Kibiti: Polisi yaua watu wanne(4) wanaodhaniwa kujihusisha na mauaji wilayani humo

Polisi ni madaktari??Walijuaje wamekufa wakiwa njiani kuwapeleka hospitali??Inawezekanaje watu 4 wajeruhiwe halafu wote wafe wakiwa njiani kupelekwa hospitali?Kuna jambo hapa haliko sawa!
Polisi wametengeneza sinema feki pasipo kujua kuwa watanzania wa sasa wapo makini wanajua kila maigizo
 
Wana uhakika? Isije ikiwa ni raia wema. Vinginevyo Good work

Use common sense Mkuu. Hivi Raia Mwema anaweza akaona Police wanakuja akakimbia porini na akakutwa na Silaha hatari ya SMG? Umeyasoma vizuri lakini hayo maelezo ya Police?
 
Inafahamika vema kabisa kwamba maeneo mengi tu polisi wamekua wakipambana na halifu mbalimbali.

Kwa mfano kariakoo polisi walipambana Na majambazi yakiiba Kwa kutumia siraha, mbeya polisi waliwafukuzia majambazi walioiba pesa benki nk

Sasa inawezekana mkoa wa pwani kuna makundi hayo pia. Kutokana na mauaji yanayoendele Kwa Sasa ni dhahiri sasa kuna kundi jipya la uharifu linalowaua viongozi wa mitaa,vijiji,kata Na polisi.

Ndio maana taarifa inasema WANAOSADIKIWA, maana haijajulikana Kama ni majambazi wa kawaida tuliowazoea kila siku ama ndio wale wa mauaji ya kibiti.
Safi sana na ninakuelewa.

Kwa muktadha wa maelezo yako ku ''rush'' kwa kusema 'wanaosaidikiwa' ni dalili ya kutaka ku appease (kuridhisha) kuna linaloendelea kuhusiana na mauji ya Pwani.

Sioni kama ni tatizo kubwa, tatizo ni kupoteza focus

Kama ulivyosema itaonekana majambazi ya Pwani yanakabiliwa vema.
Ikitokea hakuna matokeo mazuri kutakuwa na tatizo la kufafanua ni kwanini

Picha katika vichwa vya wanajamii ni kuwa yanauawa ambayo ni mapema mno kuiweka machoni

Nadhani Polisi walitakiwa kujiridhisha kwa forensic exam kuwa kuna uhusiano na mauaji au la
Kisha ifuate taarifa kamili bila kuwepo maneno 'inasadikiwa'
 
Polisi ni madaktari??Walijuaje wamekufa wakiwa njiani kuwapeleka hospitali??Inawezekanaje watu 4 wajeruhiwe halafu wote wafe wakiwa njiani kupelekwa hospitali?Kuna jambo hapa haliko sawa!
Kabisa Mkuu, halafu tujiulize,

1. Kwa nini wanadhani ni wauaji?

2. Kwa nini wamewaua wote bila Kuacha wa kuwasaidia kufanya upelelezi?

3. Je polisi imepata madhari gani?

4. Maiti za waliouwawa tunaweza kuonyeshwa?

Nahisi tunajengwa kisaikolojia, ili tuamini kuwa sasa hali ni shwari.
"TIME WILL TELL US THE TRUTH"
 
Wanaodhaniwa? Kulikuwa na sababu gani iliyowafanya waonekane ni wauaji hadi na wao kuuawa?

Hili swala la polisi kujifanya wao ndio Judge, Jury and Executioner sidhani kama italeta amani.


Correction.

Ndio maana tunasema mnaanzisha sredi humu muwe na habari kamili. Sasa mtu mwanzon alileta akisema wanadhaniwa. Muda huu naona sredi iko tofauti na mwanzoni.
Usipost sredi kama bado huna uhakika.
Ukianza kuwarushia risasi polisi wewe utakua ni mtu wa amani kweli na hali kama ya kibiti. Hata kama tunawachukia mapolisi lakini tujaribu pia kuwa wakweli.
 
Jeshi la Polisi nchini limefanikiwa kuwaua wahalifu wanne wanaosadikiwa kuwa miongoni mwa wahalifu wanaoendesha mauaji katika wilaya za Mkuranga, Kibiti na Rufiji katika mapambano yaliyodumu kwa zaidi ya nusu saa katika kijiji cha Pagae wilayani Kibiti mkoani Pwani.

Akielezea tukio hilo Mkuu wa Oparesheni Maalumu za Jeshi la Polisi, Naibu Kamishna wa Polisi Liberatus Sabas alisema tukio hilo lilitokea siku ya Alhamisi juni 29 majira ya saa tatu usiku kwenye barabara ya vumbi itokayo Pagae kuelekea Nyambunda ambapo Askari Polisi wakiwa doria walikutana na kikundi cha watu kinachokadiriwa kuwa na watu sita ambapo wahalifu hao baada ya kuona gari la Polisi walikimbilia vichakani na kuanza kuwarushia risasi Polisi.

