KERO Kero ya barabara ya Machinjioni- Kakebe Mwanza

KERO Kero ya barabara ya Machinjioni- Kakebe Mwanza

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
Joined
Jun 5, 2019
Posts
46
Reaction score
63
Barabara hii ni muhimu kwa shughuli za kiuchumi kwa maana kuna viwanda vingi maeneo hayo, soko kubwa la vyakula na machinjio kubwa ya ng'ombe.

Jambo la kushangaza kuna daladala zinazoenda maeneo mbali mbali ya jiji zinapita hapo ila barabara ni mbovu kupitiliza na haipitiki vyema kipindi cha mvua. Viingozi wa serikali wapo na ni suhala la muda mrefu ila linafumbiwa macho.

Tunaomba viongozi wawajibike ipasavyo kwamaana kodi na ushuru mwingi unatozwa maeneo hayo kutokana na shughuli nyingi za kiuchumi

Hii ndo hali halisi
Screenshot_20260219_101806_Video Player.jpg
Screenshot_20260219_101709_Video Player.jpg
Screenshot_20260219_101623_Video Player.jpg
Screenshot_20260219_101607_Video Player.jpg
 
Ni miaka sasa na bado wanampa
Sima umeya na anaishi huko🤦🏽‍♀️
na huko machinjioni ni pachafu mno mazingira yake yalikua yananikera ila ndo vile sikua na namna kwa kipindi hicho,, sitaki kuamini mpka leo bado mazingira hayaja badilika
 
Safi sana kwa uletaji wako wa taarifa
Ni mwendo wa picha na tumekusoma hio barabara waishughulikie
 
na huko machinjioni ni pachafu mno mazingira yake yalikua yananikera ila ndo vile sikua na namna kwa kipindi hicho,, sitaki kuamini mpka leo bado mazingira hayaja badilika
Pako vilevile na wanakaa matajiri wakubwa tu kule, kukiwa na vumbi kero! mvua ikinyesha kero! matope ya ajabu yanaibuka pale sokoni panatia kinyaa sio poa!🙌🏾
 
Pako vilevile na wanakaa matajiri wakubwa tu kule, kukiwa na vumbi kero! mvua ikinyesha kero! matope ya ajabu yanaibuka pale sokoni panatia kinyaa sio poa!🙌🏾
ukiwa unatembea barabarani hakuna hata kajiachia ni mwendo wa kupepesa macho usikanyage bidhaa za watu, matope au kutizama vyombo vya moto,,, bara bara ipo busy mda wote
 
Tunachokitaka wananchi ni barabara irekebishwe kwa kiwango cha lami , zege au morum. Kuanzia pale nile perch mpaka kakebe.

Haiwezekani gari za kakebe ziishie mhandu kanisani kisa barabara mbovu na mamlaka ipo. Kuna kidaraja uchwara kilijengwa maeneo ya kakebe shule ya msingi mpaka leo kameachwa vile vile.

Nimeona leo wafanyabihashara wameambiwa wafanye usafi barabarani ila haiondoi ukweli kua barabara inakua na matope makali na madimbwi ya maji mvua ikinyesha.

Tunataka barabara ya kiwango ili magari yapite kwa uhuru,.. Watu wapite kwa uhuru. Mandari ya machinjioni kakebe yapendeze na uchumi uzidi kukua zaidi sio blaa blaa.
 
Kadhalika njia ya kijereshi kuelekea machinjioni nayo iko taabani ni mbovu mnoo.

Kuna soko la gulio hua liko katika njia hiyo ni hatari mnoo . Barabara inakua finyu na madimbwi kibao.

Lile eneo lenye kitete kwanini msiliboreshe ili wafanyabihashara wafanye gulio lao kwa nafasi na sio kufanya bihashara barabarani?


Viongozi kuweni na utu. Diwani unauwezo wa kutengeneza mabango ya gharama ya uchaguzi lakini kero kama hizi za wazi hazikuhusu.


SHAME ON YOU
 
Back
Top Bottom