Faana
JF-Expert Member
- Dec 12, 2011
- 31,831
- 33,219
Napenda kuuandikia uongozi wa Kampuni ya Abood Bus Service juu ya kero kadhaa, kwanza niseme wazi kuwa lalamiko hili halijalenga kuichafua kampuni bali kuijenga kwakuwa mimi ni regular traveler kwa kutumia kampuni hiyo, vilevile sijalenga kumharibia kazi mtu yeyote ila nahimiza kutazama mambo ya msingi katika utendaji kazi na kustawisha utaifa wetu.
Nilisafiri na bus namba T868 DJP siku ya Jumapili tarehe 25.4.2021, kutoka Dsm kwenda Morogoro, safari ilianza Ubungo majira ya saa 6:33 mchana na ilikuwa njema, dereva alikwenda mwendo mzuri kabisa ambao hakuna abiria aliyeulalamikia , intertainment kwenye screen zilikuwa kwa sauti ya kawaida ambayo haikuwa na kero kwa wasafiri.
Lalamiko langu linakuja ilipofika majira ya saa 10:41 - 10:44 jioni tukiwa eneo la Kingolwira ulichezwa muziki mmoja ambao sikufanikiwa kusoma jina unaitwaije, lakini muziki ule ulimalizikia kwa maandishi UNIVERSAL (nasikitika sikuweza kurekodi video husika), muziki ule kiukweli haukuzingatia kabisa maadaili ya utanzania wetu kwa maana ya kwamba wachezaji wake walikuwa uchi kabisa na wengi wa wachezaji wale walikuwa ni wanawake ambao chuchu zao zilionekana wazi na hata sehemu za siri zilionekana wazi, kwa wanaoujua muziki huo wanaweza kutusaidia kwakuwa wachezaji hao walionekana kwenye matope wakati fulani.
Binafsi nadhani ifike mahali Mheshimiwa Abdulaziz Abood ambaye ni mmiliki wa kampuni ya Abood, uwe makini na madereva wako na hasa linapofika suala la burudani kwenye mabasi, madereva wale si wote wenye kuheshimu utu, ni kama wanaona wasafiri wote ni wahuni wapenda ngono, na tafsiri yake ni kwamba kampuni yako inamtazamo wa kuendekeza sana masuala hayo, binafsi nakufahamu Mh. Abood kuwa ni Muislamu safi usiyeshabikia mambo ya kihuni kihuni, najiuliza maswali kadhaa,
Wanaosafiri kwenye mabasi yale ni watu wa aina mchanganyiko na wenye heshima zao, wasichukuliwe poa, wapo watoto, vijana, wazee wa aina zote wa kiume na wakike, waislamu, wakristo na hata wasio na dini, utamaduni wetu wa kitanzania haujatufikisha hapo kwenye kutazama picha za namna ile kwenye public, abiria wengi tulikwazika na jambo lile, inawezekana dereva hakujua kwakuwa yeye mwenyewe hakuwa mtazamaji wa kinachoendelea kwenye screen, upo uwezekano wanaojaza hizo burudani kwenye flash ni vijana wenye mtazamo huo wa kingonongono na hivyo dereva kujikuta anatumbukia kwenye mtego pasipokujijua, na kama anajua basi ana matatizo kichwani.
Itoshe kusema kwamba Mh. Abood, tunaupenda sana usafiri wako, ni usafiri mzuri, mabasi yanasafishwa vizuri, mwendo mzuri, lakini kuna jambo la kulitazama kwa jicho la karibu, ikikupendeza tunaomba:-
Nilisafiri na bus namba T868 DJP siku ya Jumapili tarehe 25.4.2021, kutoka Dsm kwenda Morogoro, safari ilianza Ubungo majira ya saa 6:33 mchana na ilikuwa njema, dereva alikwenda mwendo mzuri kabisa ambao hakuna abiria aliyeulalamikia , intertainment kwenye screen zilikuwa kwa sauti ya kawaida ambayo haikuwa na kero kwa wasafiri.
