Kidudu mtu awa gunzo kwa walaji mboga za majani

Kidudu mtu awa gunzo kwa walaji mboga za majani

Sefu jafary

JF-Expert Member
Joined
Jun 5, 2016
Posts
382
Reaction score
258
Kama kichwa kinavyo someka, moja ya habari zilizo enea na ambazo huwapa watu wengi hofu ni kuwepo kwa huyu mdudu.

Hofu huzidi kutanda baada ya kuwepo habari kuwa mdudu huyu ana mdhara na kuna maeneo amesababisha vifo.

Mbali na habari ya vifo pia shape ya huyu mdudu huwaogopesha watu wengi na kuwafanya waamini juu ya kinacho zungumziwa.

Kingine ni maneno yanayo enezwa na baadhi ya watu, ambayo hayajulikani kama ni ya ukweli au ni uzushi

Mfano: Vifo vinavyo semekana vimetokana na huyu mdudu huenea kwa kasi sana bila ya kuwa na ushahidi (Evidence)

Mpaka sasa mdudu huyu amesababisha soko la mboga za majani kuyumba katika baadhi ya maeneo na kuyafanya maisha yazidi kuwa magum.

Hivyo basi kama kuna mwenye ukweli wowote juu ya Kidudu mtu aweke hadharani kama njia ya kutusadia sisi ambao hatujui.

Mambo ambayo yana hitaji ufafanuzi ni pamoja na:

1: Ukweli juu ya Kidudu mtu; ana madhara au hana?

2: Kama yapo kivipi: akiliwa pamoja na mboga au hata akitambaa ni tatizo?

NB: Kuna watu wengi wamejazwa hofu kwa habari za kusikia na ambazo hazina ushahidi.

Hivyo kama habari zako ni za kusikia na huna ushahidi, sio vibaya ukaangalia comments za wengine bila kuchangia chochote.

Nawasilisha mada mezani na:

Hapa chini ni picture ya huyo mdudu.
f5cbd0582aa50ab62007d464abc0168b.jpg
 
Dada wa kazi na majirani wamekazana kidudu mtu,hataki ninunue mboga za majani eti tutakufa,Jana nikanunua majani ya maboga,nikamwambia nipikie,yaunge na nazi,nikagonga na ugali na kasamaki kakukaanga,hadi sasa na type hapa JF na hata kizunguzungu sina,kesho usiku kisamvu na ubwabwa.

Kidudu mtu kama yupo mabwana afya wangepiga marufuku uuzaji wa mboga mboga za majani.

Nikiwauliza yukoje,ooh jirani alimuona,ooh kama popo,ooh kwenye cabbage, ooh kwenye kisamvu!!!
 
Ndugu kula kisamvu. Hakuna kitu kamà hicho huo ni uvumi tu. Niambie ni wangapi wamekfa mpaka sasa, wamekufa wapi? Majina yao ni nani? Umewahi kusikia wizara ya afya iseme?

Sitarudi hapa mpaka ujibu maswali yangu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom