Kasomi
JF-Expert Member
- Sep 3, 2014
- 11,036
- 20,337
KENYA WAMETUPIGA KWENYE MSHONO TENA.
Kenya umepiga marufuku mahidi ya Tanzania kwa kuwa Yana sumu inayosababisha Cancer na wametangaza hadharani na wameitangazia Dunia.
Mwaka 1776 Jasusi wa Kimarekani William Carmichael alitumwa na Taifa lake kwenda kutafiti na kujua ni kwa namna gani USA inaweza kuteka soko la Tumbaku Duniani ambalo lilikuwa limeshikiliwa na bara Ulaya. Kipindi hicho Ukraine ilikuwa ikizalisha tumbaku Bora kabisa na nyingi Duniani.
Jasusi huyu alitokea kwenye kitengo Cha Economic intelligence. Economic intelligence ni kitengo katika mashirika ya kijasusi mengi duniani lakini department hii hudili na kuangalia threats za nchi husika kiuchumi. Hawa hutafiti, huchunguza mataifa Mengine kuhusu Uchumi wao na namna ya kuudidimiza. Marekani wao kwa Sasa Taifa ambalo linachunguzwa Sana ni China na Korea Kaskazini. Lengo ni kuwadhibiti wasiliteke soko la Dunia kwa bidhaa zao au wasiibuke Kama super power duniani.
Sio nchi kwa nchi tu huchunguzana Bali hata Kampuni na Kampuni zinazozalisha bidhaa za aina Moja huchunguzana. Nafikiri unakumbuka mgogoro wa Simu za Huwawei na Kampuni la Google.
Kwa Africa Mashariki Kenya ni mojawapo ya Taifa ambalo limewekeza kwenye Economic intelligence, na Taifa tishio kwao ni Tanzania. Tukumbuke Tanzania ina rasilimali nyingi kuliko Kenya, ina nufaika na Geographical location yake na pia hatuna ukame Sana.
Kenya wanajua wazi kuwa isingelikuwa bandari ya Daresalam na Tanga Basi wao wangenufaika Sana kupitia bandari ya Mombasa. Bandari zetu zinapunguza Sana bidhaa za mataifa Mengine kupitia Kenya hili kwao ni tishio.
Kenya wanajua kabisa Kama sio vivutio vyetu tulivyo navyo Basi wao wangeongoza kwa utalii Africa Mashariki na wangelipiga pesa nyingi Sana kwenye utalii.
Mwaka juzi madereva wa Tanzania wa utalii pamoja na kuwa walifuata taratibu zote walinyimwa kuchukua watalii waliokuwa wanakuja Tanzania kutalii ambao walishukia Kenya. Tanzania ilivumilia kwa Muda lakini ilifika mahali tukajibu kwa kupunguza trip za Kenya airways kuja nchini. Walipoona hivyo wakaondoa lile zuio la madereva wetu wa utalii kuingia Kenya. Ndio maana nchi iliwekeza Sana kwenye Kununua ndege kwa kuwa ili ujitawale vizuri lazima uwe na uwezo wa kushindana angani, ardhini na majini.
Mwaka 2018 tuliingia nao tena Mzozo wa kiuchumi tukigombea bomba la mafuta toka Uganda lipitie wapi. Wakenya walipiga trip Sana kwenda Uganda kwa mzee Museven hatimaye tukawashinda Tena kwenye Vita ile.
Mwaka 2020 wakati wa Corona Madereva wote wa Tanzania ilikuwa hawaruhusiwi kuingia Kenya lakini wa Kenya walikuwa wakiruhusiwa Hadi tulipifunga mipaka ya Hororo kule Tanga na Namanga Arusha ndio walitia akili wakatuachilia.
Mwaka 2021 mwanzoni kule Rombo ilikuwa dereva wa Bodaboda akivuka Kwenda Kenya alikuwa akishikwa na kufungwa au kufunguliwa Kesi. Mkuu wa Mkoa Wa Kilimanjaro alipambana na issue hii Sana na naimani imetulia kwa Sasa.
Kuna kipindi wakenya walitaka kuwafukuza wafanyabiashara wote waliopo Nairobi toka Tanzania nafikiri mnakumbuka.
ISISUE YA MAHINDI.
