Kero za Wananchi Shinyanga Vijijini

Mwanaukweli

JF-Expert Member
May 18, 2007
4,786
1,710
Zahanati ya kata ya Usule wilaya ya Shinyanga vijijini haina maji. Wagonjwa wanaolazwa hapo, wakiwemo akina mama wajawazito wanaokaribia kujifungua hulazimika kwenda na maji yao.

Vilevile baada ya kujifungua hakuna maji ya kufanya usafi, jambo ambalo hulazimisha akina mama hao kutunza nguo zao chafu mpaka wanapotoka ndipo zikafuliwe nyumbani, jambo ambalo ni hatari sana kiafya kwa wagonjwa wanaolazwa hapo.

Wakati huo huo wanalazimika kulipia fedha ili zahanati inunue maji ya kufulia mashuka ya zahanati waliyotumia.

attachment.php

Zahanati ya Usule kwa nje

attachment.php

Zahanati ya Usule kwa ndani
attachment.php

Mganga wa Usule akielezea matatizo.
attachment.php

Afisa Mtendaji wa Kata ya Usule
5.+Nape+akikumbatiana+na+Mgeja  +walipokutana+Kahama.jpg

Mh. Khamis Mgeja, Mbunge wa Shinyanga Vijijini akiwa na Bw. Nape Nnauye.





Kero hizi zitatatuliwa lini? Hawa watu wanahitaji nao maisha bora, miaka 51 baada ya uhuru watayapata lini hayo maisha bora?

Mbunge yuko wapi muda huu? Anangoja uchaguzi ukaribie ndio aje na maneno mazuri?
 
Last edited by a moderator:
Wananchi wa Shinyanga vijijini wanahitaji mbunge wao awatembelee na kusikia kero zao.
 
Mateso makubwa kwa wana shinyanga vijijini ,hakuna hata Huduma ya maji kwenye zahanati achilia mbali madawa na vifaa vingine vya tiba ikiwemo vipimo,usione hivyo tu,wilaya Hiyo haina hata hospitali ya wilaya,Huku mbunge mwarabu akijidai kuwaletea maendeleo wasukuma aw vijijini shy.tunasikia CDMA wameanza kuonyesha nia ya kulipata Hilo jimbo ili wakomboe walalahoi wanaoteseka na Lindi la umasikini.VIVA CDM kazeni Buti tuko nyuma yenu
 
Back
Top Bottom