Malingumu
JF-Expert Member
- Apr 5, 2012
- 616
- 433
Habarini,
Mi ni msikilizaji wa Clouds Redio kwa baadhi ya vipindi kikiwemo kipindi cha JAHAZI kinachoanza jioni majira ya saa kumi mpaka moja jioni.
Katika kipindi hiki E. Kibonde ni mmoja wa watangazaji wa kipindi hicho.
Mara kwa mara huyu jamaa amekuwa akileta stori sana za mapenzi.
Yani amekuwa akiongea mambo mengi yenye maudhui ya mapenzi na imekuwa kawaida yake sana, nafikiri wale watangazaji wenzake huwa wanakuwa karibu na 'kitufe' cha kuruhusu tangazo liende hewani maana wakati mwingine huwa wanamkatiza kabla ya kumaliza stori zake hizo ambazo anaona zinafaa.
Nimemfatilia sana kwa vipindi kadhaa na nimegundua kuwa yupo hivyo. Yani wakati mwingine hata kama stori wanayoongelea haihusiani kabisa na mapenzi yeye ataileta ataivuta mpaka tu ije kumalizika kwa kitendo cha mapenzi.
Kipindi hiki si cha majira ya usiku hivyo huweza kusikilizwa na kila rika maana ile siyo bia kusema hairuhusiwi kwa walio chini ya umri wa miaka 18, hivyo hata walio wadogo husikiliza.
USHAURI WANGU:
Kama mmoja wa wadau wa kipindi chao cha JAHAZI nashauri aache hiyo tabia, na kama anapenda sana hizo stori basi aombe wampangie kipindi cha usiku na Diva wakaongelee huko usiku.
OVER.
Sent from my SM-J110H using JamiiForums mobile app
Mi ni msikilizaji wa Clouds Redio kwa baadhi ya vipindi kikiwemo kipindi cha JAHAZI kinachoanza jioni majira ya saa kumi mpaka moja jioni.
Katika kipindi hiki E. Kibonde ni mmoja wa watangazaji wa kipindi hicho.
Mara kwa mara huyu jamaa amekuwa akileta stori sana za mapenzi.
Yani amekuwa akiongea mambo mengi yenye maudhui ya mapenzi na imekuwa kawaida yake sana, nafikiri wale watangazaji wenzake huwa wanakuwa karibu na 'kitufe' cha kuruhusu tangazo liende hewani maana wakati mwingine huwa wanamkatiza kabla ya kumaliza stori zake hizo ambazo anaona zinafaa.
Nimemfatilia sana kwa vipindi kadhaa na nimegundua kuwa yupo hivyo. Yani wakati mwingine hata kama stori wanayoongelea haihusiani kabisa na mapenzi yeye ataileta ataivuta mpaka tu ije kumalizika kwa kitendo cha mapenzi.
Kipindi hiki si cha majira ya usiku hivyo huweza kusikilizwa na kila rika maana ile siyo bia kusema hairuhusiwi kwa walio chini ya umri wa miaka 18, hivyo hata walio wadogo husikiliza.
USHAURI WANGU:
Kama mmoja wa wadau wa kipindi chao cha JAHAZI nashauri aache hiyo tabia, na kama anapenda sana hizo stori basi aombe wampangie kipindi cha usiku na Diva wakaongelee huko usiku.
OVER.
Sent from my SM-J110H using JamiiForums mobile app