Kidudu mtu awa gunzo kwa walaji mboga za majani

Kidudu mtu awa gunzo kwa walaji mboga za majani

Dada wa kazi na majirani wamekazana kidudu mtu,hataki ninunue mboga za majani eti tutakufa,Jana nikanunua majani ya maboga,nikamwambia nipikie,yaunge na nazi,nikagonga na ugali na kasamaki kakukaanga,hadi sasa na type hapa JF na hata kizunguzungu sina,kesho usiku kisamvu na ubwabwa.

Kidudu mtu kama yupo mabwana afya wangepiga marufuku uuzaji wa mboga mboga za majani.

Nikiwauliza yukoje,ooh jirani alimuona,ooh kama popo,ooh kwenye cabbage, ooh kwenye kisamvu!!!
Mkuu umenichekesha sana [emoji1] [emoji1] [emoji1]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ujue kidudu mtu kwa mi nnavyojua ni mnafiki, sasa kuona uzi una jina hili huku upo MMU nikajua kuna mtu kaja kutupa somo la maisha sasa tena mambo ya visamvu vipi tena hapa?

Umezingua mdau
 
4650b47b6a9ecf16dc69f1800d87e7df.jpg
Huyo hapo kidudu mtu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kisamvu kikolee Nazi.

Halafu kibaki Asubuhi kwa Uporo.

Kiporo cha Wali kwa Kisamvu sio mchezo
 
huko kijiji kimoja mkoan morogoro watu wamekufa.tatizo waandishi habar wako bize na lissu
 
Dada wa kazi na majirani wamekazana kidudu mtu,hataki ninunue mboga za majani eti tutakufa,Jana nikanunua majani ya maboga,nikamwambia nipikie,yaunge na nazi,nikagonga na ugali na kasamaki kakukaanga,hadi sasa na type hapa JF na hata kizunguzungu sina,kesho usiku kisamvu na ubwabwa.

Kidudu mtu kama yupo mabwana afya wangepiga marufuku uuzaji wa mboga mboga za majani.

Nikiwauliza yukoje,ooh jirani alimuona,ooh kama popo,ooh kwenye cabbage, ooh kwenye kisamvu!!!
Mkuu kinachoitwa kidudu mtu ni 4th stage larva(kiwavi) au pupa(buu)stage wa kipepeo kitaalam anayeitwa "Spalgis epius." Kidudu mtu hana madhara yeyote.Huyo kipepeo anaitwa kwa lugha ya kingereza cha kawaida Apefly, jina ambalo linatokana na pupa au buu lake kufanana na sokwe.Hana madhara yeyote kama nilivyo tangulia kusema hapo awali,ila kama kawaida osha mboga zako halafu pika.

Wadudu hawa wanapatikana sana nchi za Asia.
 
Mkuu kinachoitwa kidudu mtu ni 4th stage larva(kiwavi) au pupa(buu)stage wa kipepeo kitaalam anayeitwa Spalgis epius.Hana madhara yeyote.Anaitwa kwa lugha ya kingereza cha kawaida Apefly, jina ambalo linatokana na pupa au buu lake kufanana na sokwe.Hana madhara yeyote,ila kama kawaida osha mboga zako halafu pika.Wadudu hawa wanapatikana sana Asia.

Hapa nyumbani kwangu wamejazana tele hawa vidudu mtu. Nawaona tu ukutani
 
Hapa nyumbani kwangu wamejazana tele hawa vidudu mtu. Nawaona tu ukutani
Uwe na amani mkuu,hawana madhara yeyote.Safisha ukuta wako vizuri tu usiwe na vumbi, kwa kuwa wanapenda sehemu zenye vumbi.
 
Mfalme wangu hata mimi leo nilisikia pahala wakizungumzia hiko kidudu eti ukikipika bahati mbaya mtu akakila kichwa kinavimba kinakua kikubwaaaa badae kinapasuka eti...


Mahondaw wa Smart911
Siyo kweli super dear...
 
Anaitwa apefly ni jamii ya kipepeo..ni mdudu rafiki kwa mimea sababu anakula wadudu waharibu kwenye mapapai...uzushi mwigine wowote sio kweli

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom