Kenya kuna hiyo mnayoita Tume Huru, lakini bado...!

Barbarosa

JF-Expert Member
Apr 16, 2015
22,584
27,787
Nchi ya Kenya baada ya kuandika Katiba yake mpya imeweka hiyo ambayo WatanZania wafuasi wa Lowasa & Co. wanaiita Tume huru, ambayo wanataka na sisi pia tuwe nayo kwamba kwa maneno yao hiyo ndiyo itahakikisha Uchaguzi wa TZ kuwa wa huru na haki kwa mujibu wa wana ukawa, lkn wasichokijua ni kwamba mpaka aleo hii wapinzani wa Kenya chini ya Raila Odinga ambaye alikuwa Makamu wa Raisi wakati wa uchaguzi na alishiriki kwenye uundwaji wa hiyo Tume anasema kwamba aliibiwa kura, yaani Uhuru Kenyata aliiba kura na hivi sasa kuna ishu kubwa na Tume hiyo kwamba haitendi haki!

Hii inaonyesha kwamba hapa Afrika sisi ni watu wa kutafuta visingizio siku zote inanikumbusha maneno ya Raisi Kikwete aliyesema Mwafrika huwa hakubali kushindwa hata siku moja hivyo hata hapa TZ kama tukiwa na Tume kama ya Kenya bado hakutaondoa malalamiko ya wale watakaoshindwa, hivyo kila kitu kibakie kama kilivyo leo!
 
hata huo ufisadi watu wengi wanakomaa na katiba mpya kuwa ndio mwarubaini wa ufisadi
kenya ndo wanakatiba mpya ambayo inasifiwa na kila mtu lakin ndo kwanza ufisadi unashamiri pamoja na kuwa na hiyo katiba nzuri
 
hata huo ufisadi watu wengi wanakomaa na katiba mpya kuwa ndio mwarubaini wa ufisadi
kenya ndo wanakatiba mpya ambayo inasifiwa na kila mtu lakin ndo kwanza ufisadi unashamiri pamoja na kuwa na hiyo katiba nzuri
Stupid comment/views? May be! Nani alisema KATIBA MPYA huwa inaondoa ufisadi. Nimesoma na kusikia mijadala mingi, na watu wanasema KATIBA NZURI ni moja ya viungio vya kupambana na ufisadi. Katiba nzuri peke yake bila uongozi wenye dhamira haitoshi. Lesson number one to you: Katiba mpya sio sawa na katiba nzuri.
 
Endelea kupalilia kibarua. Ila mkumbushe mtukufu Magu asisahau kukata kodi posho zenu pia.
 
Nchi ya Kenya baada ya kuandika Katiba yake mpya imeweka hiyo ambayo WatanZania wafuasi wa Lowasa & Co. wanaiita Tume huru, ambayo wanataka na sisi pia tuwe nayo kwamba kwa maneno yao hiyo ndiyo itahakikisha Uchaguzi wa TZ kuwa wa huru na haki kwa mujibu wa wana ukawa, lkn wasichokijua ni kwamba mpaka aleo hii wapinzani wa Kenya chini ya Raila Odinga ambaye alikuwa Makamu wa Raisi wakati wa uchaguzi na alishiriki kwenye uundwaji wa hiyo Tume anasema kwamba aliibiwa kura, yaani Uhuru Kenyata aliiba kura na hivi sasa kuna ishu kubwa na Tume hiyo kwamba haitendi haki!

Hii inaonyesha kwamba hapa Afrika sisi ni watu wa kutafuta visingizio siku zote inanikumbusha maneno ya Raisi Kikwete aliyesema Mwafrika huwa hakubali kushindwa hata siku moja hivyo hata hapa TZ kama tukiwa na Tume kama ya Kenya bado hakutaondoa malalamiko ya wale watakaoshindwa, hivyo kila kitu kibakie kama kilivyo leo!
Katiba ya Kenya sio nzuri. Bado imempa rais madaraka ya ki-mungu. Bado imetoa nafasi kwa wanasiasa kuwa kila kitu na kila mahali. Ukiangalia mlolongo wa vyeo vya kisiasa kuanzia juu mpaka chini unatoa mwanya wa wanasiasa kuwa kila kitu.
 
