Kenya Airways kusitisha safari 40 za ndege kufuatia mgomo wa marubani

Shujaa Mwendazake

JF-Expert Member
Jul 11, 2015
3,734
6,292

Zaidi ya abiria 9,000 wamekwama katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Jomo Kenyata Kenya (JKIA) jijini Nairobi na katika viwanja vingine vya ndege vya kimataifa duniani kufuatia mgomo wa marubani wa shirika la ndege la Kenya Airways.

Shirika la ndege la Kenya Airways limesema hadi safari 40 za ndege zinaweza kusitishwa katika siku ya kwanza ya mgomo wa marubani.

Mamia ya abiria wamehamishiwa katika mashirika mengine ya ndege, na wengine kupewa malazi katika hoteli jijini Nairobi wakisubiri mipango mipya ya usafiri.
Shirika hilo la ndege hata hivyo linasema linaendesha safari za ndege chache za kimataifa kwa kutumia marubani ambao sio wanachama wa chama cha marubani na ambao hawashiriki mgomo huo.

Foleni ndefu zimeshuhudiwa siku nzima ya Jumamosi huku wasafiri wenye wasiwasi wakisubiri kwa saa kadhaa kujua hali ya safari zao.

"Nilikuwa nikisafiri kwenda Mumbai kwa sababu za matibabu, na sasa ni lazima nighairi safari za ndege na uhifadhi wa hoteli, ni ghali sana," abiria mmoja aliambia BBC kwenye uwanja wa ndege.
 
Back
Top Bottom