Leo nimebahatika kuhudhuria kesi ya Nsanzugwanko dhidi mh. Zaituni Agripina buyogera mbunge wa kasulu vijijini.kumbuka leo mh. Zaituni ndipo alikuwa anatoa ushahidi wake dhidi ya tuhuma zilizotolewa na nsanzugwanko kuwa alimtuukana kuwa ni mchawi,alimuua marehemu teddy magayane na bernad machupa aliyekuwa mgombea udiwani wa mwali,ccm ni chama cha mafisadi. Kesi inasikilizwa na jaji aruna muroso(kama sijakosea jina) na mawakili wa serikali ni advo rweyongeza, Advo
ndamgoba(kama sijakosea jina) na advocate rweyemamu anayemwakilisha mh zaituni buyogera. Ndugu Nsanzugwanko anawakilishwa na advocate musa. kesi ilianza kwa mh. Zaituni kuongozwa na wakili wake Advo
rweye
.Uliwai kutolea kashfa Nsanzu kama alivyoeleza kwenye mashtaka yake?? Mh. Zai
.sijawai.Mashitaka haya ni kwa kuwa nilimshinda kwenye uchaguzi. Advo rweye ..Je unamfahamu nsanzugwanko? Mh. Zai..ndiyo..ninamfahamu.alikuwa mgombea ubunge nccr mwaka 2000.alikuwa boss wangu nccr na alinisfundisha siasa.mwaka 2002 alihamia ccm.mwaka 2005 niligombea nae ila mimi kura hazikutosha Advo rweyi
unamfahamu benard machupa?? Mh. Zai
..namfamu alikuwa mgombea udiwani wa kata nyachenda/mwali.alifariki tarehe 9/10/2010 na ilibidi tusimamishe kampeini kwa siku tatu. Advo rweyi
.Ulimtuhumu nsanzu kumuua Bernard machupa tarehe 7/10/10 unasemaje? Mh. Zai..si kweli haya ni majungu.nitasemaje kuwa bernad aliuawa na nsanzu tarehe 7/10 wakti alifariki tarehe 9/10?haya ni majungu Advo zai
.ulitoa tuhuma za wizi na mauaji wakti huko zeze.tuhuma hizi unazisemaje? Mh. Zai
si kweli.kata hii sisi ndiyo tulikuwa na diwani.mimi niliongelea zahanati ikizingatiwa kata hii ilikuwa na majengo pasipo mganga.watu wa eneo hili walikuwa wanaenda jimbo la kigoma kusini kijiji cha nyanganga. Advo rweyi..sera zako zilikuwa zipi? Mh zai
.nilitumia irani ya nccr na vipaumbel vyangu ilikuwa ardhi,elimu,afya,barabara na kilimo Advo rweyi
mwisho kabisa unamwambia nini jaji? Mh zai
naomba mahakama initangaze mimi ndiye mbunge,pili alipe gharama za kesi hii Advo rweyi
Unaujua ugomvi wa nsanzu na mwenyekiti ndaheza? Mh. Zai
sijui. Baada ya muongozo huo advo rweyongeza alitaka kufahamu kama aliwai lalamikiwa sehemu yoyote hile na mh. Zai alikanusha kabisa. Jaji alimruhusu advo musa aanze kuuliza maswali nayo yalukuwa kama ifuatavyo Advo musa
..Elimu yako? Mh. Zai
nilimaliza std 7 mwaka 1983 Advo musa
..mtoto wa kwanza ilimzaa mwaka gain? Mh. Zai
.nilimzaa mwaka 1985 Advo musa
..taja majina yako Mh. Zai
naitwa Zaituni agripina buyogera Advo musa
..Jina la baba yako? Mh. Zai
anaitwa athuman buyogera Advo musa
.nyumbani kwenu kuna zaituni wangapi? Mh..zai
tuko wengi kwani hakina zaituni Advo musa..kwanini uitwe zaituni..ubini wa baba yako haupo? Mh jaji ameingilia kati. Wewe usiingilie mambo ya familia ohh ana wake wangapi baba,kwanini mnaitwa zaituni agripina.malalamiko haya ungepeleka kwa wale wa uzazi na vifo ili watupe maelezo ya majina haya.tunataka ushahidi siyo kupoteza muda. Advo musa anakubali ngoma inaendelea. Advo musa
Unajua kiingereza? Mh. Zai
mimi sijui kiingereza najua Kiswahili Advo musa
kwanini ulikuwa unaenda na vitabu hasa kijani kwenye kampeini? Mh..zai
nilikuwa naenda na kitabu cha buruu ambacho ni irani ya nccr na kingine ilikuwa ratiba ya mkutano. Advo musa
sera zako ulizitoa wapi?? Mh. Zai
nilizitoa kwenye irani ya nccr Advo musa
tusomee mahali zilipo Mh. Zai..sisomi ila zimo humu Jaji ameingilia kati kwa kumwambia advo musa,hatutaki kusoma kitabu hapa.chama kinaweza kuwa na sera 30 lakini huyu alitoa zinazomfaa.awezi kueleza sera ya bahari wakati kasulu hakuna bahari. Advo musa endelea Advo musa. Kabla ya kufunga kampeini.siku moja kabla kule rungwe mlifanya maandalizi nccr.je ni maandalizi gain? Mh. Zai
mimi sijui ya 29/10 najua mkutano wa 30/10.ukienda mkutanoni unakuta watu wameishaitwa . Advo.musa
kuna umbali gain toka nyumbani kwako hadi ofisi ya ccm Mh. Zai
sijui labda km au mita??/sijui. Labda kama hapa na kituo cha polisi. Jaji anaingilia kati kujua umbali naanawauliza maaskari umbali nao wanasema ni kama 0.5 hadi km 1. Baada ya kumaliza naye jaji aliuliza maswali yafuatayo Jaji
.unaishi kijiji gain? Mh..zai
ninaishi kijiji kumsenga Jaji
umeishajenga kwenye jimbo lako? Mh..zai
bado..mimi niko jimbo la kaslu mjini Jaji
ulikuwa unaudhuria mikutano ya hapa mjini?? Mh.. zai
hapana.nilkuwa natoka vijijini muda umeenda. Mwisho jaji amemshukuru kwa ushahidi wake uliochukua masaa 4 NILIYOYAONA Nsanzu halalamikii tofauti ya kura alizozidiwa kama elfu 7 hivi bali ameleta kashfa Jaji ni mzuri kwa kusikiliza na kutoa ushauri hasa mawakili wakimbana zaidi shahidi. Kesi hizi ni zakuteketeza kodi za walala hoi wa Tanzania basi Kesi bado inaendele na mashahidi bado wanaendelea wa upande wa utetezi Nawasilisha