Kwanza Kenya wametufanyia mbaya Sana kutangaza Moja kwa Moja bila kutupa taarifa kama jirani mwema tuyapime Kama kweli yana Sumu. Tafsiri rahisi Ni kwamba mahindi yetu yatakuwa yamekosa soko kwenye nchi zote kwa kuwa tu Kenya imetangaza Moja kwa Moja kuwa yana Sumu.
Sijui kama Balozi wetu Kenya anafanya kazi gani Ila ningeshauri abadilishwe apelekwe mtu mwingine mwenye uwezo wa kunusa mbali na mwenye ushawishi na anayeweza kutibu mipasuko ya nchi zote mbili. Taifa hili lina vijana Smart wanaoweza kucheza hii michezo kwa umadhubuti mkubwa..... Tuna nchi ambazo tuna maslahi nazo Kama Kenya si pa kupeleka Balozi Ni Balozi economic intelligence huanzia hapa. Someni historia ya Balozi wa Kenya nchini Tanzania. Yupo very Smart Hadi Rais aliwahi kutamani kumpa uraia.
Nalaumu kuhusu Balozi lakini pia idara nyingine kwa kuwa Kenya toka mwaka Jana walishaonyesha interest ya kununua mahindi toka Mexico, Malawi na Zambia kwa kuwa aidha wanayapata kwa Bei rahisi na hakuna mlolongo wa Kodi. Fuata link ifuatayo ambayo gazeti la the East African lilishaonyesha Dalili kuwa Kenya itaagiza mahindi toka kwenye hayo mataifa.
Kenya in plan to import 2m bags of maize by May
Inawezekana Kenya imeyapata Mahindi kwenye mataifa hayo kwa Bei Rahisi zaidi kuliko hapa kwetu. Na Kenya wametunyima Soko la mahindi kipindi ambacho wanauhitaji mkubwa Sana w mahindi kutokana na Nzige na Corona.
Tulitamka hadharani kuwa wakati watu wakiwa lockdown sisi tulime mahindi tutakuja kuwauzia. Sasa kwa kauli hii ya Kenya hatutauza popote. Tuboreshe idara zetu nyeti.
Wametuotea katika hili. Je, ni kweli yana sumu au ni Siasa ya kiuchumi? Wametupiga panapouma.
Pia soma; Tanzania ni Taifa kubwa, tusiyumbishwe
Kenya umepiga marufuku mahidi ya Tanzania kwa kuwa Yana sumu inayosababisha Cancer na wametangaza hadharani na wameitangazia Dunia.
Mwaka 1776 Jasusi wa Kimarekani William Carmichael alitumwa na Taifa lake kwenda kutafiti na kujua ni kwa namna gani USA inaweza kuteka soko la Tumbaku Duniani ambalo lilikuwa limeshikiliwa na bara Ulaya. Kipindi hicho Ukraine ilikuwa ikizalisha tumbaku Bora kabisa na nyingi Duniani.
Jasusi huyu alitokea kwenye kitengo Cha Economic intelligence. Economic intelligence ni kitengo katika mashirika ya kijasusi mengi duniani lakini department hii hudili na kuangalia threats za nchi husika kiuchumi. Hawa hutafiti, huchunguza mataifa Mengine kuhusu Uchumi wao na namna ya kuudidimiza. Marekani wao kwa Sasa Taifa ambalo linachunguzwa Sana ni China na Korea Kaskazini. Lengo ni kuwadhibiti wasiliteke soko la Dunia kwa bidhaa zao au wasiibuke Kama super power duniani.
Sio nchi kwa nchi tu huchunguzana Bali hata Kampuni na Kampuni zinazozalisha bidhaa za aina Moja huchunguzana. Nafikiri unakumbuka mgogoro wa Simu za Huwawei na Kampuni la Google.
Kwa Africa Mashariki Kenya ni mojawapo ya Taifa ambalo limewekeza kwenye Economic intelligence, na Taifa tishio kwao ni Tanzania. Tukumbuke Tanzania ina rasilimali nyingi kuliko Kenya, ina nufaika na Geographical location yake na pia hatuna ukame Sana.
Kenya wanajua wazi kuwa isingelikuwa bandari ya Daresalam na Tanga Basi wao wangenufaika Sana kupitia bandari ya Mombasa. Bandari zetu zinapunguza Sana bidhaa za mataifa Mengine kupitia Kenya hili kwao ni tishio.
