Kesi ya EPA... washtakiwa hawana kesi !!

Mag3

Platinum Member
May 31, 2008
13,064
22,757
UPANDE wa utetezi katika kesi ya wizi wa Sh1.8 bilioni kwenye Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA) inayomkabili Rajabu Maranda na ndugu yake, Farijala Hussein, umedai kuwa washtakiwa hao hawana kesi ya kujibu kwa sababu hakuna mtu yeyote aliyetoka (BoT) na kusema kuwa benki hiyo iliibiwa.
"Mahakama inatakiwa kutoa maamuzi kwa kuzingatia ushahidi na si kufanya kazi kwa hisia kwa sababu inaweza ikajiweka katika wakati mgumu kusema washitakiwa wana kesi ya kujibu wakati BoT haijaja kulalamika kama imeibiwa,"
alidai Magafu.
"Anayestahili kulalamika ni BoT kwa sababu wao ndio waliopewa dhamana ya kutunza fedha hizo na ndio walikuwa wamiliki wa akaunti ya EPA," alidai.
"BoT ina viongozi mbalimbali wakiwemo gavana, manaibu wake, mkurugenzi wa fedha, mkurugenzi wa sera na uchumi, mkurugenzi wa utawala na utumishi na wakuu wa vitengo tofauti, lakini hakuna kati yao aliyefika mahakamani kutoa ushahidi kwamba benki hiyo iliibiwa" alimalizia.

Swali - kwanza, mwizi ni nani, mlalamikaji ni nani na anayeshitakiwa ni nani kwa kumwibia nani. My take - Usanii wa serikali at its best. Wanasheria wa JF, mnasemaje.
 
Huo ndiyo kweli yenyewe. Washitakiwa wakitumia competent lawyers, serikali chali. Kwa sababu hata yule internal aditor wa benki (shahidi) alikiri kwa malipo yalikuwa halali!!! Kazi ipo hapo. BOT ndiyo inatakiwa kushtakiwa, ieleze kuwa fedha hizo ziliyeyukaje??? Kwa taratibu za hela transaction kubwa ni lazima ziwe verified, sasa je BOT walifanya hivyo???

Ningekuwa mimi ni Magafu, ningeandaa utetezi ambao ni kiboko, hata hapo alitaja simple sana, kuwa eti BOT hawajalalamika kuwa waliibiwa. Hautoshi, kuna evidence hyingi kuwa washtakiwa wakisimamia watatoka, then waanza kudai fidia. Siasa bwana, ni kichekesho.
 
Mlalamikaji sio lazima awe BOT ila ni Serikali kwa kuwa hata BOT ni ya serikali. Kwa hiyo tuseme kama hela imeibiwa BOT na hakuna aliyelalamika pale BOT tuseme huo sio wizi? This is a ridiculous argument by the Defence Council and mind you, it is doomed to be overuled by the court.
 
Mlalamikaji sio lazima awe BOT ila ni Serikali kwa kuwa hata BOT ni ya serikali. Kwa hiyo tuseme kama hela imeibiwa BOT na hakuna aliyelalamika pale BOT tuseme huo sio wizi? This is a ridiculous argument by the Defence Council and mind you, it is doomed to be overuled by the court.

Sasa kwa kuwa BOT haikuvunjwa, pesa zikaibiwa na wezi wakakamatwa, kama mlalamikaji ni serikali, mshtakiwa alitakiwa awe nani. Nakumbuka tamko la serikali la awali kuwa hizo pesa hazikuwa na mwenyewe, sasa aliyeibiwa ni nani.

Au tuchukue mfano wa kawaida tu - unanitunzia mali yangu halafu anakuja mtu na kwa kutumia nyaraka feki anakushawishi na wewe kwa hiari yako mwenyewe unampa hiyo mali. Hapa mlalamikaji anatakiwa awe nani na mlalamikiwa awe nani.
 
Kosa lolote la jinai huwa ni dhidi ya Serikali/Jamhuri na Serikali/Jamhuri huwa ndio mlalamikaji, ndio maana kwenye hukumu huwa wanaandika: 'Republic versus AB' hata kama aliyeibiwa ni mtu binafsi. Kwenye kesi hii technicallities zitasaidia kupunguza kasi ya kesi lakini sio matokeo endapo ushahidi uko wazi.
 
Kama nakumbuka vizuri Serikali ilisema kuwa fedha fedha za EPA sio zake ila ni za watu binafsi na zitatumiwa na Serikali. Endapo kama wenyewe wangezihitaji basi Serikali ingeangalia namna ya kurefund. Kama hazina mwenyewe ziliendaje BOT? Hata kama hazingekuwa na wenyewe ndio iwe tiketi ya kuunda makampuni hewa na kwenda kuzikwapua? Oh, Please, open your mind!
 
Back
Top Bottom