Mwanaukweli
JF-Expert Member
- May 18, 2007
- 4,786
- 1,710
Zahanati ya kata ya Usule wilaya ya Shinyanga vijijini haina maji. Wagonjwa wanaolazwa hapo, wakiwemo akina mama wajawazito wanaokaribia kujifungua hulazimika kwenda na maji yao.
Vilevile baada ya kujifungua hakuna maji ya kufanya usafi, jambo ambalo hulazimisha akina mama hao kutunza nguo zao chafu mpaka wanapotoka ndipo zikafuliwe nyumbani, jambo ambalo ni hatari sana kiafya kwa wagonjwa wanaolazwa hapo.
Wakati huo huo wanalazimika kulipia fedha ili zahanati inunue maji ya kufulia mashuka ya zahanati waliyotumia.
Zahanati ya Usule kwa nje
Zahanati ya Usule kwa ndani
Mganga wa Usule akielezea matatizo.
Afisa Mtendaji wa Kata ya Usule
Mh. Khamis Mgeja, Mbunge wa Shinyanga Vijijini akiwa na Bw. Nape Nnauye.
Kero hizi zitatatuliwa lini? Hawa watu wanahitaji nao maisha bora, miaka 51 baada ya uhuru watayapata lini hayo maisha bora?
Mbunge yuko wapi muda huu? Anangoja uchaguzi ukaribie ndio aje na maneno mazuri?
Vilevile baada ya kujifungua hakuna maji ya kufanya usafi, jambo ambalo hulazimisha akina mama hao kutunza nguo zao chafu mpaka wanapotoka ndipo zikafuliwe nyumbani, jambo ambalo ni hatari sana kiafya kwa wagonjwa wanaolazwa hapo.
Wakati huo huo wanalazimika kulipia fedha ili zahanati inunue maji ya kufulia mashuka ya zahanati waliyotumia.
Zahanati ya Usule kwa nje
Zahanati ya Usule kwa ndani
Mganga wa Usule akielezea matatizo.
Afisa Mtendaji wa Kata ya Usule
Mh. Khamis Mgeja, Mbunge wa Shinyanga Vijijini akiwa na Bw. Nape Nnauye.
Kero hizi zitatatuliwa lini? Hawa watu wanahitaji nao maisha bora, miaka 51 baada ya uhuru watayapata lini hayo maisha bora?
Mbunge yuko wapi muda huu? Anangoja uchaguzi ukaribie ndio aje na maneno mazuri?
Last edited by a moderator: