Kesi madai ya fedha mahakamani inahitaji dhamana?

Kig

JF-Expert Member
Aug 13, 2012
1,076
456
Habari zenu watalaamu na wadau wa sheria. Naomba kujua kama mtu akifikishwa mahakamani kwa kudaiwa fedha ya mkopo na mtu binafsi, atatakiwa kuandaa wadhamini wa kumdhamini akiwa mahakamani?
 
Kwakua haina kifungo automatically, huna haja ya mdhamini.
Kesi za jinai ndio huhitaji hilo maana kuna element ya kufungwa jela iwapo utapatikana na hatia.
 
kesi zinahusu fedha kama mtu yupo mahabusu anatakiwa atoe nusu ya kile anachodaiwa kama dhamana...
 
Kesi ya madai hata kufungwaa hufungwiii labda udaiwee na serikalii
Jidanganye hivyo, jaribu kuyakanyaga kwa mtu ambaye ataamua kukukomalia uone kama hujaenda jela, gharama zote za kukutunza huko anakulipia uone!! Kama juhakaa jela, hadi ulipe pesa zake.
 
Jidanganye hivyo, jaribu kuyakanyaga kwa mtu ambaye ataamua kukukomalia uone kama hujaenda jela, gharama zote za kukutunza huko anakulipia uone!! Kama juhakaa jela, hadi ulipe pesa zake.
Sasa mtu unalipaa pesa ili mtu afungweee na bado unzidi kumuhudumia ni Utahiraaa au wehuu???
 
Sasa mtu unalipaa pesa ili mtu afungweee na bado unzidi kumuhudumia ni Utahiraaa au wehuu???
Ukilitazama kwa upeo wako, utaona hivyo ila kwa tuliotumia njia hiyo ilitusaidia kupata pesa zetu zote!! Hiyo unaifanya ki mkakati sio ili mradi tu!! Na hata huyo mdaiwa mwanzoni ataona masihara ila inapofikia hatua hiyo anaona unakabidhiwa uende naye magereza, mwenyewe, ndio sasa anajua kumbe nimekwisha!! Nilimdai pesa zaidi ya miaka mitano, kesi iko mahamani tu, kila siku chenga, ila ilipotoka hukumu nikamlipia segerea gharama za kumtunza za miezi miwili, mbona baada ya mwezi tu walinitafuta na kunilipa pesa zangu zote!!!
 
Ukilitazama kwa upeo wako, utaona hivyo ila kwa tuliotumia njia hiyo ilitusaidia kupata pesa zetu zote!! Hiyo unaifanya ki mkakati sio ili mradi tu!! Na hata huyo mdaiwa mwanzoni ataona masihara ila inapofikia hatua hiyo anaona unakabidhiwa uende naye magereza, mwenyewe, ndio sasa anajua kumbe nimekwisha!! Nilimdai pesa zaidi ya miaka mitano, kesi iko mahamani tu, kila siku chenga, ila ilipotoka hukumu nikamlipia segerea gharama za kumtunza za miezi miwili, mbona baada ya mwezi tu walinitafuta na kunilipa pesa zangu zote!!!
hahahaaaa...............
 
hahahaaaa...............
Eti mdaiwa hafungwi!!!wewe mbona niliipata pesa yangu yote, watoto wake wanauwezo mkubwa , ila waliona ni upuuzi!!na mimi nilijua tu ngoja mzee awekwe ndani watajitokeza tu!!na kweli ndio kilichotokea!!
 
Back
Top Bottom