Kelele Hoteli ya Bahari Beach

Asante kwa ushauri mzuri.

Yako mambo mengi sana yameanzia JF na leo Serikali imeyatekeleza. Hawa NEMC hata humu wapo na wamesoma hii habari tangu jana. JF NI KISIMA CHA HABARI.

Nawaomba NEMC muifanyie kazi issu hii ili tuishi kwa amani. Naamini kazi ya NEMC sio BOMOA BOMOA tu!!!!

Vitu vya kuangalia:-
1. Ni halali hotel iliyo karibu na makazi ya watu kuporomosha muziki wa maspika makubwa. Tena sauti inaambaa Bahari Beach na Kunduchi yote. Je hiyo ni haki??

2. Je usajili wa hiyo Hotel unaruhusu hicho kinachofanyika??? Usisahau Hotel hii ni Hotel ya kitalii.

3. Kuingia tu mlangoni unalipa wakati Serikali imesema beach zote ni wazi. Usisahau hapo bei ya soda tu ni issue.

4. Hotel inakodisha watu wanaofunga ndoa. Wakifanyia sherehe nje basi ukumbi unahamia sebuleni kwenye majumba ya watu.

Mimi nadhani kwa uungwana wajaribu kulifanyia kazi jambo hili. Hivi Club Billicanas ingekuwa hivi mji wa Dar ungekuwaje???

Mambo ya NEMC kusubiri Serikali za Mtaa zilalamike ni uzushii. Wajifunze kufanya kazi na jamii kwa njia zote na wawe more proactive na sio reactive.

Asanteni

Queen Esther

?
Peleke lalamiko lako ofisi ya serikali za mitaa. huku hutapata ufumbuzi
 
Queen Esther kumbe we ni mtoto wa kishua? PM tafadhali tuyajenge kidogo!
 
Hata saivi kuna kelele
Nahisi kuna live band hapo
 
Tanzania inatakiwa kuanza kuwa na sera za mipango miji kama mji wa casino wa Las Vegas, Marekani.

Na hakika wakati Bahari Beach, Kunduchi beach, Silversands n.k ''mjini Dar'' maeneo hayo wakati yakiwa mbali na meneo ya kuishi watu serikali ilitakiwa kufanya eneo hilo kuwa maalum kwa ajili ya starehe, casino, ''red district'' kama Amsterdam na huduma za mahoteli tu, lakini serikali ikaacha watu watumie maeneo hayo kuwa ya makazi ya watu na hatimaye wanaanza kulaumu ''makelele''.

Mfano mwingine eneo la Wazo Hill Dsm labda ilikuwa iwe eneo la viwanda tu lakini serikali ikatoa eneo hilo kuwa la makazi ya watu sasa, wakaazi wanapiga kelele ''uchafuzi wa hali ya hewa''.

Wakulima walikuwa na maeneo maalum, vile vile wafugaji walikuwa na maeneo maalum lakini sasa hakuna sera za namna hiyo matokeo 'mapigano'' kati ya wafugaji na wakulima.
 
LEO NI HATARI ZAIDI.

MKUTANO WA CHADEMA UNAOENDELEA HUKO YAANI UTAFIKIRI MASPIKA YAKO MAJUMBANI KWETU.
SAA HIZI ANAONGEA HALIMA MDEE DUUUU!!!

Hii sio haki kabisa. Huo mkutano wa CHADEMA inakuwa Kama tunalazimishwa kusikiliza?????? Kuna nini na hii hotel. Kulikoni kuamua kututesa na watoto wetu hivi.

Serikali tusaidieni jamani. Hao NEMC hata siwaelewi, au ndio Kama issue ya mama Lwakatare??

Queen Esther

Hata saivi kuna kelele
Nahisi kuna live band hapo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…