Kibonoka genius

Kibonoka genius

mickey drizzy

Member
Joined
Jun 19, 2015
Posts
30
Reaction score
3
Wazee wawili walikua wamekaa chini ya mti wakizungumza kuhusu watoto wao huku kila mtu akimsifia mtoto wake:

BABA KIBONOKA: Wewe huniambii kitu, mwanangu ana akili kuliko hata wako
BABA KIPONDO: Mwanao zero tu hana kitu
BABA KIBONOKA: Aaah! wewe humjui yule, hapa kwenyewe yupo ndani anajisomea
BABA KIPONDO: Aaah wapi.. labda sio Kibonoka ninaemjua mimi.. aache kucheza asome? mwenzake Kipondo yuko ndan anasoma
BABA KIBONOKA: Acha kuzuga wewe muite wako na mimi nimuite wangu
BABA KIPONDO: We KIPONDO
KIPONDO : Naam
BABA KIPONDO : Njoo na ulichokua unakifanya

Mara akatoka Kipondo akiwa amebeba madaftari yake
KIPONDO : Hii hapa baba
BABA KIPONDO: Baba Kibonoka umeona? haya muite wako

BABA KIBONOKA HUKU AKIJIAMINI: We "KIBONOKA"
kimya
We "KIBONOKA" si nakuita huniskii au dharau hebu njoo na hayo madaftari yako

KIBONOKA AKAITIKA AKIWA JUU YA ULE MTI: Daaaah! Mzee kausha kwanza nimtoe huyu ndege maana nimetega tangu juzi asubuhi hata shule sijaenda...

Kama wewe ndo baba, ungefanyaje?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom