jingalao
JF-Expert Member
- Oct 12, 2011
- 35,053
- 28,245
Kwa mwenendo wa kisiasa nchini mtakubaliana nami kuwa uchaguzi mkuu 2015 ni mwisho wa wabunge waliozoea kuchaguliwa kwa mkumbo wa bendera ya ccm.
Nasema hivi kwa kuwa chama changu kimepoteza na kitazidi kupoteza mvuto na hivyo kufanya sifa ya mgombea kuwa kigezo muhimu cha kupata ubunge.
Isitoshe,mwaka 2015 kutakuwa na ushindani mkali kiasi cha kuacha kila mgombea kujipigania kivyake na sio chama kupigania wagombea.
Kwa upande wa wagombea wa chadema hali itakuwa kinyume kwani bendera ya chama chao au tuseme vuguvugu la chama litawabeba wagombea.
Ni wazi wananchi wanaopenda mabadiliko wataamua kuzitupia kura zao kwa chadema bila kujali sifa za wagombea huku wakitumia umakini mkubwa katika kuamua wanaccm wachache kurudi au kuingia bungeni.
Ni muda wa kujipanga kibinafsi kama unataka kushinda uchaguzi kupitia ccm!ni muda wa kujipanga kwa kujiweka mbali na uchafu uliovikwa chama cha ccm.
Ni hayo tu kwa leo!
KWA HISANI YA MTU WA TANZANIA
Nasema hivi kwa kuwa chama changu kimepoteza na kitazidi kupoteza mvuto na hivyo kufanya sifa ya mgombea kuwa kigezo muhimu cha kupata ubunge.
Isitoshe,mwaka 2015 kutakuwa na ushindani mkali kiasi cha kuacha kila mgombea kujipigania kivyake na sio chama kupigania wagombea.
Kwa upande wa wagombea wa chadema hali itakuwa kinyume kwani bendera ya chama chao au tuseme vuguvugu la chama litawabeba wagombea.
Ni wazi wananchi wanaopenda mabadiliko wataamua kuzitupia kura zao kwa chadema bila kujali sifa za wagombea huku wakitumia umakini mkubwa katika kuamua wanaccm wachache kurudi au kuingia bungeni.
Ni muda wa kujipanga kibinafsi kama unataka kushinda uchaguzi kupitia ccm!ni muda wa kujipanga kwa kujiweka mbali na uchafu uliovikwa chama cha ccm.
Ni hayo tu kwa leo!
KWA HISANI YA MTU WA TANZANIA