Kero kifusi barabara ya Bunyokwa

Manyiri

Member
Oct 27, 2007
80
15
Ni wiki ya Pili sasa hadi Leo Tarehe 13/02/2021 vifusi vilivyowekwa katika barabara ya Bonyokwa ya Segerea kuelekea Bonyokwa kwa Kichwa havijasawazishwa.

Hii imekuwa kero kubwa kwa watumiaji wa barabara hii kwani inasababisha usumbufu mkubwa wa magari kupishana na inaweza kusababisha ajali hasa sehemu ya Mlima na mteremko mkali magari yanapata Shida kupishana.

Vifusi hivi kucheleweshwa kusawazishwa ni sawa sawa na Kusema “justice delayed is justice denied “.

Naomba wahusika wanaowasimamia hawa watu wasiojitambua kwa kutelekeza vifusi hivi wafuatilie.
 
Back
Top Bottom