Mzee wa ruksa naye bana, inasemekana kuwa yeye ndiye JK anamtumia sasa hivi kutuliza migawanyo ndani ya ccm.
Kutakuwa tu na maelezo mazuri ya kwanini hili limeruhusiwa kupigwa picha na kuwekwa kule kwa mzee wa propaganda za ccm - michuzi.
Hapo ujumbe ni upi..binafsi zijaweza kuwaelewa hawa watu kabisaa!!
Zaidi ni kuwa hiyo blogu ya masupu nimeiondoa kabisa kwenye favourites zangu kwa sababu iko too biased.
Kwanza katika blog ambazo nilikuwa naziamini kiasi kwamba siwezi pitisha siku bila kuipitia ni blog ya bwana michuzi, ila kwa sasa najionea kichefuchefu kabisa kuifungua kwani najua lazima takutana na habari na picha za watu wa ccm zaidi ya asilimia 80. Ule usemi wake wa sibagui sichagui atayenizika simjui ni danganya toto tupu, kwani ameshindwa kabisa kuficha hisia zake kuwa yeye ni kada wa kutumainiwa wa ccm.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.