Khitma ya Juma Mwapachu

Khitma ya Juma Mwapachu

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
22,454
Reaction score
32,980
KHITMA YA JUMA MWAPACHU
Ndugu na jamaa leo walikusanyika nyumbani kwa Juma Mwapachu kusoma khitma.
Mtume SAW kifo kinatosha kuwa mawaidha.

Kwangu binafsi kuwa kwenye nyumba ile kulirejesha kumbukumbu nyingi za furaha nikiwa na marehemu ukumbini kwake tukizungumza mengi.

Halikadhalika katika hadhira ile niliwaona watu wengi ambao kwa namna moja au nyingine walirejesha fikra zangu kwa marehemu.

Katika wengi tuliohudhuria khitma hii sisi wakati wa uhai wake Juma Mwapachu alikuwa kaka mkubwa kwetu kwa kila hali.

Juma Mwapachu alitutangulia sisi kwa kila kitu kuanzia kuingia Chuo Kikuu hadi katika ajira iwe serikalini, shirika la umma au binafsi.

Juma Mwapachu alikuwa mwanafunzi wa University of East Africa wakati sisi wengi wetu tuko sekondari.
Katika niliowaona pale khitmani waliosoma University of East Africa alikuwa Mohamed Ismail na Prof. Issa Shivji.

Waliobakia niliowafahamu walisoma Dar es Salaam University na hatukulikuta hata vumbi lake pale chuoni.
Juma Mwapachu kwa wengi wetu tuliokuwa pale kama nilivyosema alikuwa kaka.

Sasa nawaangalia wale wa rika la kaka Juma Mwapachu Yusuf Kalala, Mohamed Ismail, Prof. Issa Shivji wote wamejikusanya wamekaa pamoja.

Miaka imekwenda lakini wanapendeza.
Katika hawa kwangu mimi kila mtu ana historia ya yake ya kupendeza.

Issa Shivji alitikisa bongo za wasomi wengi wa wakati ule kwa kitabu chake, "Class Struggles in Tanzania."
Kwa nyakati zile kitabu hiki kilikuwa kitabu cha kutisha.

Kaka Yusuf Kalala mwanafunzi wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika Muslim School kipi asichokijua kuhusu Dar-es-Salaam?

Siku moja namwambia Bi Bahai keshafariki.
Akaniambia yu hai.

(Kulikuwa na Bahia wawili na wote maarufu - Bi. Bahia Lumelezi na Bi. Bahia mke wa Sheikh Mzee Ali Comorian. Mmoja katika hawa ndiye aliyekuwa kutangulia mbele ya haki).

Juma Mwapachu alipanda mabega ya Mohamed Ismail kukwea mlingoti uliokuwa unapeperusha Union Jack kuiteremsha chini katika maandamano dhidi ya Uingereza kutochukua hatua Ian Smith alivyotangaza uhuru wa Southern Rhodesia yaani "Uniletaral Declaration of Independence," maarufu UDI.

Wanafunzi wa Chuo Kikuu walikuwa wameandamana kutoka Mlimani kuja Ubalozi wa Uingereza.
Wanafunzi walikuwa wamejaa ghadhabu.

Huu ulikuwa mwaka wa 1965.
Juma Mwapachu na Mohamed Ismail wote wanafunzi wa sheria walikuwa vijana wadogo.

Kisa hiki alinihadithia Mzee Ahmad Rashaad Ali aliyeshuhudia tukio hilo kwa macho akiwa na akiwajua hawa watoto kama alivyopenda kuwaita.

Mzee Rashaad akisema Juma Mwapachu alikuwa akiendeleza vile vita vya baba yake Hamza Kibwana Mwapachu dhidi ya Waingereza wakati wa kupigania uhuru wa Tanganyika.

Tulipokuwa tunachukua chakula akanijia mtu akaniuliza kwa nini nimekataa kuzungumza.
Nilikuwa nimesimama na Chief Edward "Ted" Makwaia wa Siha, Usukuma.