Stupid comment/views? May be! Nani alisema KATIBA MPYA huwa inaondoa ufisadi. Nimesoma na kusikia mijadala mingi, na watu wanasema KATIBA NZURI ni moja ya viungio vya kupambana na ufisadi. Katiba nzuri peke yake bila uongozi wenye dhamira haitoshi. Lesson number one to you: Katiba mpya sio sawa na katiba nzuri.



Sasa ndiyo umeandika nini? Kenya tunaambiwa ndiyo wana moja kati ya nzuri Afrika lkn Ufisadi uliotokea ndani ya Katiba nzuri na bora klk zote Afrika hauajwahi kutokea nchini Kenya hata klk wakati wa Chama kimoja na bado Raisi yuko madarakani na hakuna aliyechukuliwa, Uchaguzi wa Uraisi mpaka leo hii wanasema Uhuru Kenyata aliiba kura na Raila Odinga kama alivyo fisadi Lowasa anasema kwamba alishinda uchaguzi na Tume ilimpora ingawaje hiyo Tume yeye ndiyo alishiriki kuiunda na inadaiwa ni huru, na sasa hivi kuna bonge la skendo kuhusu hiyo Tume!
 
Sasa ndiyo umeandika nini? Kenya tunaambiwa ndiyo wana moja kati ya nzuri Afrika lkn Ufisadi uliotokea ndani ya Katiba nzuri na bora klk zote Afrika hauajwahi kutokea nchini Kenya hata klk wakati wa Chama kimoja na bado Raisi yuko madarakani na hakuna aliyechukuliwa, Uchaguzi wa Uraisi mpaka leo hii wanasema Uhuru Kenyata aliiba kura na Raila Odinga kama alivyo fisadi Lowasa anasema kwamba alishinda uchaguzi na Tume ilimpora ingawaje hiyo Tume yeye ndiyo alishiriki kuiunda na inadaiwa ni huru, na sasa hivi kuna bonge la skendo kuhusu hiyo Tume!
Ndio maana basi nakuambia katiba ya Kenya sio nzuri. Kama uliambiwa hivyo, basi jaribu kuipitia uone. Usikubali kufuata tu mkumbo wa kutafuniwa.
 
Ndio maana basi nakuambia katiba ya Kenya sio nzuri. Kama uliambiwa hivyo, basi jaribu kuipitia uone. Usikubali kufuata tu mkumbo wa kutafuniwa.


Lkn ndiyo model ya Katiba inayopendekezwa na ukawa, mimi nilikuwa wala sina mpango na mambo ya Katiba ya Kenya mpaka pale niliposikia sifa kemu kem ktk kwa wana ukawa na kwamba walitaka waunde katiba yetu kwa mfano wa Katiba ya Kenya na ndiyo maana nikaanza kujielimisha kuhusu Katiba hiyo Kenya na madudu niliyoyakuta huko yalinikatisha tamaa, Wanasiasa wa Kenya wameiba Dola (US) bilioni na zaidi na bado utafiti haujakamilika na hakuna aliyeshitakiwa na Raisi ambaye ndiye msimamizi bado yuko!
 
Lkn ndiyo model ya Katiba inayopendekezwa na ukawa, mimi nilikuwa wala sina mpango na mambo ya Katiba ya Kenya mpaka pale niliposikia sifa kemu kem ktk kwa wana ukawa na kwamba walitaka waunde katiba yetu kwa mfano wa Katiba ya Kenya na ndiyo maana nikaanza kujielimisha kuhusu Katiba hiyo Kenya na madudu niliyoyakuta huko yalinikatisha tamaa, Wanasiasa wa Kenya wameiba Dola (US) bilioni na zaidi na bado utafiti haujakamilika na hakuna aliyeshitakiwa na Raisi ambaye ndiye msimamizi bado yuko!
Bado nasisitiza. Katiba nzuri bila dhamira ya kweli haisaidii. Wala tusiende mbali mpaka Kenya. Tuvuke hapo Zanzibar. Mwenyeketi wa tume ya uchaguzi ta Zanzibar ameamua yeye (kwa kushirikiana na CCM) kukiuka katiba na kufuta matokeo ya uchaguzi. Hili linatakiwa kukupa funzo: Hata katiba iwe nzuri namna gani bila utashi wa kuiheshimu ni bure.
 
