mbavu nene
Senior Member
- Nov 17, 2012
- 102
- 85
Ccm kimekuwa chama kikongwe sana barani Africa ambacho mpaka Leo kipo madarakani lakini ni chama ambacho kwamiaka yote hiyo kimeshindwa kutufikisha watanzania mahali ambapo tulipaswa kufika kimaendeleo kulingana na rasilimali zilizopo nchini. Ni ukweli usiofichika Kwamba kuna wachache ndani ya Ccm Kwa muda mrefu wamekuwa wanufaika wakuu wa rasilimali za nchi wengine tukiumia.
Naufurahia mgogoro ulioanza ndani ya Ccm maana wanufaika na watu waliotutesa Kwa miaka mingi Kwa kula mkate Wa taifa peke yao wameguswa/wametikiswa na kiukweli hawatakubali ndio utakuwa mwisho wao pamoja na chama chao cha kifisadi. Watanzania sio wajinga tena waking'ang'ania chama wataachiwa ila watanzania tutaamua maana tuliwaona tukawasikiliza tukawapa nafasi lakini walituumiza sana sasa sisi tunamjua tunayemtaka vyovyote itakavyokuwa ila tutamchagua huyo.
Kwaheri Ccm yamafisadi mmetuumiza Kwa muda mrefu.
Hii nchi ni yetu sote.
Naufurahia mgogoro ulioanza ndani ya Ccm maana wanufaika na watu waliotutesa Kwa miaka mingi Kwa kula mkate Wa taifa peke yao wameguswa/wametikiswa na kiukweli hawatakubali ndio utakuwa mwisho wao pamoja na chama chao cha kifisadi. Watanzania sio wajinga tena waking'ang'ania chama wataachiwa ila watanzania tutaamua maana tuliwaona tukawasikiliza tukawapa nafasi lakini walituumiza sana sasa sisi tunamjua tunayemtaka vyovyote itakavyokuwa ila tutamchagua huyo.
Kwaheri Ccm yamafisadi mmetuumiza Kwa muda mrefu.
Hii nchi ni yetu sote.