Mwinjilist mtume nabii
JF-Expert Member
- Feb 21, 2015
- 2,437
- 1,100
Jamani hii ni hatari, ebu fuatilieni mjifunze, mke na mume wanaishi pamoja na wanapendana tu, sasa huyu mke ana rafiki yake wa karibu sana, ambaye hajaolewa na anamwonea wivu sana mwenzake. Kwani na yeye alikuwa anapenda sana kuolewa.
Sasa kilichotokea huyu rafiki akamfuata mume wa yule dada na kumwambia uongo eti mkeo amekwenda kwa mganga na amepewa dawa kaambiwa akupake mgongoni leo usiku ukiwa umelala ili usiwe na sauti.
Na yule mume kwa kuwa anajua ni rafiki wa karibu sana wa mkewe akaamini, akalichukulia serious na akasema nitakuwa makini nione. Baada ya hapo yule rafiki akamfuata rafiki yake mke wa jamaa akamwambia rafiki yangu hii ni siri ya ndani mimi nakupa tu kwasababu ni rafiki wa damu, unajua mumeo ana mkia mgongoni?
Amewekewa na mganga ili ww usimfuatilie katika mambo yake, basi na huyu mke akaamini akasema leo usiku nitamkagua. Kwahiyo sasa wote wakawa makini bila kujijua. Jamaa akawa anakoroma,mwanamke akaanza kumpapasa na ghafla mume akaamka na ndio ikawa mwisho wa ndoa, mume kwa fadhila kamchukua rafikiye.
Sasa kilichotokea huyu rafiki akamfuata mume wa yule dada na kumwambia uongo eti mkeo amekwenda kwa mganga na amepewa dawa kaambiwa akupake mgongoni leo usiku ukiwa umelala ili usiwe na sauti.
Na yule mume kwa kuwa anajua ni rafiki wa karibu sana wa mkewe akaamini, akalichukulia serious na akasema nitakuwa makini nione. Baada ya hapo yule rafiki akamfuata rafiki yake mke wa jamaa akamwambia rafiki yangu hii ni siri ya ndani mimi nakupa tu kwasababu ni rafiki wa damu, unajua mumeo ana mkia mgongoni?
Amewekewa na mganga ili ww usimfuatilie katika mambo yake, basi na huyu mke akaamini akasema leo usiku nitamkagua. Kwahiyo sasa wote wakawa makini bila kujijua. Jamaa akawa anakoroma,mwanamke akaanza kumpapasa na ghafla mume akaamka na ndio ikawa mwisho wa ndoa, mume kwa fadhila kamchukua rafikiye.