(Ted ndiye aliyenijulisha kwa Juma Mwapachu mwaka wa 1967).
Nilimjibu kuwa sikukataa ila nasaa walizotoa masheikh zetu zilitosha.

Lakini kama ingekuwa hadhira nyingine si khitma ningeeleza kisa hiki cha kutunguliwa bendera ya Mwingereza Juma Mwapachu kapanda mabega ya Mohamed Ismail kuuparamia mlingoti wa Union Jack.

Lakini kisa hiki ningekieleza kwa urefu kama alivyonihadithia Mzee Rashaad kuanzia jana yake Mzee Ahmed Rashaad akiwa Deputy Permanent Secretary Information alipokwenda nyumbani kwa Mwalimu Nyerere kutaka kauli yake kuhusu tatizo la Rhodesia ili Wizara ya Habari itoe "Press Release."

Rashaad alikumkuta Mwalimu nyumbani kwake anazungumza na Dossa Aziz na Lucy Lameck.
Kuna stori kubwa Nyerere alimhadithia Mzee Ahmed Rashaad Ali.

1746302550925.jpeg

Kushoto: Wakili Mohamed Ismail, Shariff, Yusuf Kalala, Prof. Othman Chande na Ali Boxer
1746302592332.jpeg
 
Mmojawapo ya familia zilizonufaika sana kupitia kutambulika na kupewa fursa na Nyerere
 
Uhuru wa Tanganyika ni kama tulipewa tu na makoloni, hakukuwa na mapambano makubwa.
Yoda,
Soma kipande hicho hapo chini:

''Tarehe 1 Februari, 1950, makuli walifanya mgomo mkali sana ambapo walipambana
vilivyo na askari wa kuzuia fujo.

Serikali ilichukulia kuwa migogoro ya mara kwa mara ya makuli ni siasa za vurugu na
fujo dhidi ya serikali.

Serikali iliwatuma askari wa kuzuia fujo (Kavirondoí kama walivyokuwa wakiitwa na watu
wa Pwani) wakakomeshe mgomo.

Hawa Kavirondo walikuwa askari toka bara waliojulikana kwa upofu na ukatili wao katika
kutekeleza amri za kikoloni.

Aghalabu walikuwa, kama kanuni, wakipelekwa kufanya kazi mbali na makwao ili wasipambane na watu wa kwao, endapo itabidi kuamriwa hivyo.

Kavirondo walionekana kama vibaraka wa wakoloni na watu washenzi.

Katika mapigano baina ya Kavirondo na makuli, Kavirondo 19 waliuawa.

Makuli wengi walikamatwa, wakatupwa rumande na mashitaka ya jinai
yalifunguliwa dhidi yao.

Mwezi Juni, 1950, Dockworkers Union ilivunjwa kwa amri ya mahakama na shughuli za vyama vya wafanyakazi hazikuibuka tena hadi mwaka 1955 baada ya kuasisiwa kwa TANU.''

Endelea kusoma...

''Kanda ya Ziwa, Bukoba mwanasiasa mkongwe Ali Migeyo, akiwa na umri wa 53
alikuwa akihangaika kufungua matawi ya TAA katika jimbo la Ziwa Magharibi.

Akiwa Kamachumu katika kampeni hii, Migeyo alishambuliwa na mabomu ya
kutoa machozi alipokuwa akihutubia mkutano wa hadhara.

Migeyo alikuwa na kipawa cha kuzungumza na hotuba zake zilikuwa za kusisimua kiasi kwamba ilikuwa rahisi sana kwake kuwapandisha watu jazba.

Siku ile ya mkasa wa mabomu alikuwa akiwaandaa wananchi kuipokea TANU.

Alipokuwa akihutubu askari walikuja kuwatawanya watu kutoka kwa viwanja vya
mkutano.

Mabomu ya machozi yalitupwa na Migeyo akatiwa mbaroni.

Tarehe 14 Aprili, 1954 Migeyo alihukumiwa kifungo cha miaka 3 kwa kufanya mkutano bila ya kibali.''
(Kutoka kitabu cha Abdul Sykes).
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom