Kesi ya Lwakatare hatarini kufutwa tena

Kesi ya Lwakatare hatarini kufutwa tena

ccm msishindane na mungu mungu yeye anaona waja wake tunavyopata shida, njaa, shida ya maji , elimu chafu. mungu huyu aliye hai hawezi kukubali udhalimu kma huu. kwa hakika tutashinda
 
Nilisema.DPP na Polisi wanatoboana macho sasa. Kazi inaendelea!
 
Kazi kweli,kila anaetokeza kwasasa ni kamata,bambika kesi yoyote ile iwe ya kigaidi,utekaji nk,mwisho kitaeleweka tu,ndugu msiwe na hofu..uhuru unakuja.
 
Hivi Hawa TCRA walisajili namba za simu ili iweje?mbona wanakuwa washenzi sana?inatia hasira sana
.Yani MaCCM sijui yamerogwa?na Prezidaa hivi karogwa au Kuna nini?
 
Tutasikia mengi.Mwisho wa siku watasema CHADEMA.Kuna siku hata shetani atawaruka kuwa hajawatuma kutenda dhambi hiyo.Aliwashawaishi tu ila kosa umelitenda mwenyewe..............
 
Wameshaumbuka Mkuu sasa wako busy katika juhudi zao muflisi za kuipanga upya movie yao ambayo watazamaji wameishaistukia. Mara kesi imefutwa mara imefunguliwa tena!!!, Usanii mtupu!!!! Vyombo vyote vya dola (polisi, jeshi na mahakama) vimekuwa ni vitengo vya magamba havina credibility hata chembe!!!
subiri mkuu haraka ya nn? Tuache kuweweseka
 
Hivi Mbowe hana tena controll na gazeti la Tanzania Daima? Maana naona linazidi kuipaka matope kebineti ya Kinondoni kwa umbeya wao kila asubuhi.
 
Chanzo : Tanzania Daima,

Usitegemee kupata taarifa isiyokuwa na muelekeo fulani
 
Chama dhaifu kimetupatia serikali dhaifu inayoongozwa na Rais dhaifu mwenye udhaifu wa fikra na dira. Kufutwa na kufunguliwa kesi ileile ni dalili tosha ya serikali dhaifu yenye watendaji dhaifu chini ya Rais wao dhaifu inayoshindwa hata kutoa ufumbuzi kwa suala la kitoto kama kuchinja kitoweo.
 
Wanaoweweseka ni hao wanaotaka kutiana vidole machoni kwamba ushahidi haujatimia na kuendeleza usanii wa kutaka kutafuta ushahidi ambao haupo ili kufungua kesi ya ugaidi, mara kesi ifutwe mara ifunguliwe tena!!!. Magaidi wa kweli wameshajulikana.

subiri mkuu haraka ya nn? Tuache kuweweseka
 
Hawana jipya Mkuu, ahadi zao za tangu 2005 hawana hata moja waliyotimiza sasa wanaona 2015 inazidi kukaribia na sera zao ni usanii mtupu hivyo wameamua kuja na sera moja tu ya kupandikiza ushahidi dhidi ya Viongozi wa CHADEMA ili kuwachafua na hivyo kukichafua CHADEMA. Kumbuka hata Dr Slaa wakati akihudhuria kikao cha Bunge kule Dodoma miaka michache iliyopita walimtegeshea chumbani kwake vinasa sauti. Polisi magamba wakadai wanachunguza lakini hadi hii leo hakuna ripoti ya polisi kuhusu mhusika wa vinasa sauti vile.

Kinachoonekana hapa ni dhahiri kuwa kuna msukumo wa kisiasa kulazimisha Lwakatare ashitakiwe kwa makosa ya ugaidi wakati ushahidi uliopo ni mdogo sana kushadia makosa ya ugaidi.

Inaonekana DPP hajaridhika na ushahidi uliopo na polisi wanafanya kila wawezalo kutafuta na kutengeneza ushahidi wa kumshawishi DPP.

Lakini kwa hali inavyoendelea tutarajie lolote kutoka kwa DPP, jeshi la polisi au mahakama kuu manake hapa kuna nguvu kubwa sana ya kisiasa inayoizunguka kesi hii kuliko uhalisia na sheria yenyewe.
 
Asante sana BAK kwa taarifa ila wajue kuwa penye ukweli uongo hujitenga. Mwisho wa siku serikali itashindwa na sijuia itawaambia nini watanzania kodi zao zinapotelea katika kesi za kutunga kisa kuwaogopa CDM. Kama wangekuwa na sera nzuri na utekelezaji mzuri wasingetumia nguvu kubwa mno kuzima upinzani. Shame on them.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Back
Top Bottom