Kete ya CCM urais 2015 naiona kwa Wasira

Kete ya CCM urais 2015 naiona kwa Wasira

Njaa Mbaya

JF-Expert Member
Joined
Jul 4, 2012
Posts
666
Reaction score
178
Ndugu wana bodi nimepitia utafiti wa twaweza na nimefanya survey kupata maoni ya wananchi wa kawaida sana juu ya nani anaweza kuibeba bendera ya CCM kuelekea ikulu 2015 nimeona wana mtu mmoja wa uhakika ni Wasira.

Edo kwa sasa ni ngumu mno kumuuza ukizingatia kidonda cha juzi cha escrow kimetibua kabisa na ya richmond.

Hivyo wananchi wengi wametibiliwa upya kabisa na ufisadi wa escrow na wameuunganisha na ule wa richmond ambao muhusika mkuu ni Edo.

Mkuu Kayanza nae alikuwa ameonekana kama angeweza kuibeba bendera lakini amepoteza matumaini kwa umma baada ya wananchi kuona hajui hata hela ya escrow ni ya nani. Hivyo ni heshima tu imembakiza kwenye UPM lakini wananchi hawana tena matumaini nae.

Mzee Sita yeye alijimaliza kwenye bunge la katiba hakuna tena mtanzania anafikilia tena hata yeye ameliona hilo.Mheshimiwa Membe ni mtu ambae kwa kweli amekosa kabisa mvuto na wananchi wengi hawampi kabisa nafasi ndani na nje ya CCM hivyo nafasi yake ya kubeba bendera ya chama kunako 2015 ni finyu mno.

Mwigulu ana hoja za wananchi maskini wa Tanzania ila watanzania wengi wanaona muda wake bado atakuwa kama JK 1995 dhidi ya Mzee Mkapa. J Makamba wengi wanamuona kama ni mtu mwenye ndoto ya uraisi lakinu watanzania wanamuona kama asiye na nafasi kwa aina ya rais anayehitajika kwa sasa.

Ngeleja na Pro. Tibaijuka wote tunajua wamechafuka hivyo siyo hitaji tena la watanzania. Sasa mtu ambae anaweza kubeba ajenda za chama na watanzania kwa ujumla ni comrade Wasira, ni mtu mwenye uwezo wa kujenga hoja, mwenye kuijua historia ya nchi na mahitaji ya wananchi kwa wakati huu, asiye na makundi wala mitandao na mwenye kukubalika ndani na nje ya chama.

Haya ni baadhi ya mengi niliyoweza kuyatafiti juu ya hawa ambao wameonyesha nia ukizingatia kuwa bado CCM ina nafasi kubwa ya kushinda na kuongoza dola 2015. Ni nafasi sasa ya kuwafuatilia hawa waonyesha nia ili kuwajua kwa undani ndipo mtakubali mtu asiye na kashfa ya ufisadi ni Wasira na ndiye kete pekee ya CCM 2015.
 
Umeandika mengi lakini mimi nikujibu kifupi: uraisi unahitaji personality na kuwa alert all the time. Unayemsema Hana personality hiyo na ana historia ya kulala mchana bungeni.
 
Umeandika mengi lakini mimi nikujibu kifupi: uraisi unahitaji personality na kuwa alert all the time. Unayemsema Hana personality hiyo na ana historia ya kulala mchana bungeni.

Hatumtafuti malaika kila binadamu ana kasoro, kikubwa ni uwezo na dhamiri ya dhati ya kulitumikia taifa. Sijawai kusikia dunia watu wanachagua kiongozi kwa personality labda ufafanue unamaanisha nini
 
Hoja sio kulala bungeni Wala kucheka bungeni au kulia bungeni Bali tuangalie uadirifu na uchapakazi pia mchango wa mtu katika kukijenga chama chake!!
 
Hatumtafuti malaika kila binadamu ana kasoro, kikubwa ni uwezo na dhamiri ya dhati ya kulitumikia taifa. Sijawai kusikia dunia watu wanachagua kiongozi kwa personality labda ufafanue unamaanisha nini

