Kifo cha CCM

mbavu nene

Senior Member
Joined
Nov 17, 2012
Posts
102
Reaction score
85
Ccm kimekuwa chama kikongwe sana barani Africa ambacho mpaka Leo kipo madarakani lakini ni chama ambacho kwamiaka yote hiyo kimeshindwa kutufikisha watanzania mahali ambapo tulipaswa kufika kimaendeleo kulingana na rasilimali zilizopo nchini. Ni ukweli usiofichika Kwamba kuna wachache ndani ya Ccm Kwa muda mrefu wamekuwa wanufaika wakuu wa rasilimali za nchi wengine tukiumia.

Naufurahia mgogoro ulioanza ndani ya Ccm maana wanufaika na watu waliotutesa Kwa miaka mingi Kwa kula mkate Wa taifa peke yao wameguswa/wametikiswa na kiukweli hawatakubali ndio utakuwa mwisho wao pamoja na chama chao cha kifisadi. Watanzania sio wajinga tena waking'ang'ania chama wataachiwa ila watanzania tutaamua maana tuliwaona tukawasikiliza tukawapa nafasi lakini walituumiza sana sasa sisi tunamjua tunayemtaka vyovyote itakavyokuwa ila tutamchagua huyo.
Kwaheri Ccm yamafisadi mmetuumiza Kwa muda mrefu.

Hii nchi ni yetu sote.
 
Mwisho wa CCM ni mwaka 2020 ambapo chama hiki kitafutika kabisa ndani ya bara la Afrika na kusahaulika. Hakuna mtanzania mwenye akili timamu atakayekubali kuwarudisha hawa mafisadi na wachumiatumbo wakubwa madarakani.
 
Mwisho wa CCM ni mwaka 2020 ambapo chama hiki kitafutika kabisa ndani ya bara la Afrika na kusahaulika. Hakuna mtanzania mwenye akili timamu atakayekubali kuwarudisha hawa mafisadi na wachumiatumbo wakubwa madarakani.

Usiku hukulala nini? Mbona unaota mchana?
 
Utakufa wewe na kuicha CCM inapete. CHADEMA ndiyo wanaweza kufa sio gar kubwa
 
Umeandika kwa akili mno. Walikula sana wakavimbewa wakamteua ngosha wakidhani yatakuwa mazoea yaleyale kula na familia zao. Sasa kawagusa wanapiga kelele. Kama wanadhani CCM inapendwa wamguse. watabaki na CCM yao ila sisi bingwa tunamjua. Magu wanyooshe.
 
Tunamshukuru Mungu kutupa jiwe ili chakavu kife kupitia kwake tutashuhudia matanga.Walituaminisha wakoloni wabaya kumbe heri ya mkoloni tungekuwa mbali sana kuzidi south Africa Kwa raslimali zetu ,ajira teletele,miundombinu,elimu,afya,viwanda, Mashamba makubwa makubwa,biashara nk.Miaka 60 hata nyumba za nyasi ccm imeshindwa zifuta.
 
Niambie chama kipi kinachobebwa na dola kimedumu duniani. Chama cha China kimedumu hata sasa sababu kinabebwa na wananchi wa China na si dola.
 
Chama chochote kikibebwa na dola badala ya wananchi ni lzm kitakufa.Wapi KANU, cha ukombozi Malawi,nk someni history za kufa Kwa vyama vya ukombozi vilikufaje
 
Mwisho wa CCM ni mwaka 2020 ambapo chama hiki kitafutika kabisa ndani ya bara la Afrika na kusahaulika. Hakuna mtanzania mwenye akili timamu atakayekubali kuwarudisha hawa mafisadi na wachumiatumbo wakubwa madarakani.
Kwa 2me iliyopo?
 
Kama hakikufa wakati wa Lowasa anahamia Chadema usitegemea kitakufa kwa sasa.
 
Reactions: Oii
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…