Wakati huo huo, Katibu Mkuu wa chama hicho, Bw. Yusuf Makamba alisema ushindi wa mwanawe, Bw. January Makamba katika Jimbo la Bumbuli ulikuwa wa lazima na iwapo angeshindwa ilikuwa ni fedheha kwake na kwa chama hicho.
Alisema kijana wake alipokuwa akigombea kuchaguliwa na chama hicho kukiwakilisha katika Uchaguzi Mkuu hakuwa January kama January bali alikuwa mtoto wa Katibu Mkuu wa CCM, hivyo ilikuwa lazima ashinde.
Source-Majira
Jamani hata kauli za kisiasa zinakua chuki? Tulisema humu kuwa CHADEMA lazima itashinda, tulikuwa seriuos au ni kauli za kisiasa. Mengine yaacheni hayana maana hapa!