Sabas alisema baada ya hali hiyo kutokea Askari nao kwa ujasiri walijibu na mapambano hayo yalidumu kwa zaidi ya nusu saa ambapo Polisi walifanikiwa kuwajeruhi wahalifu wanne kwa risasi ambao baadaye walifariki dunia wakiwa wanapelekwa hospitali.

"Katika tukio hilo tumefanikiwa kupata silaha mbili aina ya SMG na magazine mbili pamoja na risasi 17 zilizokuwa zinatumiwa na wahalifu hao na hii ni dalili kuwa tunaendelea vizuri na oparesheni yetu ambayo inashirikisha vyombo vingine vya ulinzi na Usalama katika wilaya hizi tatu za Mkuranga, Kibiti, na Rufiji" Alisema Sabas.

Aidha Sabas ametoa wito kwa wahalifu wengine kuacha mara moja kufanya vitendo hivyo kwa kuwa vyombo vya ulinzi na usalama vinaendelea kufanya jitihada zote za kuhakikisha kuwa maeneo hayo yanakuwa salama na wananchi wanaishi katika hali ya amani na usalama.

Vilevile amewataka wananchi kutoa taarifa zitakazowezesha kupatikana wahalifu wengine ili kuhakikisha kuwa kila mmoja anaishi kwa usalama ambapo kwa ambaye atakayetoa taarifa zitakazowezesha kupatikana kwa wahalifu hao kiasi cha shilingi milioni kumi kitatolewa na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro.


Chanzo: ITV
Ngoja tusubiri kama watajibu mapigo.. counter attack iwe 1-1... maana dude limeamshwa hilo
 
Hongera sana polisi naona kwenye hayo "mapambano" hakuna polisi aliyejeruhiwa ila "raia wanaohisiwa ni wahalifu" wamekufa!!
 
Sasa mkuu unadhani watu kama hao wanakubali kukamatwa wakiwa hai? Na umesikia jamaa walianza kurusha risasi. Hata S.W.A.T na FBI huwa wanawauwa watuhumiwa hasa kama ni cop killers.
iweje polisi wasijeruhiwe? hapo hakukuwa na mapambano bali waliwakamata wakawapeleka porini na kuwaua kisha wakazuga kuwa yalikuwa mapambano ya Nusu saa tu tena gizani? Wametengeneza sinema pasipo kutafakari kuwa watanzania wameamka uwezo kutambua mbinu zao,
 
Wamesema inasadikika au kudhaniwa kwa sab hawana uhakika kwa sab hawezi kusema wamefariki lkn cha msingi ni wahalifu.
Yes sina tatizo na suala la uhalifu. Ninachosema ni kuwa Polisi kutumia maneno 'inasadikiwa' ni kutoa picha wasio na uhakika nayo kama ulivyosema (Hawana uhakika).

Ikiwa hawana uhakika kauli muhimu ni mapambano kati yao na majambazi hadi watakapopata uhakika wa aina ya majambazi. Je, ni majambazi yanayopora tu au ni Majambazi yanayohusiana na tukio

Hapa tunakuja katika hoja nyingine kuwa yanapotokea mauaji au uhalifu lazima kufanyike uchunguzi utakaokusanya kila ushahidi katika tukio. Siku nyingine likitokea jingine ni rahisi ku link matukio

Kama kuna maganda ya risasi kwa mauaji yaliyopita, yanaweza kuoanishwa na silaha kujua kama ndzo zimetumika. Kwa nchi za wenzetu hata alama kama fingerprint zinatumika

Ndio maana nchi za wenzetu likitokea tukio la aina yoyote kuna ule uzi wanaoweka na kukusanya kila kinachoonekana kinaweza kuwa na maana katika uchunguzi hata kama ni shanga, sindano n.k.

Kuna lugha inayotumika kwa wenzetu 'person of interest' hadi uchunguzi utakapobaini ni kitu gani
 
Inawezekana waliuwaua hao raia kwa makosa ili kubalanzisha stori lazima watangaze walikua wanapambana nao kwa nusu saa.
Alafu wahalifu 4 walijeruhiwa na wote wakafa wakiwa njiani kuelekea hospitali. Ngoja tuwasikilize wakina marijani tushawazoea hao.
 
Kama habari hii ni kweli lipo tatizo

Kudhania tu hakumfanyi mtu kuwa na hatia na adhabu!
Kumbuka kuwa hairuhusiwi kwa RAIA kutembea usiku kwa maeneo hayo. Hawa walikuwa wanatembea usiku tena kama kikundi halafu wakiwa na silaha! Bado mnawatetea!
 
Polisi wamewahi kuua MTU hadharani wakati wanaanza operesheni hii kwa njia ya fujo wizi na uporaji na ubakaji ,wameua kijiji cha Jaribu wakaiba vijiji vya Jaribu huko kibiti na Njopeka huko mkuranga
 
Back
Top Bottom