Kauli tata za Mama Salma Kikwete

Kauli tata za Mama Salma Kikwete

Sitakagi hata kumsikiliza , anaongea kama anafundisha watoto .
 
Ukiona watu wanalilia mabadiliko, ujue ni CCM, kweli ukiona kila kitu ujue ni CCM
 
Hahahhhhhhhhh mbavu zinauma! Mtoa mada umetufurahisha mnoooooooo! Uchaguzi kampeni na viburudisho! Huku tunaita kukurupuka! Acha aweke audio au video ajisikie mwenyewe labda atagundua. Sasa magari na magorofa ndio maisha mazuri no wonder mkulu alisema bora maisha.
 
Uliyegemea usikie la maana kutoka kwa mtu anayevaa vitenge vya ccm!!!be serious jamaa.
 
Huyo mwalimu wa darasa ala saba ana kazi

alikuwa na uwezo wa kufundisha Darasa la Saba huyu? Naona kama alikuwa anapayuka alipokuwa kule lindi!

Inawezekana siyo kosa lake kwan Jei huwa mitaa ya Tz hajui zaidi ya mamtoni

ila siyo kosa lao ni ccm tu

mabadiliko ni lazima ccm haina hadhi ya kuongoza taifa letu
 
Acha uzushi uelewa wako mdogo unapelekea kuleta mada zisizo na mashiko...
 
Kwa kuwa mlimmiss sana mumewe tumewaletea mama tena..
 
Ukitafakari sana alichosema mama kina maana kubwa.
CCM imetawala kwa mingi kwa lugha rahisi ni kuwa Serikali ya CCM inayopitisha bajeti kila mwaka ndio iliyoamua na inayoendelea kuamua mustakbali wa maisha Watanzania.

Sasa kama imefanya vyema mimi sijui ila kama imefanya vibaya inabidi itafakari.
Miaka hamsini baada ya Uhuru hizi ni aibu
1.umaskini uliopindikia - tunaikumbatia TASAF itatue tatizo kwa kuwapa watu fedha
2.huduma duni za afya - bado maeneo mengi hayana zahanati na huko zilizopo hazina.dawa za kutosha
3.kiwango duni cha elimu : wanafunzi.wengi wanamaliza elimu ya msingi wakiwa hawajui kusoma na kuandika. Matokeo mabovu ya kidato cha nne.

Nilikuwa nikisikia vita dhidi ya Ujinga, Maradhi na Njaa.....
Nahisi tumeshashindwa hii vita.
 
Back
Top Bottom