tatizo jf siku hz mmekuwa mashabiki wa simba na yanga
kuna recodi zake za kipindi za kampeni kabla hajaanza kupigwa pigwa na polisi ukiyasikiliza yanaconnection na haya aliyoyaongea kwenye record yake hii hivyo sidhani kama kupigwa ndiyo kumesababisha labda yameongeza...Nafikiri kipigo alichopata kwa kutolewa na polisi kwenye ukumbi wa jiji pamoja na matumizi ya uongo ya CCM dhidi ya CHADEMA yanamfanya Lema kuwa chuma cha pua. Misukosuko huongeza ujasiri, Jamaa anajua sana ku-connect na voters pamoja na watanzania na ninafikiri CCM wakiona hivi ndiyo wanamwona ni mchochea vurugu. Big up Lema
Hakika umenifanya nifumbue macho, najiuliza CHITAMBALA wa mbeya aliyajua haya au ndio ana agenda gani ya siri na CCM?
Kwanza kwa Lema, ulipotaka kutoa ushahidi kuwa Pinda kadanganya bungeni spika akakataa usilonge mjengoni bali mkaonane 'faragha' na huko umpe mambo yako. Na Lissu pia majuzi nimekuona umeng'aka na Ngeleja kudanganya na wewe pia umealikwa 'faraghani' ukampe spika mambo yako; sasa swali - huko faraghani mlifanya nini na matokeo yake ni yapi? Maana huu utakuwa uhuni sasa, waziri anadanganya na nyinyi mambo mnamalizia faraghani.Naombeni jibu hapa jukwaani. Mbona Zitto aliposhambulia uongo wa Karamagi alipigwa chini vikao kibao na hakuitwa faraghani? au ni kwa sababu enzi zile spika hakuwa demu?