Kenya wanajua kabisa Kama sio vivutio vyetu tulivyo navyo Basi wao wangeongoza kwa utalii Africa Mashariki na wangelipiga pesa nyingi Sana kwenye utalii.
Mwaka juzi madereva wa Tanzania wa utalii pamoja na kuwa walifuata taratibu zote walinyimwa kuchukua watalii waliokuwa wanakuja Tanzania kutalii ambao walishukia Kenya. Tanzania ilivumilia kwa Muda lakini ilifika mahali tukajibu kwa kupunguza trip za Kenya airways kuja nchini. Walipoona hivyo wakaondoa lile zuio la madereva wetu wa utalii kuingia Kenya. Ndio maana nchi iliwekeza Sana kwenye Kununua ndege kwa kuwa ili ujitawale vizuri lazima uwe na uwezo wa kushindana angani, ardhini na majini.
Mwaka 2018 tuliingia nao tena Mzozo wa kiuchumi tukigombea bomba la mafuta toka Uganda lipitie wapi. Wakenya walipiga trip Sana kwenda Uganda kwa mzee Museven hatimaye tukawashinda Tena kwenye Vita ile.
Mwaka 2020 wakati wa Corona Madereva wote wa Tanzania ilikuwa hawaruhusiwi kuingia Kenya lakini wa Kenya walikuwa wakiruhusiwa Hadi tulipifunga mipaka ya Hororo kule Tanga na Namanga Arusha ndio walitia akili wakatuachilia.
Mwaka 2021 mwanzoni kule Rombo ilikuwa dereva wa Bodaboda akivuka Kwenda Kenya alikuwa akishikwa na kufungwa au kufunguliwa Kesi. Mkuu wa Mkoa Wa Kilimanjaro alipambana na issue hii Sana na naimani imetulia kwa Sasa.
Kuna kipindi wakenya walitaka kuwafukuza wafanyabiashara wote waliopo Nairobi toka Tanzania nafikiri mnakumbuka.
ISISUE YA MAHINDI.
Kwanza Kenya wametufanyia mbaya Sana kutangaza Moja kwa Moja bila kutupa taarifa kama jirani mwema tuyapime Kama kweli yana Sumu. Tafsiri rahisi Ni kwamba mahindi yetu yatakuwa yamekosa soko kwenye nchi zote kwa kuwa tu Kenya imetangaza Moja kwa Moja kuwa yana Sumu.
Sijui kama Balozi wetu Kenya anafanya kazi gani Ila ningeshauri abadilishwe apelekwe mtu mwingine mwenye uwezo wa kunusa mbali na mwenye ushawishi na anayeweza kutibu mipasuko ya nchi zote mbili. Taifa hili lina vijana Smart wanaoweza kucheza hii michezo kwa umadhubuti mkubwa..... Tuna nchi ambazo tuna maslahi nazo Kama Kenya si pa kupeleka Balozi Ni Balozi economic intelligence huanzia hapa. Someni historia ya Balozi wa Kenya nchini Tanzania. Yupo very Smart Hadi Rais aliwahi kutamani kumpa uraia.
Nalaumu kuhusu Balozi lakini pia idara nyingine kwa kuwa Kenya toka mwaka Jana walishaonyesha interest ya kununua mahindi toka Mexico, Malawi na Zambia kwa kuwa aidha wanayapata kwa Bei rahisi na hakuna mlolongo wa Kodi. Fuata link ifuatayo ambayo gazeti la the East African lilishaonyesha Dalili kuwa Kenya itaagiza mahindi toka kwenye hayo mataifa.
Kenya in plan to import 2m bags of maize by May
Inawezekana Kenya imeyapata Mahindi kwenye mataifa hayo kwa Bei Rahisi zaidi kuliko hapa kwetu. Na Kenya wametunyima Soko la mahindi kipindi ambacho wanauhitaji mkubwa Sana w mahindi kutokana na Nzige na Corona.
Tulitamka hadharani kuwa wakati watu wakiwa lockdown sisi tulime mahindi tutakuja kuwauzia. Sasa kwa kauli hii ya Kenya hatutauza popote. Tuboreshe idara zetu nyeti.
Wametuotea katika hili. Je, ni kweli yana sumu au ni Siasa ya kiuchumi? Wametupiga panapouma.
Pia soma; Tanzania ni Taifa kubwa, tusiyumbishwe