Kauli ya Magufuli inathibitisha pasipo shaka kuwa anaingilia mhimili wa mahakama

Mystery

JF-Expert Member
Mar 8, 2012
15,484
30,159
Tumemsikia wenyewe kwa masikio yetu, katika ufunguzi wa maktaba mpya hapo Chuo kikuu cha Dar-es-salaam, Rais Magufuli akitamka waziwazi huku akimsifia Lowassa na kudai kuwa huyo ni kiongozi wa mfano na kumpa ujumbe kuwa akawaeleze viongozi wenzake wajifunze ku-behave ama sivyo wataishia gerezani!

Kwanza kauli hiyo siyo sahihi kabisa, kwa kuwa ni chombo cha mahakama pekee kinachoweza kuthibitisha tuhuma ya mtu

Kwa kutoa kauli hiyo tayari yeye keshawahukumu viongozi wa Chadema kuwa wana hatia!

Tunajua kuwa Mwenyekiti wa chama kikuu cha upinzani na Mbunge wa kuchaguliwa na wananchi wa jimbo la Hai, Freeman Mbowe na mbunge mwenzake wa Jimbo la Tarime mjini, Esther Matiko, wanaendelea kusota gerezani segerea kwa kilichodaiwa na mahakama ya Kisutu kuwa wameidharau mahakama hiyo

Hivi kwa kutamka maneno hayo Rais wa nchi haoni kuwa anaingilia mhimili wa mahakama katika kufanya maamuzi yake na kuonyesha kuwa hata kufutwa kwa dhamana ya kina Mbowe imetokana na influence yake??

Hivi Rais haijui kanuni ya kimahakama ambayo inazuia kutoa kauli kwa kesi inayoendelea mahakamani??

Kama anaijua iweje yeye anatoa kauli ya vitisho kuwa viongozi wenzake na Lowassa wataishia gerezani, huku akijua kuwa kuna kesi inayoendelea Kisutu na kuna viongozi wa Chadema ambao dhamana zao zimefutwa kwa njia ya utata??

Hivi viongozi hao wa Chadema si walishaweka pingamizi la kumkataa Hakimu anayeendesha kesi yao??

Kwa kawaida unapokataliwa na washitakiwa kuendelea na kesi yao inabidi wewe Hakimu ukubaliane na uamuzi huo wa washitakiwa na ukae pembeni ili Hakimu mwingine ateuliwe kuendelea na kesi hiyo

Hivi Hakimu Mashauri anaweza kutupa sababu za kukataa kujitoa kuendelea na kesi hiyo ambayo washitakiwa wenyewe wamesema hawana Imani naye kutokana na mwenendo anaouunyesha wa kupendelea upande mmoja??

Mwenendo wa kesi ya akina Mbowe na kauli iliyotolewa na Rais Magufuli kuwa viongozi wa Chadema wasio-behave wataishia jela ni kauli mbaya kabisa kuwahi kutolewa na Rais was nchi hii

Hivi viongozi wengine watakaofikishwa mbele ya mahakama watakuwa na Imani gani na mahakama baada ya kauli hii ya Rais??

Mungu ibariki Tanzania
 
Mbowe yupo Mahabusu Kwa kosa la kukiuka dhamana yake, alipewa Masharti kadhaa Moja wapo Ni kutosafiri nje ya Nchi bila ya Ruhusa ya Mahakama Na akakubaliana Na sharti Hilo ndipo akapewa dhamana, kashindwa kutii Masharti ya dhamana yake Mwenyewe Kwa hiyari yake sio Kila kitu kumsingizia Rais
 
Ametoa ushauri tu hakuingilia
Unaijua kanuni ya kimahakama inayopiga marufuku kuongelea kesi inayoendelea mahakamani??

Ni kwanini Rais ameongelea kuendelea kuwaweka viongozi wa Chadema ndani, wakati akijua kuwa kesi hiyo bado inaondelea na haijafanyiwa Judgement??

Huoni kwa kutoa kauli ile hadharani ana-influence maamuzi anayotaka yeye Rais ili mahakama iyatekeleze??
 
Anajisahau sana wakati mwingine, hasa akiwa kwenye hadhara, kitendo cha KUTISHIA (THREATS) kama kiongozi hakileti picha nzuri na wala hakifai. Hasa kutishia kufunga watu gerezani kwa wale wanaoi kosoa serikali.

Je raia wote wakiamua kua kama viongozi wa upinzani, na kuikosoa serikali, ataweza kufunga nchi nzima gerezani???
 
Mbowe yupo Mahabusu Kwa kosa la kukiuka dhamana yake, alipewa Masharti kadhaa Moja wapo Ni kutosafiri nje ya Nchi bila ya Ruhusa ya Mahakama Na akakubaliana Na sharti Hilo ndipo akapewa dhamana, kashindwa kutii Masharti ya dhamana yake Mwenyewe Kwa hiyari yake sio Kila kitu kumsingizia Rais
Wewe unasemaje kuwa kashindwa kutii wakati wakili wake alionyesha hata vithibitisho vya sababu ya Mbowe kutoweza kuhudhuria mahakamani??
 
Wewe unasemaje kuwa kashindwa kutii wakati wakili wake alionyesha hata vithibitisho vya sababu ya Mbowe kutoweza kuhudhuria mahakamani??

Wewe taja Hapa sababu Moja tu Moja tu ya msingi ya Mbowe kwenda Marekani, Belgium Na kwingineko bila ya Yeye Au wakili wake kufika Kisutu Mahakamani kuomba ridhaa ya Mahakama
 
Hivi Rais haijui kanuni ya kimahakama ambayo inazuia kutoa kauli kwa kesi inayoendelea mahakamani??...... Mbona Hyo Kanuni Inayokataza haujaitaja? Na Hyo Kanuni Inamkataza Nani?
 
Unaijua kanuni ya kimahakama inayopiga marufuku kuongelea kesi inayoendelea mahakamani??

Ni kwanini Rais ameongelea kuendelea kuwaweka viongozi wa Chadema ndani, wakati akijua kuwa kesi hiyo bado inaondelea na haijafanyiwa Judgement??

Huoni kwa kutoa kauli ile hadharani ana-influence maamuzi anayotaka yeye Rais ili mahakama iyatekeleze??
Tutajie Hyo Kanuni
 
Hivi Rais haijui kanuni ya kimahakama ambayo inazuia kutoa kauli kwa kesi inayoendelea mahakamani??...... Mbona Hyo Kanuni Inayokataza haujaitaja? Na Hyo Kanuni Inamkataza Nani?
Inamkataza mtu yeyote nchini, bila kujali wadhifa wake ndani ya Jamii
 
Wewe unasemaje kuwa kashindwa kutii wakati wakili wake alionyesha hata vithibitisho vya sababu ya Mbowe kutoweza kuhudhuria mahakamani??
Ni Vithibitisho Gani Wakili Wake Alionyesha? Umewahi Kuona Ruling Uliyotolewa Juzi Na Kisutu?
 
Anajisahau sana wakati mwingine, hasa akiwa kwenye hadhara, kitendo cha KUTISHIA (THREATS) kama kiongozi hakileti picha nzuri na wala hakifai. Hasa kutishia kufunga watu gerezani kwa wale wanaoi kosoa serikali.

Je raia wote wakiamua kua kama viongozi wa upinzani, na kuikosoa serikali, ataweza kufunga nchi nzima gerezani???
Ikulu ni mzigo - JK NYERERE
 
Back
Top Bottom