Kesi namba 458 inayomkabili Mkurugenzi wa Jamii Media, Maxence Melo kutajwa leo

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
3,962
13,736
Habari wanaJF,

Leo katika Mahakama ya Kisutu inakuja kwa kutajwa(mention) kesi ya Jamhuri dhidi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Jamii Media, Ndg. Maxence Melo ambayo ni kesi namba 458 ya Mwaka 2016 iliyochini ya Hakimu Mkazi, Victoria Nongwa.

Katika kesi hii, Maxence anashtakiwa kwa makosa mawili:

1) Kuendesha mtandao ambayo nchini, yaani .tz (Tanzania domain).

2) Kushindwa 'kutoa ushirikiano' kwa Jeshi la Polisi kwa kuzuia taarifa binafsi za wateja wa mtandao wake.

Aidha mpaka siku ya leo ni siku ya 60 tangu kesi hii imeanza na kwa mara ya mwisho upande wa Jamhuri ulidai Upelelezi ulikuwa bado unaendelea.

978a77c4-a2f9-4646-9e4e-7972cfc645c9.jpg

========
UPDATES

Kesi namba 458 inayomkabili Mkurugenzi Mtendaji wa Jamii Media, Maxence Melo yaahirishwa hadi Machi 9, 2017. Hakimu Mkazi Victoria Nongwa anayesimamia kesi hiyo hakuwepo.

Kuna uwezekana kesi hii ikaunganishwa na nyingine yenye mashtaka yanayofanana na zote zikawa zinaendeshwa kwa siku moja.
 
Wangehangaika katika kutengeneza ajira kuliko kudeal na kesi ambazo hazina maana kabisa ni kuchezea kodi zetu bure.
Kila la kheri Maxence Melo pamoja na uongozi wa Jamii Forum naamini Mungu yupo upande wenu mtashinda vita hii kandamizi dhidi ya serikali.
 
KUTOKA KISUTU, DAR: Kesi inayomkabili Mkurugenzi wa Jamii Media, Maxence Melo yaahirishwa hadi Machi 9 kutokana na Hakimu Mkazi, Victoria Nongwa kutokuwepo.
 
Back
Top Bottom