Kete ya CCM urais 2015 naiona kwa Wasira

Kete ya CCM urais 2015 naiona kwa Wasira

Utafiti:Ni neno panai sana...lkn kitaalamu ukitaka kujiridhisha na tafiti nyingi za kisiasa hasa zinazohusu nani anafaa kuwa kiongozi....tafiti nyingi huwa zinakosa VALIDITY NA RELIABILITY.
Kwa kutumia macho na maskio pamoja na fikra,Wasira ni kati ya watu wanaotumiwa na CCM katika kitengo cha propaganda..."Yaani kuwaondoa watu kwenye logic"kiufupi hiyo ndiyo kazi ya Akina LUKUVI,NAPE,LUSINDE nawengine wa jinsi hiyo.
Ukizingatia sifa za uraisi Wasira hana sifa ya UMAKINI wa kumtosha kusimamia nchi kama RAISI.Hii ni sawa na kumwajiri Msanii kuwa Dakitari wa upasuaji.
Wito kwa mtoa mada.ni kweli Wasira anataka uraisi na alishaanza harakati jimboni kwake mapema sana.lakini ukitaka kujua Wasira anaweza kuwa raisi au hawezi nenda jimboni kwake BUNDA kawaulize wananchi,nakushauri uanze na tarafa ya chamriho umalizie na Bunda mjini,then uelekee makao makuu ya chama ukachunguze cv yake kwenye chama kama inamruhusu kwa mjibu wa katiba ya CCM.ukijiridhisha rudi utwambie kama DATA zako ziko VALID na RELIABLE kwa kiasi gani.
 
Kuna candidate mmoja muhimu sana mnamsahau!! Tena Kijana anaetakiwa kWa kipindi hiki ! Eddo anatakiwa aweze kuunda nae kambi mpya na kusahau yaliyopita kama wanayo!! EN!
 
Nitafurahi tukipata Rais Kijana mwenye fikra mpya na mawazo mapya. January na Mwigulu nawaombea mmoja wao apate nafasi ya kutiongoza.

umeruka maji ukaingia kwenye tope. Hakuna anayefaa kati ya hawa. Basically sasa hivi CCM hawana any presidential figure. Tusubiri labda atatokea as we get closer to October next year.
 
Jamani mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni. Hakuna mtu mwingine mwenye uthubutu wa kukemea maovu zaidi ya Lowasa. Kila mtu anafahamu alivyokua mchapa kazi akiwa waziri mkuu. Hii ya kujiuzulu uwaziri, hakujiuzulu kwakuwa kausika kuchukua pesa. Bali aliwajibika tuu kama waziri mkuu. Mchagueni airekebishe nchi hii ambayo kikundi cha watu wachache wanagawana rasilimali za nchi kama nchi ni ya kwao wenyewe. Tatizo kubwa ambalo tunalo wananchi ni kwamba tunakwenda kwa ushabik wa vyama. Tukitaka mafanikio ktk nchi hii, kwanza kabisa tuacheni ushabik wa kivyama. Zote tuungane tumchague mtu atakaetusaidia kuiondoa hii hali iliyoko kwa sasa hivi ambae sii mwingine ni EDWARD NDOYAA LOWASA. Mpeni kura zenu wote na hamjajutia.

Naomba nikufahamishe kuwa mtu mwenye shaka ya uadilifu hata kama ni mtenda kazi maamuzi yake yanakuwa double standards kwenye issue ambayo anakuwa hana maslai maamuzi yake yanakuwa tofauti na mahali ana maslai. Ni ngumu sana kwa kiongozi ambaye uadilifu wake ni wa mashaka kuaminika na ambaye yiko tayari kutumia fedha kupata madaraka ni hatari.
Ni kweli jamaa ni mjasiri katika kuchukua maamuzi lakini tunataka mwenye uadilifu ili maamuzi yake yawe kwa manuafaa ya taifa.
 
Wassira atasubiri sana kwani hana sifa za kuwa Rais material,kwanza hata ktk jimbo lake hakubaliki na alipita kwa kumnunua mgombea wa cdm na kwa sasa pia analumbana na ESTHA BULAYA anayekuja kwa kasi jimboni humo.T.2015 ENL ndo suluhu ya JMT
 
Wassira ni muadilifu kwa viwango vya CCM huwezi mfananisha na EL. Ni kweli kabisa sifa kuu ya Raisi ajaye iwe uadilifu. Tukishindwa kupata raisi mwadilifu wa kweli tumekwisha.
 
Wassira atasubiri sana kwani hana sifa za kuwa Rais material,kwanza hata ktk jimbo lake hakubaliki na alipita kwa kumnunua mgombea wa cdm na kwa sasa pia analumbana na ESTHA BULAYA anayekuja kwa kasi jimboni humo.T.2015 ENL ndo suluhu ya JMT

Hatutaki kiongozi bubu kwenye masuala ya kitaifa kama Katiba na Escrow
 
Wassira atasubiri sana kwani hana sifa za kuwa Rais material,kwanza hata ktk jimbo lake hakubaliki na alipita kwa kumnunua mgombea wa cdm na kwa sasa pia analumbana na ESTHA BULAYA anayekuja kwa kasi jimboni humo.T.2015 ENL ndo suluhu ya JMT

jiandae kisaikolojia kwasababu wapinzani wanachukua nchi 2015
 
The next presedent is prof. Mwandyosa pm is dr. Pombe...hutaki kaa chini.
 
The next presedent is prof. Mwandyosa pm is dr. Pombe...hutaki kaa chini.

Ni mtizamo wako tunauheshimu kizuri naomba tuwapime wote kwa vigezo na historia za utendaji wao mimi kete yangu bado kwa Wasira sababu ninazo za kuhamini hivyo
 
Sawa Wasira inawezekana akawa kiongozi mzuri ila sio kwa wakati wa sasa.Wengi wataonekana wanafaa kwa sababu ya ubovu wa viongozi wengi wa sasa...bado tutafute nani anayetufaa.
 
Ndugu watanganyika wenzangu tujitahidi kila kona ya nchi tuchague wabunge mchanganyiko; kama ilivyo marekani tuwe na wabunge wengi kutoka upinzani kuisimamia vyema serikali. Kwa kuwa wengi wetu sio wanachama wa chama chochote, tuangalie uwezo bila kujali chama anachotoka. Kwa upande wa Rais tayari mtumishi mmoja wa Mungu Nabii ametabiri wapinzani kushinda kwa kishindo, anasema CCM imekuwa chukizo kubwa mbele za Mungu. Tumsifu Yesu Kristu.
 
Bwana rais
 

Attachments

  • 1418094654938.jpg
    1418094654938.jpg
    16.5 KB · Views: 71
Back
Top Bottom