Kero za wapiga debe stand za mabasi/daladala

Kero za wapiga debe stand za mabasi/daladala

Ulimbo

JF-Expert Member
Joined
Aug 14, 2009
Posts
3,766
Reaction score
4,046
Kuna watu wanajiita wapiga debe kwenye vituo vya mabasi.
1: Watu hawa wamekuwa kero sana kwa wasafiri, kwani wamekuwa wakikubaliana bei na wasafiri, na baada ya msafiri kuingia kwenye gari, wao wanabaki pale baada ya kupewa kiwango fulani cha fedha

Unafika maali unatoa nauli mliyokubaliana, Konda anakuambia hamjakubaliana hivyo. Ukimwambia ulikubaliana na aliyekuwa anapiga debe anakujibu kirahisi tu, Mimi ndiye konda na yule mimi simjui, kwani uliongea na mimi?

Hapo itabidi ulipe kiwango husika na kuharibu bajeti yako.

2: Baadhi ya wapiga debe wamekuwa wakiwaibia abiria fedha na simu.

3. Wengine wanajitokeza kushusha mizigo kweny gari, na wanakulazimisha uwalipe.

VIJANA WENGI HAWAFANYI KAZI ZAIDI YA KUKAA KWENYE |VITUO VYA MABASI NA KUDAI MAKONDAKTA WAWAPE HELA KWA LAZIMA

JE MAMLAKA HUSIKA WANAFAHAMU HIZI KERO? JE WAMESHINDWA KUWEKA UTARATIBU WA WENYE MABASI KUSIMAMIA JAMBO HILI?
 
Dikteta Uchwara alisema waachwe tu wasibugudhiwe.
 
Machinga na wapiga debe walimpigia kura hivyo waachwe tu.
 
Huyo konda hajakutana na mimi.Kama hamtambui mpiga debe kwanini alimuacha amtaftie abiria???
Mimi nilishawahi muambia mpiga debe nina nauli pungufu akasema panda katikati ya safari konda nampa nauli anazingua eti sijaomba kutoa pungufu wakati napanda.Niliwasha moto balaa nikamwambia nlimuomba nlomkuta mlangoni kama hamtambui hainihusu. Ikabidi apokee nilichompa.
Hawa wanaong'ang'ania kubebea abiria mizigo nao ni pasua kichwa. Unakuta unamwambia asibebe ye anakazana tu. unamwambia kaka shusha mzigo ye anajitoa ufahamu anajitia haelewi - baadae anakuambia "buku"....mi naishia kumwambia asante kwa huduma yako, bhaaaaas.Hata azingue vipi ,we utabebaje mzigo wangu bila makubaliano?
 
Nakumbuka Siku moja naenda ubungo kupanda bus za kwenda Arusha..nipo nabegi langu wakaja wapiga debe bro unaenda WAP?..nikawajibu naelekea Zanzibar kilichofata..nikusonya na kuniambia bro unazarau kazi za watu
 
Nakumbuka Siku moja naenda ubungo kupanda bus za kwenda Arusha..nipo nabegi langu wakaja wapiga debe bro unaenda WAP?..nikawajibu naelekea Zanzibar kilichofata..nikusonya na kuniambia bro unazarau kazi za watu
 
Nakumbuka Siku moja naenda ubungo kupanda bus za kwenda Arusha..nipo nabegi langu wakaja wapiga debe bro unaenda WAP?..nikawajibu naelekea Zanzibar kilichofata..nikusonya na kuniambia bro unazarau kazi za watu

Yaani imekuwa kama lazima hivi, utawakuta kwenye kituo wanalazimisha wapewe hela utafikiri wana hatimiliki na kile kituo.
 
Back
Top Bottom