Nchi ya Kenya baada ya kuandika Katiba yake mpya imeweka hiyo ambayo WatanZania wafuasi wa Lowasa & Co. wanaiita Tume huru, ambayo wanataka na sisi pia tuwe nayo kwamba kwa maneno yao hiyo ndiyo itahakikisha Uchaguzi wa TZ kuwa wa huru na haki kwa mujibu wa wana ukawa, lkn wasichokijua ni kwamba mpaka aleo hii wapinzani wa Kenya chini ya Raila Odinga ambaye alikuwa Makamu wa Raisi wakati wa uchaguzi na alishiriki kwenye uundwaji wa hiyo Tume anasema kwamba aliibiwa kura, yaani Uhuru Kenyata aliiba kura na hivi sasa kuna ishu kubwa na Tume hiyo kwamba haitendi haki!

Hii inaonyesha kwamba hapa Afrika sisi ni watu wa kutafuta visingizio siku zote inanikumbusha maneno ya Raisi Kikwete aliyesema Mwafrika huwa hakubali kushindwa hata siku moja hivyo hata hapa TZ kama tukiwa na Tume kama ya Kenya bado hakutaondoa malalamiko ya wale watakaoshindwa, hivyo kila kitu kibakie kama kilivyo leo!
Ni kweli sisi hatukabali kushindwa umeona CCM walivyokataa wakaamua kuliko kukubali bora turudie uchaguzi
 
Yaani mtoa mada kila siku ukitoa thread tu lazima umponde Lowasa hivi kakufanya nn, au alikupigia mkeo?
 

Sasa ndiyo umeandika nini? Kenya tunaambiwa ndiyo wana moja kati ya nzuri Afrika lkn Ufisadi uliotokea ndani ya Katiba nzuri na bora klk zote Afrika hauajwahi kutokea nchini Kenya hata klk wakati wa Chama kimoja na bado Raisi yuko madarakani na hakuna aliyechukuliwa, Uchaguzi wa Uraisi mpaka leo hii wanasema Uhuru Kenyata aliiba kura na Raila Odinga kama alivyo fisadi Lowasa anasema kwamba alishinda uchaguzi na Tume ilimpora ingawaje hiyo Tume yeye ndiyo alishiriki kuiunda na inadaiwa ni huru, na sasa hivi kuna bonge la skendo kuhusu hiyo Tume!
Mnaambiwaga na nani? Dogo Unazijua siasa za Kenya vizuri au?
Unamjua vizuri mtu anaitwa Jomo Kenyatta?
Unajua Kikuyu wewe?
Kama hujui nyamaza coz naona kazi uliyotumwa hapa sasa inakushinda
 
Mnaambiwaga na nani? Dogo Unazijua siasa za Kenya vizuri au?
Unamjua vizuri mtu anaitwa Jomo Kenyatta?
Unajua Kikuyu wewe?
Kama hujui nyamaza coz naona kazi uliyotumwa hapa sasa inakushinda



Mambo ya kusema unamjua unamjua hayahitajiki hapa, wewe kama unajua funguka hapa, tunaongelea uhusiano wa Katiba Mpya na Tume Huru ya Uchaguzi, hivyo ukumbi ni wako unaweza kufunguka kama ukipenda!
 

Mambo ya kusema unamjua unamjua hayahitajiki hapa, wewe kama unajua funguka hapa, tunaongelea uhusiano wa Katiba Mpya na Tume Huru ya Uchaguzi, hivyo ukumbi ni wako unaweza kufunguka kama ukipenda!
Anzisha Uzi wake wa kuomba msaada ueleweshwe otherwise kuna Kenya forum
 
Back
Top Bottom