Chakula cha KFC sikielewi kabisa

SweetyCandy

JF-Expert Member
Joined
Sep 17, 2022
Posts
5,225
Reaction score
9,916
Naomba msaada wa hili .
Ukienda mfano bar au mgahawa unasikia harufu za kupikwa za vyakula na pia asubuhi namapema unaonavitu vinaletwa soda , maji, na vyakula vibichi. Ili vipikwe .

Ila ukienda KFC HUONI CHOCHOTE KILICHOPIKWA WANATOA TU KWENYE TREI ZAO MNACHUKUA . ILA KUONA WANAVYOPIKWA HAKUNAGA .

nyie hamshtuki??
Msaada
 
Fast food aka hutakiwi kukaa kusubiria Chakula. KFC ni fast food restaurant, vitu vinawekwa spice na kila kitu vinakaa kwenye fridge vinasubiria order vinaonjeshwa mafuta unakula.

Sio Tu KFC Bali fast food zote zipo hivyo, Merry brown, subway etc.
 
Hapo unataka kuona mpishi ametoka jikoni jasho linamtiririka.
Amekaa kwenye kiti anakunywa Pepsi.

Unataka kuona mdada anaosha vyombo vichafu

Unataka kuona wamewekwa kwenye beseni kubwaa wanachanganya na viungo.
Huku ukusikia mpeleekee fundi maiko supu na chapati tatu,


Huku muhudumu anaimba natesa aaah na ndiyo maana niko vzr iiih lengo anamchamba boss wake a mama wa chapati ..........


Huku mteja mie natega sikio nisikie kulkoni..... Misemo

Huku dada mwingine kakunja mdomo mithili ya kudaiwa Kodi ya mwezi akiosha vyombo huku muhudumu mwingine aliyevurugwa na mwenziwe akisimama mbele ya mteja huku mdomo kaukunja kama ngano iliyokandwa jana jioni

Cc Seran mamnyong'ode
 
Wewe endelea kula huko huko kwa mama ntilie. KFC, Macdonald, tuachie sisi
 
Saratani za baadae hizo watu wapige hela
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…