Khalifa: Waandishi wa Habari wanayo haki ya kutoa maoni yao, sio jukumu la JAB kuwaonya

Khalifa: Waandishi wa Habari wanayo haki ya kutoa maoni yao, sio jukumu la JAB kuwaonya

Nyakijooga

JF-Expert Member
Joined
Dec 9, 2018
Posts
427
Reaction score
666
Mwandishi wa Habari Khalifa Said amesema kuwa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imekuwa ikitumia mamlaka yake kinyume na sheria kwa kuwachukulia hatua waandishi wa habari wanapotoa maoni yao, hasa wanapokosoa upande wa Serikali. Amesema kuwa jukumu la JAB ni kusimamia maadili ya uandishi wa habari, si kudhibiti maoni ya waandishi.

Katika video aliyoichapisha kwenye ukurasa wake wa Facebook, Khalifa amesema kuwa waandishi wa habari wana haki ya kikatiba ya kutoa maoni yao kama walivyo watu wengine.
 
Magazeti ya kufungia hayapo tena yote yanapamba watawala tu hivyo bila huko kujitutumua hawana cha kufanya.

Kazi yao ni kusimamia maadili ya uandishi au maadili ya waandishi?
 
Back
Top Bottom