Acha kupotosha na kutishia watu wewe poyoyo, unaishi kwa kukariri badala ya kutafuta ukweli. Mi nawashauri watu wote walioomba hizo kazi wawe wavumilivu, kama ambavyo mngetarajia, maombi ya kazi yalikuwa mengi sana na kumbukeni ilikuwa kuelekea sikukuu za mwisho wa mwaka hivyo taratibu za uchambuzi na hatimaye kuita wasailiwa zinaendelea na huenda zikachukua muda mrefu kidogo. Ila cha kuwatia moyo tu ni kwamba, kati ya Taasisi zilizoboresha mifumo yao hasa ya ajira ni BoT, hapo kigogo wa kukubeba ni vyeti na performance yako katika usaili tu, hakuna muujiza, rushwa wala ubin! Hebu jiulizeni nyie mnaodanganywa eti ile ni sehemu ya watoto wa vigogo, ukichunguza ni asilimia ngapi ya wafanyazi wa BoT ni watoto, ndugu, marafiki au wana nasaba na hao vigogo mnaowasema? Hivi mnajua Bo Tina wafanyakazi wangapi jumla, na kati yao watoto wa vigogo ni wangapi? Na je, Benno Ndulu ni mtoto wa kigogo gani wa nchi hii? Hebu tumieni akili japo kidogo kufikiri!