Kazi ya Dr. Bilal ni MC wa serikali ya JK?

Kiwi

JF-Expert Member
Sep 30, 2009
1,054
990
Heshima kwenu wadau,

Mara kadhaa nimekuwa nikijiuliza swali kuhusu kazi ya Makamu wa Rais wa JMT, Dr. Mohamed Bilal. Job description yake kiongozi huyu wa ngazi ya juu kwenye serikali ni kuweka mawe ya msingi, kufungua makongamano, warsha na semina? Hivi hana kazi nyingine? Kila kukicha kwenye TV, magazeti na mpaka kwenye Michuzi hukosi kumwona akiwa kwenye harakati za ufunguzi ama kufunga mojawapo ya matukio kama hayo. Hivi kweli amekosekana mtu mwingine wa kufanya kazi kama hizo mpaka zifanywe na Makamu wa Rais? Ama ndiyo 'job description' yake inavyosema? Kuna haja gani basi ya kupokea mshahara na marupurupu kibao ya cheo cha Makamu wa Rais kama kazi yake ni sawa na MC kwenye tafrija ambazo kwa Tanzania yetu haziishi?
 
Kazi kubwa ya Makamu Raisi akiwepo ni mambo ya Mazingira ambayo naona Dr. Omary Ali Jumaa tu ndio aliiweza vizuri!
 
Wa Zanzibar ndani Serikali ya Muungano wanakuwa assigned kazi za Hovyo hovyo Kabisa...
 
vyeo vya kuweka ili watu fulani wanyamaze bwana!!!
 
Heshima kwenu wadau,

Mara kadhaa nimekuwa nikijiuliza swali kuhusu kazi ya Makamu wa Rais wa JMT, Dr. Mohamed Bilal. Job description yake kiongozi huyu wa ngazi ya juu kwenye serikali ni kuweka mawe ya msingi, kufungua makongamano, warsha na semina? Hivi hana kazi nyingine? Kila kukicha kwenye TV, magazeti na mpaka kwenye Michuzi hukosi kumwona akiwa kwenye harakati za ufunguzi ama kufunga mojawapo ya matukio kama hayo. Hivi kweli amekosekana mtu mwingine wa kufanya kazi kama hizo mpaka zifanywe na Makamu wa Rais? Ama ndiyo 'job description' yake inavyosema? Kuna haja gani basi ya kupokea mshahara na marupurupu kibao ya cheo cha Makamu wa Rais kama kazi yake ni sawa na MC kwenye tafrija ambazo kwa Tanzania yetu haziishi?
Saa zingine usitake kutuonesha kuwa unachuki na Makamu wa Rais! Chukua KATIBA YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA YA MWAKA 1977.Kisha soma ibara ya 47.Huyo mzee hakujiweka mwenyewe katika nafasi ile!


:boxing:
 
cheo cha makamu wa raisi mara nyingi hutumika kama kupunguza sintofahamu katika pilika za kisiasa......hasa kwa CCM....lakini kwa mujibu wa katiba yetu ya sasa huwa tunasahau kuwa makamu wa raisi ndiyo huwa raisi wa jmt pale ambapo raisi hana uwezo wa kuongoza tena.......tunatakiwa tuitafakari kwa kina nafasi hii ya pili kwa ukubwa katika nchi yetu.....
 
Saa zingine usitake kutuonesha kuwa unachuki na Makamu wa Rais! Chukua KATIBA YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA YA MWAKA 1977.Kisha soma ibara ya 47.Huyo mzee hakujiweka mwenyewe katika nafasi ile!


:boxing:

Sina chuki wala sikufikiria ya kuwa Mzee Mohamed Gharib Bilal amejiweka mwenyewe kwenye hiyo nafasi. Rejea swali langu, kwa nini katika kazi zote ambazo kwa heshima aliyonayo na wadhifa wake serikali imeamua kumweka katika kiwango kama hicho? Kwa mawazo yangu yeye ni mtu muhimu sana hastahili kushushwa wadhifa kiasi hicho na kugeuzwa 'Master of Ceremony' wa serikali ya JMT. Ndiyo maana nikauliza kwa wadau ikiwa pamoja na wewe, kama hivyo ni sahihi kumtumia Makamu wa Rais wa JMT kama mtu wa kukata utepe, kufungua makongamano, kuweka mawe ya msingi n.k. Kama kudhalilishwa basi anadhalilishwa na serikali. Usinitupie madongo mimi kwa kutumia nafasi yangu halali ya kidemokrasia kuuliza kama hivi inakubalika kwa Dr. Bilal kutumiwa vibaya namna hii. Nilimalizia kwa kuuliza kama wanaona hatuhitaji mtu wa kushika wadhifa kama huo basi ni bora wakifute hicho cheo, kuliko kumlipa mshahara wa Makamu wa Rais kama kazi wanayofikiria kumpa ni duni ambayo hata mtu yeyote anaweza kuifanya!
 
Budget yake na ofisi yake yote kuanzia staff,safari,mikasi,security,housing,magari(Mercedes,cruisers),chartered Jets etc ni billions,na anachofanya hakieleweki kama huu sio ufisadi wa mchana kweupe ni nini???...budget yake kwa mwaka ni zaidi ya billion 50
 
FUNGU 31: OFISI YA MAKAMU WA RAIS
60. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2011/12, naomba Bunge lako Tukufu, liidhinishe makadirio ya matumizi ya Ofisi ya Makamu wa Rais, Fungu 31, ya shilingi 52,822,422,000/=. Kiasi hicho kinajumuisha shilingi 1,323,754,000/= mishahara ya watumishi, shilingi 39,088,289,000/= fedha za Matumizi Mengineyo na shilingi 12,410,379,000/= fedha za Matumizi ya Maendeleo. Aidha, fedha za Maendeleo zinajumuisha fedha za ndani shilingi 6,067,014,000/= na fedha za nje shilingi 6,343,365,000/=.
 
Kwa lugha nyingine thamani yake ya kutembeza mikasi kwa mwaka na billion 50 ni sawa na kujenga daraja la Kigamboni,kwa miaka mitano na billion zaidi ya 400 kwa mikasi yake ile foleni ya Dar ingekwisha.....huu ni wizi wa raslimali za wananchi,hiyo post waiondoe au wakate 95% of their budget.
 
Mleta mada umeleta hii mada kwa muda mufaka binafsi huwa nakerwa na shughuli anazopewa makamu wangu wa raisi.Hizi shughuli haziendani kabisa na hadhi yake
 
Back
Top Bottom