati Mwangosi lakini yaliyopangwa na Serikali ya CCM ilikuwa sharti yatimie, Hata mungu hatakuwa pamoja na CCM ambao wako pembeni wakifurahia na kushangilia misheni yao ya kutoa roho za watu ikikamilika, mambo yote 2015 patakuwa hapatoshi,polisi wa CCM aandaeni na agizeni makontena ya risasi,bora mtumalize kabisa walipa kodi maskini walalahoi wa TZ,then mtawale mawe na visiki.Laana lazima itakuwa upande wenu na serikali dhalimu iliyofilisika ya Sisiemu.
A%20S-devil1.gif
 
Kulikuwa na kipindi asubuhi hii kinaongelea kama Kifo cha mwandishi huyu ni cha bahati mbaya au kimepangwa.

Hicho kipindi kiliwekwa katika vipengele, pia nipo kukitazama na nilikuta Mkuu wa Polisi akizungumzia kifo na vurugu hizo huku akisisitiza kuwa vyama vya Siasa vifuate taratibu zilizowekwa ili kuepusha vurugu, kwa mtazamo wangu ni dhahiri kuwa hizo lawama kuhusu kifo cha marehemu wanawatupia CDM.

Muasisi wa kipindi hicho cha Channel Ten cha Baragumu ambaye kwa sasa ni mfanyakazi wa Vodacom, kamzunguzia wasifu wa marehemu David Mwambosi kwa upana akisisitiza alivo mchapa kazi na jinsi alivokuwa akipenda kwazi na kufanya hio kazi kwa staili yake ya pekee.

Wakati wowote ataongea kiongozi wa CDM (Afisa habari) ambae hadi wakati huu inaonesha kwa bahati mbaya sana kapigiwa simu na hayupo hewani. Nia ya mtangazaji ni swali kwa wana CDM kama ilikuwa maandamano ama kufunguliwa kwa tawi na nini neno lao kuhusu tukio.

Wananchi mbali mbali wamepiga simu kutoa maoni... Ni wazi kuwa wote wanalaumu Jeshi la polisi.
Polisi wa Tanzania 85% ya wale waliomaliza F4 waliondoka na division 0 au Division 4 ya points 30 na kuendelea na wengi walitumia vyeti vyetu watanzania tulio wengi ili kuupata huo upolisi ,ndiyo maana wengi hata hawatumii common sense ,wanatumia nguvu nyingi kuliko maarifa ,hata pale panapohitaji advocacy wao minguvu mingi,Haya mauaji yalipangwa maksudi ili kuwatisha CHADEMA. Hii ni aibu kwa serikali dhalimu ya CCM,si uliona yule poalisi msomi mwenye nyota 3 alijitahidi kumwokoa Hayati Mwangosi lakini yaliyopangwa na Serikali ya CCM ilikuwa sharti yatimie, Hata mungu hatakuwa pamoja na CCM ambao wako pembeni wakifurahia na kushangilia misheni yao ya kutoa roho za watu ikikamilika, mambo yote 2015 patakuwa hapatoshi,polisi wa CCM aandaeni na agizeni makontena ya risasi,bora mtumalize kabisa walipa kodi maskini walalahoi wa TZ,then mtawale mawe na visiki.Laana lazima itakuwa upande wenu na serikali dhalimu iliyofilisika ya Sisiemu.
A%20S-devil1.gif
 
Maundumula tume ipi ambayo imeshawahi kuundwa hata tanzania na ikaja na jibu la uhakika
Unategemea nini mwenye tume akiwa ashatoka na majibu yake ambayo anayasema hadharani
Chagonja alisema waliofanya fujo songea ni wahuni na tume iliundwa ambayo mpaka leo hata majibu hakuna.
Huwa naona ni ulaji mwingine tuu unafanyika kwa hao wanaoteuliwa kwenye hizo tume
m

Tuseme tume huru.
 
Back
Top Bottom