Kero daraja la Nyerere-Kigamboni Dar es Salaam

vngenge

JF-Expert Member
Apr 19, 2011
539
270
Sisi watumiaji ambao ndio wateja wa daraja la Nyerere Kigamboni tunakerwa na hii tabia ya watendaji hapa darajani.

Nyakati ambazo ni busy asubuhi na jioni, mageti matatu au manne kati ya saba yaliyopo ndio hufanya kazi, jambo linalosababisha foleni na hivyo kudhoofisha lengo la serikali la kuondoa kero za usafiri kwa kuboresha miundombinu.

Nimefanya uchunguzi wa muda mrefu na kugundua kuwa hii imekuwa ni tabia wala sio ubovu wa haya mageti kama ambavyo nilidhani hapo mwanzo.

Watanzania tujifunze kufanya kazi kwa bidii, tuache uvivu na tumuunge mkono kiongozi wetu kwa kufanya kazi kwa bidii na maarifa.

Tunawataka wahusika kuchukua hatua ili kuondoa usumbufu kwa kuhakikisha mageti yote yanafanya kazi muda wote.
 
Naunga mkono hoja.

Pia kipande cha barabara kutoka darajani hadi tungi kijengwe kwa kiwango cha lami,ni aibu mradi mkubwa kama ule kushindwa kumalizia kipande cha takribani Km 1 kuunganishwa na daraja.
 
Naunga mkono hoja.

Pia kipande cha barabara kutoka darajani hadi tungi kijengwe kwa kiwango cha lami,ni aibu mradi mkubwa kama ule kushindwa kumalizia kipande cha takribani Km 1 kuunganishwa na daraja.
Mbona hiyo ni kawaida Yao...hujaona sehemu ambayo lami inapigwa kwa sababu Kuna mtu fulani....kwa wengine ni vumbi tu
Natoaa mfano,lami iliyopigwa hananasif kuelekea kanisa almaarufu kwa pinda ni kwa sababu ya waziri Mkuu aliyepita,sehemu nyingine ni kwa mwinyi mikocheni lami ile ilipigwa kwa ajili yake....sehemu nyingine adaestate pale alipokuwa anaishi wazir wa ujenzi na ambaye sahv ni prezda lami ilipigwa barabara tu ya kuekekeaaa Keane kwenginekoo
Mashimoo tu....kwengine kinitonyama mabatini kwa Akija mstafuu Yule mamá lami ilipigwa hadi kuelekea kwake lkn sahv barabara ishakuwaa kimeooo....
Kwa haya nliyosema serikali inaweza kutekeleza Sema Kuna uzembe fulani au upendeleooo fulani unaofanyika....
 
Mbona hiyo ni kawaida Yao...hujaona sehemu ambayo lami inapigwa kwa sababu Kuna mtu fulani....kwa wengine ni vumbi tu
Natoaa mfano,lami iliyopigwa hananasif kuelekea kanisa almaarufu kwa pinda ni kwa sababu ya waziri Mkuu aliyepita,sehemu nyingine ni kwa mwinyi mikocheni lami ile ilipigwa kwa ajili yake....sehemu nyingine adaestate pale alipokuwa anaishi wazir wa ujenzi na ambaye sahv ni prezda lami ilipigwa barabara tu ya kuekekeaaa Keane kwenginekoo
Mashimoo tu....kwengine kinitonyama mabatini kwa Akija mstafuu Yule mamá lami ilipigwa hadi kuelekea kwake lkn sahv barabara ishakuwaa kimeooo....
Kwa haya nliyosema serikali inaweza kutekeleza Sema Kuna uzembe fulani au upendeleooo fulani unaofanyika....

Yaani hiki kitu Tanzania kimeshakuwa sugu sijui tuite ujinga. Maendeleo yanapelekwa kwenye eneo kwa sababu ya uwepo wa mtu fulani. Kiasi imefikia hata ukitaka kutafuta kiwanja mpaka uulize kuna mkubwa fulani ndio huduma inafika.

Umeme haufiki eneo au kukatika hovyo hadi usikie mkurugenzi wa Tanesco anaishi huko.

Barabara haijengwi hadi usikie kuna bosi wa Tanroad anaishi huko.

Maji hayapelekwi au kukatwa hadi usikie kuna mkubwa anaishi huko.

Bajeti zinapelekwa kiupendeleo. Inaniuma sana. Sijui kwetu Bangulo atakuja kuishi mkubwa gani tupapte huduma stahiki.
 
Cc:Dengue,kweli mpaka awepo mkubwa fulani au mtoto/familia ya mkubwa fulani ndiyo miundo mbinu itawekwa Sawa......sehemu nyingine hata pale kwa nyerere njia ya kwenda rose guarden Kuna mtaa kwa nyuma unaitwa wamata..mtoto wa mamá Anna m..... Aliponunua nyumbaaa tu lami ikapigwaaa....
Yaaani Kuna maisha mpe Huyu na mruke huyuuu
 
Sisi watumiaji ambao ndio wateja wa daraja la Nyerere Kigamboni tunakerwa na hii tabia ya watendaji hapa darajani.

Nyakati ambazo ni busy asubuhi na jioni, mageti matatu au manne kati ya saba yaliyopo ndio hufanya kazi, jambo linalosababisha foleni na hivyo kudhoofisha lengo la serikali la kuondoa kero za usafiri kwa kuboresha miundombinu.

