Kazanazo
JF-Expert Member
- Aug 16, 2023
- 7,074
- 11,270
Mteja ni mfalme,,,
Tumesemwa sana watoa huduma kuwa tuna lugha chafu, tunachezea simu muda wa kutoa huduma, muda wote hatuna change na mambo kibao. Sasa ngoja tuone upande wa pili wa wateja ukoje?
Aisee wateja wa bongo ni wasumbufu sana kuwahudumia inatakiwa usiwe na bandama wala nyongo ili hata akikushika mata** usikasirike la si hivyo utamtimua asirudi tena
Kwanza wengi hawajui kusoma wala kuandika, anaweza akakataa kitu wakati maandishi yanaonesha mfano umuuzie vocha ukamuingizia akakatwa na message katumiwa na deni lililobaki linaonesha na bado atakwambia hujamtumia na atajaza nzi wengi sana
Huwa hawafuatilii vitu vidogo vidogo wakawa na elimu navyo hata kwa uchache, utakuta mteja anamlalamikia wakala kamkata ela nyingi(makato ya kawaida sio lipa) wakati makato huwa hakati wakala bali kuna chati za miamala zinaonesha makato na hata umuoneshe hataki kuelewa
Mteja anakupa elfu 10 anataka kitu cha jero waenda hangaika change ukirudi ukimrudishia anatoa rundo la pesa za change anachanganya na ulizompa anaweka kwenye waleti au kipochi(dadeq) sasa unajiuliza huyu ni kopela au nini? Na hii inafanya siku nyingine hata hana kweli unamwambia tu sina change
Dah! Wateja huwa wana lugha za kukatisha tamaa sana, unakuta unauza duka limejaa mavitu ila kitendo cha kuuliza vocha ukamwambia sina aisee atafoka na kutukana na kukwambia "funga basi sasa hapo unafanya kazi gani maana kila kitu wewe huna"
Zipo nyingi sana izo ni chache tu
Ombi: ni kweli wateja wetu nyie ni wafalme lakini ufalme wenu unatokana kuwa na wahudumu hebu jaribuni kutuhurumia watoa huduma nasisi ni binadamu kama nyie tuna nyongo na bandama na mambo mengine tuhurumiane mtupe hela zenu nasisi tuwape huduma au bidhaa ni hayo tu
Tumesemwa sana watoa huduma kuwa tuna lugha chafu, tunachezea simu muda wa kutoa huduma, muda wote hatuna change na mambo kibao. Sasa ngoja tuone upande wa pili wa wateja ukoje?
Aisee wateja wa bongo ni wasumbufu sana kuwahudumia inatakiwa usiwe na bandama wala nyongo ili hata akikushika mata** usikasirike la si hivyo utamtimua asirudi tena
Kwanza wengi hawajui kusoma wala kuandika, anaweza akakataa kitu wakati maandishi yanaonesha mfano umuuzie vocha ukamuingizia akakatwa na message katumiwa na deni lililobaki linaonesha na bado atakwambia hujamtumia na atajaza nzi wengi sana
Huwa hawafuatilii vitu vidogo vidogo wakawa na elimu navyo hata kwa uchache, utakuta mteja anamlalamikia wakala kamkata ela nyingi(makato ya kawaida sio lipa) wakati makato huwa hakati wakala bali kuna chati za miamala zinaonesha makato na hata umuoneshe hataki kuelewa
Mteja anakupa elfu 10 anataka kitu cha jero waenda hangaika change ukirudi ukimrudishia anatoa rundo la pesa za change anachanganya na ulizompa anaweka kwenye waleti au kipochi(dadeq) sasa unajiuliza huyu ni kopela au nini? Na hii inafanya siku nyingine hata hana kweli unamwambia tu sina change
Dah! Wateja huwa wana lugha za kukatisha tamaa sana, unakuta unauza duka limejaa mavitu ila kitendo cha kuuliza vocha ukamwambia sina aisee atafoka na kutukana na kukwambia "funga basi sasa hapo unafanya kazi gani maana kila kitu wewe huna"
Zipo nyingi sana izo ni chache tu
Ombi: ni kweli wateja wetu nyie ni wafalme lakini ufalme wenu unatokana kuwa na wahudumu hebu jaribuni kutuhurumia watoa huduma nasisi ni binadamu kama nyie tuna nyongo na bandama na mambo mengine tuhurumiane mtupe hela zenu nasisi tuwape huduma au bidhaa ni hayo tu