Pdidy
Platinum Member
- Nov 22, 2007
- 61,680
- 37,867
na Grace Macha, Moshi
MAKADA mbalimbali wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), akiwemo Mwenyekiti wao wilayani hapa, Godfrey Mwangamilo, jana walifurika kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Moshi wakati kada wa chama hicho, Ramadhani Mwidadi maarufu kama Gadafi, alipofikishwa mahakamani hapo kwa tuhuma za kukutwa na dawa za kulevya aina ya bangi. Akisoma shitaka hilo mbele ya Hakimu wa mahakama hiyo, Ruth Mkisi, Mwanasheria wa Serikali, Twide Mangula, alidai kuwa Gadafi na wenzake sita walitenda kosa hilo Januari 21 mwaka huu.
Mbali ya Gadafi, washitakiwa wengine ni Mwenyekiti wa Kata ya Pasua, Abdulkadri Abdalah, maarufu kama Tesha ambao wanatetewa na wakili, Godwin Sandi.
Mangula alidai, siku ya tukio washitakiwa kwa pamoja walikutwa katika Mtaa wa Benbela kwenye Manispaa ya Moshi na mabunda sita ya misokoto ya bangi.
Washitakiwa walikana shitaka na wako nje kwa dhamana hadi Februari 16, mwaka huu kesi hiyo itakapotajwa tena.
Washitakiwa wengine ni Shabani Athumani Hasani, Ibrahim Islam, maarufu kama Masawe, Vincent Malasi, Hamisi Mtengeti na Amani Ngido.
MAKADA mbalimbali wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), akiwemo Mwenyekiti wao wilayani hapa, Godfrey Mwangamilo, jana walifurika kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Moshi wakati kada wa chama hicho, Ramadhani Mwidadi maarufu kama Gadafi, alipofikishwa mahakamani hapo kwa tuhuma za kukutwa na dawa za kulevya aina ya bangi. Akisoma shitaka hilo mbele ya Hakimu wa mahakama hiyo, Ruth Mkisi, Mwanasheria wa Serikali, Twide Mangula, alidai kuwa Gadafi na wenzake sita walitenda kosa hilo Januari 21 mwaka huu.
Mbali ya Gadafi, washitakiwa wengine ni Mwenyekiti wa Kata ya Pasua, Abdulkadri Abdalah, maarufu kama Tesha ambao wanatetewa na wakili, Godwin Sandi.
Mangula alidai, siku ya tukio washitakiwa kwa pamoja walikutwa katika Mtaa wa Benbela kwenye Manispaa ya Moshi na mabunda sita ya misokoto ya bangi.
Washitakiwa walikana shitaka na wako nje kwa dhamana hadi Februari 16, mwaka huu kesi hiyo itakapotajwa tena.
Washitakiwa wengine ni Shabani Athumani Hasani, Ibrahim Islam, maarufu kama Masawe, Vincent Malasi, Hamisi Mtengeti na Amani Ngido.