Nimefanya uchunguzi wa muda mrefu na kugundua kuwa hii imekuwa ni tabia wala sio ubovu wa haya mageti kama ambavyo nilidhani hapo mwanzo.

Watanzania tujifunze kufanya kazi kwa bidii, tuache uvivu na tumuunge mkono kiongozi wetu kwa kufanya kazi kwa bidii na maarifa.

Tunawataka wahusika kuchukua hatua ili kuondoa usumbufu kwa kuhakikisha mageti yote yanafanya kazi muda wote.
Unachukua muda gani kufika hapo getini hadi kuvuka?!!
 
Wafungue pia na ile sehemu ya U-turn ukiwa umetoka kuvuka daraja kabla ya kufika sehemu ya kulipia ticket. Wanakuwa waroho wa pesa kwa kuziba U-turn ya kwenye design
 
Naunga mkono hoja.

Pia kipande cha barabara kutoka darajani hadi tungi kijengwe kwa kiwango cha lami,ni aibu mradi mkubwa kama ule kushindwa kumalizia kipande cha takribani Km 1 kuunganishwa na daraja.
Kitu hiki kinanishangaza sana....unajenga daraja la mabilioni unashindwa kumalizia kipande cha km 1.5!!!!!
 
Wafungue pia na ile sehemu ya U-turn ukiwa umetoka kuvuka daraja kabla ya kufika sehemu ya kulipia ticket. Wanakuwa waroho wa pesa kwa kuziba U-turn ya kwenye design
Nimeona pale wameweka matofali...ndio maandalizi ya kupafungua?! Maanake wageni huwa wanajikuta wanatoka/kuingia darajani bila kupenda.
 
Cc:Dengue,kweli mpaka awepo mkubwa fulani au mtoto/familia ya mkubwa fulani ndiyo miundo mbinu itawekwa Sawa......sehemu nyingine hata pale kwa nyerere njia ya kwenda rose guarden Kuna mtaa kwa nyuma unaitwa wamata..mtoto wa mamá Anna m..... Aliponunua nyumbaaa tu lami ikapigwaaa....
Yaaani Kuna maisha mpe Huyu na mruke huyuuu

Mkuu inakera sana. Mimi wakati nataka niweke umeme nilienda pale Tanesco Ukonga wakanizingua saana. Mwisho wa siku nikapiga simu nikajitambulisha kama mkubwa ndani ya ccm na kuwaambia ndugu yangu anahitaji umeme sehemu fulani mbona mnamzungusha? Siku hiyo hiyo nilipata umeme.
 
Mkuu inakera sana. Mimi wakati nataka niweke umeme nilienda pale Tanesco Ukonga wakanizingua saana. Mwisho wa siku nikapiga simu nikajitambulisha kama mkubwa ndani ya ccm na kuwaambia ndugu yangu anahitaji umeme sehemu fulani mbona
mnamzungusha? Siku hiyo hiyo nilipata
umeme.
Duh aise!yaani hawa jamaa badala kuweka miundo mbinu mizuri kwa wananchi ambao ni walipa kodi,wao wanawawekeaaa wavimbaa matumbooo wa serikalini
Mkuu inakera sana. Mimi wakati nataka niweke umeme nilienda pale Tanesco Ukonga wakanizingua saana. Mwisho wa siku nikapiga simu nikajitambulisha kama mkubwa ndani ya ccm na kuwaambia ndugu yangu anahitaji umeme sehemu fulani mbona mnamzungusha? Siku hiyo hiyo nilipata umeme.
 
Kwa kweli utendaji wa kazi wa daraja la kigamboni kwa sasa unakera sanaaa, hivi ni vitu baadhi vinakwaza:
1. Madirisha mengi, wanaokatisha tiketi madirisha ma3 tu kwa nin?
2. Watu wako slow mpaka wanakera, imagine asubuhi watu tunawah kazin msururu wa magari mpaka njia ya kwenda vijibweni, nin hii sasa?
3.Mtu anaona gari ni ya aina gani anakuuliza "Hivi gari yako ni aina gani?, nikate shillingi ngapi?
4. Je wafanyakazi wenu hawana ujuzi wa kutosha, au hawatoshi?

Wahusika tunaomba mlifanyie kazi hili swala, lile daraja lipo kwa ajili ya kurahisisha mambo na kufanya maisha yawe murua, sasa likiwa kero tena hatuwaelewi kabisaaaaa......

LISHUGHULIKIWE MAPEMA TAFADALI.........MNATUKWAZA

Shukrani.
 
Kwa kweli utendaji wa kazi wa daraja la kigamboni kwa sasa unakera sanaaa, hivi ni vitu baadhi vinakwaza:
1. Madirisha mengi, wanaokatisha tiketi madirisha ma3 tu kwa nin?
2. Watu wako slow mpaka wanakera, imagine asubuhi watu tunawah kazin msururu wa magari mpaka njia ya kwenda vijibweni, nin hii sasa?
3.Mtu anaona gari ni ya aina gani anakuuliza "Hivi gari yako ni aina gani?, nikate shillingi ngapi?
4. Je wafanyakazi wenu hawana ujuzi wa kutosha, au hawatoshi?

Wahusika tunaomba mlifanyie kazi hili swala, lile daraja lipo kwa ajili ya kurahisisha mambo na kufanya maisha yawe murua, sasa likiwa kero tena hatuwaelewi kabisaaaaa......

LISHUGHULIKIWE MAPEMA TAFADALI.........MNATUKWAZA

Shukrani.
pole sana
 
Back
Top Bottom