Jibu fupi ni angalia picha ya Nyerere halafu angalia ya Wasira utajua nina maana gani ninaposema personality. Pili tuwekee hapa jamvini kitu ambacho Wasira amefanya ambacho watanzania watamkumbuka. Je, kule bungeni alisimama na kusema wezi wa escrow washughulikiwe? Mimi sikumsikia! Tanzania haiwezi tena kuongozwa na watu waliotufikisha hapa tulipo sasa. Hospitali hakuna dawa lakini wanafikiria kujenga flyover na daraja la kwenda Zanzibar. They are morally bancrupt. Tunahitaji total makeover of the leadership na huyu unaemtaja doesn't qualify under any circumstances. Nimalizie-sina chuki binafsi ila haya ni mawazo yangu :confused2:
 
for sure wasira deserve much kwani mpaka sasa hakuna mgombea anaefit kwenye kiti hicho zaid yake lakin pia we unaesema analala bungen tofautisha kulala na kusinzia yy pia i binadamu and how many times umemuona akilala bungeni?? je tangu yupo bungeni yy ni kulala tu?? huwa hachangii hoja?? acheni kupaka matope watu hovyo lakin pia unaelewa maana ya personality nina hakika hujui lakin pia hakuna sifa ya upersonality kwenye urais coz unaweza kuwa na personality lakin jizi kama mzee wa richmond
 
Jibu fupi ni angalia picha ya Nyerere halafu angalia ya Wasira utajua nina maana gani ninaposema personality. Pili tuwekee hapa jamvini kitu ambacho Wasira amefanya ambacho watanzania watamkumbuka. Je, kule bungeni alisimama na kusema wezi wa escrow washughulikiwe? Mimi sikumsikia! Tanzania haiwezi tena kuongozwa na watu waliotufikisha hapa tulipo sasa. Hospitali hakuna dawa lakini wanafikiria kujenga flyover na daraja la kwenda Zanzibar. They are morally bancrupt. Tunahitaji total makeover of the leadership na huyu unaemtaja doesn't qualify under any circumstances. Nimalizie-sina chuki binafsi ila haya ni mawazo yangu :confused2:

Aliongea na kubwa alilosema ni kuwa hakuna chama cha wezi ila kuna wezi katika vyama na akasema serikali itatekeleza maazimio ya bunge sasa zaidi ya hapo ndugu yangu aseme nini
 
Yaani bora yeyote mwingine lakini sio huyu

Mimi nasema hivi CCM ina zaidi ya asilimia 90 ya kushinda urais 2015, ni vyema tukawafahamu wanaowania kiti hiki kiundani ili tufanye maamuzi sahihi. Kwa nchi ilipo leo uadilifu kwa rais ajae ni sifa mama ili kuwa na hakika kuwa rasilimali zetu zitatumika kwa manufaa ya wananchi. Hivyo tunapoanza kumchambua kiongozi sifa hii muhimu lazima ichunguzwe kwa umakini sana katika historia ya utendaji wa mgombea.
 
Jamani mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni. Hakuna mtu mwingine mwenye uthubutu wa kukemea maovu zaidi ya Lowasa. Kila mtu anafahamu alivyokua mchapa kazi akiwa waziri mkuu. Hii ya kujiuzulu uwaziri, hakujiuzulu kwakuwa kausika kuchukua pesa. Bali aliwajibika tuu kama waziri mkuu. Mchagueni airekebishe nchi hii ambayo kikundi cha watu wachache wanagawana rasilimali za nchi kama nchi ni ya kwao wenyewe. Tatizo kubwa ambalo tunalo wananchi ni kwamba tunakwenda kwa ushabik wa vyama. Tukitaka mafanikio ktk nchi hii, kwanza kabisa tuacheni ushabik wa kivyama. Zote tuungane tumchague mtu atakaetusaidia kuiondoa hii hali iliyoko kwa sasa hivi ambae sii mwingine ni EDWARD NDOYAA LOWASA. Mpeni kura zenu wote na hamjajutia.
 
Hatumtafuti malaika kila binadamu ana kasoro, kikubwa ni uwezo na dhamiri ya dhati ya kulitumikia taifa. Sijawai kusikia dunia watu wanachagua kiongozi kwa personality labda ufafanue unamaanisha nini

Mbona Kikwete mlimnadi kwa sura tu.
 
Aliongea na kubwa alilosema ni kuwa hakuna chama cha wezi ila kuna wezi katika vyama na akasema serikali itatekeleza maazimio ya bunge sasa zaidi ya hapo ndugu yangu aseme nini

Kwa hiyo maazimio yasipotekelezwa Wasira atolewe kwenye mbio za Urais! Kwa kweli system nzima ya kikwete inabidi itoke kabisa haifai kuwepo.Tunahitaji mageuzi
 
Nitafurahi tukipata Rais Kijana mwenye fikra mpya na mawazo mapya. January na Mwigulu nawaombea mmoja wao apate nafasi ya kutiongoza.
 
Back
Top Bottom