"kazi ya ualimu ni kama chunvi"

"kazi ya ualimu ni kama chunvi"

Ngeme

Member
Joined
Jun 1, 2013
Posts
33
Reaction score
28
Chunvi mara zote kwenye mboga haikosi lawama,ikizidi utasikia chunvi imezidi! Ikipungua chunvi kidogo! Usipoiweka ndo kabisa zogo! Ualimu sasa umeshakua karaha tupu hivi sasa wanafunzi wakifaulu kwa wingi utackia raia wakisema wlm wamewaonesha majibu,wakifeli wengi utackia walimu siku hizi hawafundishi kabisa he! Mwl jijue we2 ni km CHUNVI fanya tu kazi zako lkn lawama kwako ni sehemu ya maisha yako na mshahara wako ni mdogo km bei ya CHUNVI pole sn Mwl.
 
CHUNVI* = CHUMVI


Mwl unafundisha darasa la ngapi ?
 
mwalimu unafundisha somo gani? primary au secondary nahitaji jibu then ntachangia hoja yako!
 
bila shaka ni mtoto wa mwalimu huyuu :shocked:
 
mwenzenu jana tu nimekutana na mwalimu mmoja hvi,, akaniambia yaani mimi siwezi kumshauri mwanangu au ndugu yangu asomee ualimu,,,kisa work load ni kubwa balaaaa,,,shule zingine unakuta mwalimu mmoja anafundisha watoto 500...duh,,,kweli nikastajabu na kuona mazingira yao ni magumu sana
 
Majanga......nimfundishe mie afeli yeye nilaumiwe mie...majanga......avute bangi zake afeli yeye eti mie sina wito...majanga.....
 
Ona mitihani ya siku hizi: Yeboyebo Primary School: Rais was Tanzania anaitwa Kikwe......(a) ta, (b) te (c) ti, (d) to (e) tu St. Marys International School: The name of the current President of The United Republic of Tanzania Hon.Dr.Jakaya Kikwete recently launched the following event: (a) new constitutional review committee (b) coup detet(c) new ministry (d) both a and c
 
Kama unawafundisha neno CHUMVI waandike CHUNVI unategemea wafaulu....!
 
na mshahara wko unakidhi mahitaji yako?au unakopa kwa mangi mwisho wa mwezi unalipa,je unaipenda kazi yako?
kingine ulienda ualimu kwa hiari au kwa kulazimishwa?jibu
 
Waalimu wazuri wanakimbilia kuwa wanasiasa kwakuwa inalipa, unafikiri tutakuwa na taifa bora.Thubutu!
 
Usimsakame sana hiyo ni typing error na au hakuna 'm' kwenye keypad yake! Hoja umeiona na kuielewa? Ndo la msingi na sio unachungulia humu kuona nani amekosea kuandika. Haya changia hoja.
 
Back
Top Bottom