Lalamiko langu linakuja ilipofika majira ya saa 10:41 - 10:44 jioni tukiwa eneo la Kingolwira ulichezwa muziki mmoja ambao sikufanikiwa kusoma jina unaitwaije, lakini muziki ule ulimalizikia kwa maandishi UNIVERSAL (nasikitika sikuweza kurekodi video husika), muziki ule kiukweli haukuzingatia kabisa maadaili ya utanzania wetu kwa maana ya kwamba wachezaji wake walikuwa uchi kabisa na wengi wa wachezaji wale walikuwa ni wanawake ambao chuchu zao zilionekana wazi na hata sehemu za siri zilionekana wazi, kwa wanaoujua muziki huo wanaweza kutusaidia kwakuwa wachezaji hao walionekana kwenye matope wakati fulani.
Binafsi nadhani ifike mahali Mheshimiwa Abdulaziz Abood ambaye ni mmiliki wa kampuni ya Abood, uwe makini na madereva wako na hasa linapofika suala la burudani kwenye mabasi, madereva wale si wote wenye kuheshimu utu, ni kama wanaona wasafiri wote ni wahuni wapenda ngono, na tafsiri yake ni kwamba kampuni yako inamtazamo wa kuendekeza sana masuala hayo, binafsi nakufahamu Mh. Abood kuwa ni Muislamu safi usiyeshabikia mambo ya kihuni kihuni, najiuliza maswali kadhaa,
- Je, nini kinawafanya madereva kupenda sana kuweka video za nusu uchi na uchi kamili kwenye eneo ambalo watu wanasafiri na wake zao, wakwe zao, binti zao, mama zao, baba zao?
- Je, entertainment ya mtanzania wa leo ni mambo ya uchi tu?
- Hakuna mambo ya msingi yanayoweza kuonyeshwa kwenye public ili kulinda heshima za wasafiri na kampuni?
- Hao madereva hawapewi mafunzo?
- Ni nani aliyewaambia kuwa wasafiri wa Abood ni wapenda picha za ngono?
- Kama wapo wanaotaka picha hizo si wakazitazamie kwao badala ya kwenye bus?
- Kwanini madereva wanashindwa kuheshimu watu wengine?
Wanaosafiri kwenye mabasi yale ni watu wa aina mchanganyiko na wenye heshima zao, wasichukuliwe poa, wapo watoto, vijana, wazee wa aina zote wa kiume na wakike, waislamu, wakristo na hata wasio na dini, utamaduni wetu wa kitanzania haujatufikisha hapo kwenye kutazama picha za namna ile kwenye public, abiria wengi tulikwazika na jambo lile, inawezekana dereva hakujua kwakuwa yeye mwenyewe hakuwa mtazamaji wa kinachoendelea kwenye screen, upo uwezekano wanaojaza hizo burudani kwenye flash ni vijana wenye mtazamo huo wa kingonongono na hivyo dereva kujikuta anatumbukia kwenye mtego pasipokujijua, na kama anajua basi ana matatizo kichwani.
Itoshe kusema kwamba Mh. Abood, tunaupenda sana usafiri wako, ni usafiri mzuri, mabasi yanasafishwa vizuri, mwendo mzuri, lakini kuna jambo la kulitazama kwa jicho la karibu, ikikupendeza tunaomba:-
- Madereva watambue kuwa wanaosafiri kwenye mabasi yale siyo vijana wa kizazi kipya tu, wapo rika zote,
- ikikupendeza Mh. Abood weka timu itakayo screen flash zote zinazochezwa kwenye mabasi zisiwe hizo za nusu uchi na uchi kamili, na siyo kweli kwamba wote wanapenda mambo yale, ila ni kwamba watu wanakosa sehemu ya kupitishia malalamiko yao (suggestion box)
- Pamoja na miziki, burudani zipo nyingi, kuna michezo mbalimbali kama mipira, mbio za magari, mashindano ya pikipiki, vipindi elimishi kama kilimo, ufugaji, utalii, mafundisho ya dini (huu ni mwezi mtukufu wa Ramadhani) na program nyingine nyingi zenye kumfurahisha kila mmoja na siyo picha za uchi, mambo ya hivyo yasubiri muda na mahali pake na si kwenye public services.