1800
JF-Expert Member
- Dec 27, 2010
- 2,215
- 603
Wadau mwenye taarifa naomba kujuzwa hii kesi ya hawa waliokua watumishi wa wilaya ya Rombo ambao bila aibu walitafuna jumla ya 914m/= na baadae kutafuna tena 29.4m/=. Nimependa kujuzwa hivyo kwa kua kuna habari zilizo chini ya carpet kua mafisadi hawa wamehonga hela nyingi ili kesi hiyo iweze kuishia hewani,na isitoshe sijasikia tena habari juu ya kesi hii,tunataka kuona haki inatendeka,sio hela za Watanzania ziwe zinatafunwa kila siku na wajanja wachache,kwa kua kesi hii wengine ushahidi tunao,kwa kua wengne walikua ni watu wa kawaida ktk utumishi ila kwa sasa wanamiliki mijumba na hoteli za kifahari katika mikoa ya Arusha,Moshi,Dar na Morogoro,tunaomba sheria isimamie ili liwe funzo kwa mafisadi wadogo na wakubwa