Kibonde wa Jahazi-Clouds anaboa

Kibonde wa Jahazi-Clouds anaboa

Huo mpira akatangazie wapi wakati hata hapo clouds hajawahi kuitwa kwa kipindi cha michezo cha sports extra, NHC walishamaliza kazi yao.

You're very Stupid. Kila Weekend Yeye ( Ephraim Kibonde ), Maulid Kitenge, Ibrahim Masoud Maestro, Oscar Oscar na Edward Kumwembe ' Edo ' huenda Kufanya Match Commentaries and Analysis huko SuperSports / Dstv hasa kwa michezo ya Ligi za Ulaya isipokuwa Wao hufanya kwa lugha ' adhimu ' ya Kiswahili.

Baada ya ' ufafanuzi ' wangu naomba usinipotezee tena muda kwani nadhani ' Kiwango ' chako cha ' IQ ' ni kidogo sana kuweza ' kushindana ' na Mimi. Ila ningekushauri tu kwamba siku zingine kabla ' hujakurupuka ' kutaka ' Kujibizana ' na Mtu humu JF tena nadhani hasa hasa GENTAMYCINE basi jitahidi mno ujiridhishe ' Kidata ' vinginevyo ' ukijipendekeza ' kama hivi Mimi ' nitakuwasha ' tu.
 
Cha pombe huyo. Kila siku dental formula inazidi kubadilika maana meno yanadondokea kwenye beer
 
Povu

Sent from my iPhone 8 using JamiiForums mobile App

Hivi haya maneno ya chini ya post (sent from simu fulani) hivi huwa ya kweli?
Sent from my iPhone 9 using JamiiForums mobile
 
Ahamishiwe kwenye ala za roho akapambane na Diva
 
We kibonde yuko vizuri na ananogesha vizuri kipindi .mambo mengine ni yakawaida

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
 
Mi naona ni attitude yako dhidi yake tu bana...jamaa huwa ni mcheshi na anamzaha sana na asipokuwepo kny kipindi hata hufuhii jioni yako..asikudanganye mtu mimi hutumia simu kumsikiliza manake mara nyingi huwa sijafika home.
 
Ningewashaurini tu kuwa achaneni nae na msipoteze muda kwani humu JF ' threads ' za kumsema Mtangazaji Ephraim Kibonde nadhani ni nyingi mno lakini pamoja na ' Kunangwa ' kote huko bado ' Jamaa ' ni sikio la kufa lisilosikia dawa na kibaya zaidi kwetu Sisi tunaomsema kila kukicha tupo zetu hapa hapa ' Bongo ' tuki ' hustle ' wakati Yeye mwenzetu kila ' Weekend ' lazima akwee Pipa / Mbung'o / Ndege kwenda ' Jozy ' Johannesburg Afrika ya Kusini kutangaza mechi za Super Sports Swahili na pia ameshaingia ' Mkataba ' mnono mno na Watu wa NHC na bado pia ni Mtangazaji ' Mwandamizi ' Clouds Media Group na usisahau kuwa ni MC mmoja mkubwa mno hapa Tanzania bila kusahau pia kuwa ni Dj mzuri sana.

Na sisi badala ya ' Kumnanga ' kila kukicha humu JF basi ningeomba tu na sisi tujitahidi ' Kuwajibika ' ili angalau basi tuweze kufikia hata robo tatu ya mafanikio yake.
Ss tunakula biaa na tukija kwako tutakunywa zako biaaa,bia bariiiidi!
 
Habarini,

Mi ni msikilizaji wa Clouds Redio kwa baadhi ya vipindi kikiwemo kipindi cha JAHAZI kinachoanza jioni majira ya saa kumi mpaka moja jioni.

Katika kipindi hiki E. Kibonde ni mmoja wa watangazaji wa kipindi hicho.
Mara kwa mara huyu jamaa amekuwa akileta stori sana za mapenzi.

Yani amekuwa akiongea mambo mengi yenye maudhui ya mapenzi na imekuwa kawaida yake sana, nafikiri wale watangazaji wenzake huwa wanakuwa karibu na 'kitufe' cha kuruhusu tangazo liende hewani maana wakati mwingine huwa wanamkatiza kabla ya kumaliza stori zake hizo ambazo anaona zinafaa.

Nimemfatilia sana kwa vipindi kadhaa na nimegundua kuwa yupo hivyo. Yani wakati mwingine hata kama stori wanayoongelea haihusiani kabisa na mapenzi yeye ataileta ataivuta mpaka tu ije kumalizika kwa kitendo cha mapenzi.

Kipindi hiki si cha majira ya usiku hivyo huweza kusikilizwa na kila rika maana ile siyo bia kusema hairuhusiwi kwa walio chini ya umri wa miaka 18, hivyo hata walio wadogo husikiliza.

USHAURI WANGU:
Kama mmoja wa wadau wa kipindi chao cha JAHAZI nashauri aache hiyo tabia, na kama anapenda sana hizo stori basi aombe wampangie kipindi cha usiku na Diva wakaongelee huko usiku.

OVER.

Sent from my SM-J110H using JamiiForums mobile app

unammana anaongelea mambo ya ngono au mapenzi, kama ni mapenzi mimi sioni tatizo, labda kama anaomngelea na kuhamasisha ngono na ufuska.
Mapenzi yana run dunia mkuu hujui?
 
Radio kibao sana mji huu.Kama umekerwa huku hamia kule.Acha kujipa stress za ajabu mkuu
Lakini karibu redio na TV zote zinafanafanana sasahivi,
Sisi wengine kuna habari hatuwezi kukaa kuzisikiliza tukiwa na watu tunao heshimiana nao sana kama wakwe, kwahiyo ikiwa ni nyumbani nitaweka channel ya dini au wanyama, japo siku moja nilikosa pa kukimbilia, mama mkwe kakaa hapo nilipoweka channel ya dini nilikuta kinaendelea kipindi cha masuala ya ndoa wanazungumzia umuhimu wa tendo la ndoa ndani ya ndoa, nikapiga chini nikaweka channel ya wanyama nikakuta Sokwe wanapandana loh!!, ikabidi nirudi kuwaangalia watangazaji aina ya Kibonde, huyu jamaa ni nguli wa kuchomekea masuala ya mapenzi kwenye vipindi, kwahiyo msije mkashangaa siku akichomekea suala la mapenzi kwenye kipindi cha maisha ni nyumba
 
Huo mpira akatangazie wapi wakati hata hapo clouds hajawahi kuitwa kwa kipindi cha michezo cha sports extra, NHC walishamaliza kazi yao.
Ataweza wapi kutangaza mchezo wa kasi kama mpira si atajing'ata na maiki itajaa mate
 
Walimwengu tuacheni maneno manenooo, tutazame dunia hii inavyokwenda mbelee, waache waseme, mwisho watachoka, ngoma ya sikinde, tunaiendelezaa

Sent from my TECNO-W3LTE using JamiiForums mobile app
 
Kwanini usiwe unabadilisha station anapoongea mapenzi? Halafu hujui kuwa asilimia 99.99 ya matamanio yote ya binadamu ni mapenzi? Waulize akina Adam na Hawa au Eva pale edeni mwenyewe alipowaambia wasijaribu ikashindikana. Kurudi anakuta wameshakula tunda

Sent from my SM-N9005 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom