Kazi na dawa......au?

Kazi na dawa......au?

Indume Yene

Platinum Member
Joined
Mar 17, 2008
Posts
2,968
Reaction score
727
Jamani,
Nimekuwa nikiangalia picha kadhaa tangu zile za Loliondo hadi hii ya Tabora. Nimeona askari wetu ambao ni binadamu kama sisi wakienda kupata vikombe wakiwa kwenye magwanda. Swali, je hawa askari wanatumia magwanda kupata short-cut wasisimame kwenye foleni, au wakishapata vikombe wanaendelea kuangalia usalama wa raia? Utaona hapo kuna askari wangapi vile.........!!

Nawakilisha.

DSC02977.JPG
 
Nao ni binadamu kama sisi jamani wana ugua, wana kufa, wanafiwa, wana cheka, wahuzunika wanalia kama wanadamu wengine kuwa polisi sio exemption ya kuwa na magonjwa na matatizo ya kidunia.
 
Nao ni binadamu kama sisi jamani wana ugua, wana kufa, wanafiwa, wana cheka, wahuzunika wanalia kama wanadamu wengine kuwa polisi sio exemption ya kuwa na magonjwa na matatizo ya kidunia.

Kwenye maelezo yangu hapo juu naamini nimesema kuwa hao polisi ni binadamu kama sisi, wana matatizo kama yetu sisi ingawa hawapendi kukiri hadharani kama vile mishahara kiduchu, maisha magumu, hawapewi haki zao zote. Mimi nilichouliza: Je hawa polisi wanatumia gwanda kuruka kiunzi cha foleni au wakimaliza kupata kikombe wanaendelea kuangalia usalama wa raia?
 
Jamani,
Nimekuwa nikiangalia picha kadhaa tangu zile za Loliondo hadi hii ya Tabora. Nimeona askari wetu ambao ni binadamu kama sisi wakienda kupata vikombe wakiwa kwenye magwanda. Swali, je hawa askari wanatumia magwanda kupata short-cut wasisimame kwenye foleni, au wakishapata vikombe wanaendelea kuangalia usalama wa raia? Utaona hapo kuna askari wangapi vile.........!!

Nawakilisha.

DSC02977.JPG
Baada ya hapo atasahau kitu kidogo? Haya ni maigizo!
 
Baada ya hapo atasahau kitu kidogo? Haya ni maigizo!

Yohana mbatizaji hakuwaombea hawa, aliwaambia straight "...msiwashitaki watu kwa uongo na toshekeni na mishahara yenu" maana hawa ndiyo ugonjwa wao.
 
Sidhani kama wanaangalia usalama baada ya kupata kikombe. Mifano ipo kwenye daladala na viwanja vya michezo hasa mechi kubwa kubwa. Dezo kwao ni kama kawa!
 
Nawakilisha.

DSC02977.JPG


Wako wana usalama 4 hapo kwa mpigo, 2 mbele na 4 nyuma kwenye ukuta. Sasa hatujui kama kuna wengine waliokuwepo wakiangalia usalama wakati hawa wakisubiri kikombe.
 
Ukisikia viongozi wa serkali wamechoka ni pamoja na kushiriki imani kama hz, sasa wasio uelewa unategemea watafanyeje?
 
Back
Top Bottom